Ni halali kwa wakuu wa Mikoa na wilaya kuvaa nguo za CCM?

Ustaadh

JF-Expert Member
Oct 25, 2009
413
19
Kuna baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya ambao huvaa nguo zinazoshabihiana na rangi za bendera ya chama tawala wakati wa kuwapokea viongozi wa kichama. Hivi ni halali wao kufanya hivyo na hasa ukizingatia wao ni wanaongoza wananchi wote bila kujali itikadi za vyama? Picha kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya akiwa na Bw. Kinana na picha kulia ni Mkuu wa mkoa wa Tabora akiwa na Bw. Nape Nnauye.
attachment.php
 

Attachments

  • Mby1.jpg
    Mby1.jpg
    43.9 KB · Views: 337
  • TBR1.jpg
    TBR1.jpg
    46.2 KB · Views: 1,551
Hawa ni viongozi wa CCM hawana tofauti na mabalozi wa nyumba kumi wa CCM vijijini
 
Hawa ni viongozi wakisiasa wanaomuwakilisha raisi,wanahaki ya kuvaa sare za CCM
 
Kuna baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya ambao huvaa nguo zinazoshabihiana na rangi za bendera ya chama tawala wakati wa kuwapokea viongozi wa kichama. Hivi ni halali wao kufanya hivyo na hasa ukizingatia wao ni wanaongoza wananchi wote bila kujali itikadi za vyama? Picha kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya akiwa na Bw. Kinana na picha kulia ni Mkuu wa mkoa wa Tabora akiwa na Bw. Nape Nnauye.
mkuu wa mkoa anashiba wakati ndugu zake wanaoishi Natitional housing tabora wana njaa
 
Kumbuka hao ni viongozi wa CCM hivyo hawawezi kujitofautisha nao na hawawatumikii wananchi bali CCM. Kweli Watanzania tunahitaji mabadliko makubwa sana.
 
Hivi hawa wakuu wa mikoa na wilaya kwenye katiba mpya wapo?kwa waliofanikiwa kuperuz rasimu ya Warioba
 
Kuna baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya ambao huvaa nguo zinazoshabihiana na rangi za bendera ya chama tawala wakati wa kuwapokea viongozi wa kichama. Hivi ni halali wao kufanya hivyo na hasa ukizingatia wao ni wanaongoza wananchi wote bila kujali itikadi za vyama? Picha kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya akiwa na Bw. Kinana na picha kulia ni Mkuu wa mkoa wa Tabora akiwa na Bw. Nape Nnauye.

Asha Mtwangi mjumbe wa bunge maalum la katiba katika kundi lile la 201, je huko anafanya nini?
 
Kuna baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya ambao huvaa nguo zinazoshabihiana na rangi za bendera ya chama tawala wakati wa kuwapokea viongozi wa kichama. Hivi ni halali wao kufanya hivyo na hasa ukizingatia wao ni wanaongoza wananchi wote bila kujali itikadi za vyama? Picha kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mbeya akiwa na Bw. Kinana na picha kulia ni Mkuu wa mkoa wa Tabora akiwa na Bw. Nape Nnauye.

Mpendwa Ustaadh,

Kimuundo, kama ulipata bahati ya kusoma masomo ya Siasa (kabla hayajabadilika kuwa uraia), wao pia ni makada wa chama. Na kazi yao ya kwanza ni kusimamia utekelezaji wa ilani ya chama, katika maeneo yao! Kwa hiyo majibu ya swali lako ni ndiyo, wana haki ya kuvaa hizo uniform. Kama ni watumishi wa nanchi wote, sidhani.

Kwa sasa kuna mgongano wa kimuundo kidogo. Kwamba haohao uliowataja wanabeba kofia mseto. Nusu wanaonekana kwa sura ya chama na nusu kama serikali. Hii ndiyo inayopelekea wao kulipwa kwa fedha za serikali. Ni mwendelezo wa yale mabo mengi yanayofanya CCM iwe ya kihuni.

Kimsingi nafasi hizo ni kati ya nafasi ambazo zikifutwa taifa halitakuwa na hasara,wala halitapungukiwa.Ni nafasi kama hizi zinazotakiwa kufutwa ili fedha zote za mishahara, magari mafuta na wafanyakazi wa ofisi hizo zikachangie bajeti ya Serikali ya Muungano, ambayo kuna watu wanadai itakuwa gharama kuiendesha mpaka wanajeshi watagoma na kupindua serikali! Kimsingi mtendaji mkuu wa wilaya na mkoa ni Mkurugenzi na hiyo ndiyo figure rasmi ya kiserikali. Vinginevyo isingewezekana kumweka Nape kuwa mkuu wa wilaya pamoja na uhaba wa elimu na busara, lakini bado alijitutumua. Is not a big deal!
 
Last edited by a moderator:
Mbowe analipwa fedha za UMMA pia lakini anafanya kazi za UKAWA.

Kwa hiyo unatakaje? Kwamba katika nchi hii yenye siasa za vyama vingi, kila chama kiweke makada wake wilayani na mkoani? Kwa hiyo na CHADEMA, NCCR, CUF nazo ziweke wakuu wa wilaya?

