Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 61,211
- 99,960
Kuna Athari kubwa sana kwa Jeshi la Polisi kuzunguka na magari na silaha mtaani. Nimejaribu kuainisha sababu kadhaa chache;
Moja, lengo lao ni kuleta hofu kwa Wananchi lakini hali hii hujenga usugu na mazoea kuwaona kuwa si lolote si chochote. Mbinu hii ni mbaya sana.
Pili, huweza kuwajengea wananchi ujasiri wa kukabiliana nao, ni hatari sana maana kama kweli atakuepo mtu mwenye nia ovu, anaweza kuangalia the way wanavyojipambanua na mtu huyo akajenga namna ya kuwashambulia Askari. Kwa mfano, Jana nimekutana nao kigogo, wako kwenye gari kama sita! Ni rahisi sana kushambuliwa kama atakuepo mtu mwenye nia ovu.
Tatu, ili uweze kushambuliwa vizuri ni lazima umjue vizuri adui yako, yale magari yao ambayo wamejifunga mikanda ikitokea wamefanyiwa ambush watakumbuka saa ngapi kufungua seat belts na kushambulia?
Nne, askari wa Jana wengi hawana miili ya kazi, sijajua upande wa akili, lakini kwa miili ile kweli wananchi wakilianzisha hakuna atakayepona. Wajitahidi mazoezi.
Tano, ni wachache sana! Wananchi wa Kigogo peke yao wangeweza kuziba barabara na kuwaweka mtu kati tungepoteza Askari wetu kizembe sana.
Ushauri wangu, kama lengo ni kuwatisha wananchi basi tujue tumepanga mkakati wa hovyo saana maana unampa adui ABC kuhusu wewe.
Tujitafakari, umwagaji damu ni hatari kwetu sote. Tuipende nchi yetu
Moja, lengo lao ni kuleta hofu kwa Wananchi lakini hali hii hujenga usugu na mazoea kuwaona kuwa si lolote si chochote. Mbinu hii ni mbaya sana.
Pili, huweza kuwajengea wananchi ujasiri wa kukabiliana nao, ni hatari sana maana kama kweli atakuepo mtu mwenye nia ovu, anaweza kuangalia the way wanavyojipambanua na mtu huyo akajenga namna ya kuwashambulia Askari. Kwa mfano, Jana nimekutana nao kigogo, wako kwenye gari kama sita! Ni rahisi sana kushambuliwa kama atakuepo mtu mwenye nia ovu.
Tatu, ili uweze kushambuliwa vizuri ni lazima umjue vizuri adui yako, yale magari yao ambayo wamejifunga mikanda ikitokea wamefanyiwa ambush watakumbuka saa ngapi kufungua seat belts na kushambulia?
Nne, askari wa Jana wengi hawana miili ya kazi, sijajua upande wa akili, lakini kwa miili ile kweli wananchi wakilianzisha hakuna atakayepona. Wajitahidi mazoezi.
Tano, ni wachache sana! Wananchi wa Kigogo peke yao wangeweza kuziba barabara na kuwaweka mtu kati tungepoteza Askari wetu kizembe sana.
Ushauri wangu, kama lengo ni kuwatisha wananchi basi tujue tumepanga mkakati wa hovyo saana maana unampa adui ABC kuhusu wewe.
Tujitafakari, umwagaji damu ni hatari kwetu sote. Tuipende nchi yetu