Tuna tatizo serious la muundo wa uongozi na katiba zetu za vyama. Na haya ndiyo mambo yanayopaswa kujadili humu. Siyo matusi na vijembe kama wengi wetu tunavyopenda kufanya!

Hivi kuna mtu amewahi kufikiria kuwa ofisi za Mkuu wa Mkoa na Wilaya ni mzigo usio na ulazima wala umuhimu kwa serikali? Kuna haja ya kuwa na Liaison wa chama wilayani na mkoani kwa gharama za serikali? Kuna mtu amewahi kufikiria,kwa mfano ofisi hizo zikifungwa kwa nchi nzima, taifa linaokoa shilingi ngapi? Na kunamtu amewahi kufikiria kwa mfano fedha hizo zilipelekwa katika sekta nyingine kama afya, tunasaidia wagonjwa wangapi, au tunawasogezea huduma Watanzania wangapi? Najua kufungwa ofisi hizo kutasababisha wengi kupoteza ajira, na ni kweli it is tragic and paining. But kunahaja gani ya kuwa na ajira bila tija? Siyo tu uwe umeajiriwa, ila pia ni ajira yako inalisaidia nini taifa!

Mambo kama haya, pamoja na mengine kama ya ufisadi, wizi wa makusudi, ujangili, madawa ya kulevya na kulindana, ndivyo vinanifanya niamini kuwa CCM na serikali yake, haina mpango wowote wa kuleta maendeleo wala mabadiliko katika nchi hii. Kwa sababu haya mambo yanaonyesha dhahiri kuwa CCM haiko serious. Vinginevyo haiwezekani kwa watu serious,kuendelea kutuweka kwenye matumizi yasiyo ya msingi, Kuendelea kukumbatia mafisadi wanojulikana na ushahidi upo, kuendelea kukaa na wafanyabiashara haramu wa madawa ya kulevya wakati Rais ameshasema majina anayo, kuendelea kuwa na wezi wa fedha za umma kama EPA mitaani huku haijulikani hata kama fedha ni kiasi gani zimerudishwa, na wala haiwezekani kwa watu serious kuwaacha majangili wanadunda huku Rais anajigamba kuwa wanfahamika!

Kama kuna mtu anadhani maendeleo yataletwa kwa mtindo huu,mimi siyo mmoja wao. Na najua wengine wanajua kuwa nchi ina-colapse, ila kwa kuwa wao ni miongoni mwa wanofaidi hawaoni kuwa ina hasara kwao binafsi. Lakini kama kuna anayefikiria kuwa atakuwa salama, yeye kama tajiri kati ya maskini wengi, huyo mtu anatakiwa kufikiria upya. Kwa sababu ukweli ni kuwa hakutakuwa na salama!
 
Hawa ni viongozi wakisiasa wanaomuwakilisha raisi,wanahaki ya kuvaa sare za CCM

Acha hizo.hawana haki ya kuvaa nguo hizo maana mishahara yao hawagharamiwi na ccm bali kodi za wananchi wenye vyama na wasio na vyama.

Na hivi vyeo havina haja ya kuwepo maana hawana kazi mikoani na wilayani zaidi ya kuvuja jasho la walalahoi bure.
 
Mambo mengine ukichunguza sana unaweza ukaua mtu bure kipindi cha nyerere Haya mambo hayakuwepo kabisa
Wakati ule kulikuwa na chama kimoja tu kilichoshika hatamu barabara. Haya mambo yasingekuwapo kwani wakuu wa mikoa walikuwa ndio makatibu wa chama mikoani. Bahati mbaya tumeendelea na mfumo huohuo hadi sasa kasoro tu hawa wa sasa sio makatibu bali ni makada nambari moja wa chama tawala.
 
Kumbuka hao ni viongozi wa CCM hivyo hawawezi kujitofautisha nao na hawawatumikii wananchi bali CCM. Kweli Watanzania tunahitaji mabadliko makubwa sana.

Wakuu wa Mkoa na Wilaya wanapewa uongozi huo kama fadhila toka kwa Rais wa CCM, Wengi wao ni wanachama wa CCM lakini hawana elimu ya darasani wala hekima ya kawida (Kumbuka yule mkuu wa wilaya aliyewacharaza mboko walimu kule Bukoba) halafu pia hawana hata elimu ya taaluma kama Uchumi, Sociology, Planning and management, Public Relations, Diplomacy, Laws ...etc hivyo ni lazima wao wajikombe kwa Viongozi wa Chama cha CCM ambao wamewapa kula yao, mambo yote haya ya kijinga jinga hayatakuwepo pindi tukipitisha Rasimu ya Tume ya Warioba kama ilivyo bila kuchakachuliwa
 
Kabla huijajiuliza swali gumu kama hili yafaa kwanza kujiuliza Tanzania ni nchi inayooongozwa kwa kufuata ideology ipi...
Though inaaminika kwamba Tanzania ni nchi inayofuata mfumo wa vyama vingi ila hiyo ipo tu kwenye makabrasha...tunafuata Ideology ya Nyerere ya mfumo wa Chama kimoja cha siasa! Kwa ukweli huo sijui kama kuna sababu ya kustaajabu pale viongozi wa kiserikali wanapoamua kutembeza ilani ya chama chao!
 
Back
Top Bottom