Nchi kuwa na Mwanasheria mashuhuri asiye na uzalendo ni hasara kubwa sana
Huyu ni hatari kwa taifa maana huwa mchumia tumbo na mbinafsi, aweza asionekane kuwasaidia hawa wezi lakini akawaibia siri zetu na kuwapa mbinu mbalimbali za kutusumbua.
Ni aibu kubwa kwa TLS kuongozwa na bwana huyu, ambae badala ya kusaidia nchi namna ya kufanya ili nchi ilipwe na hawa wezi, yeye anakuwa upande wao na kumtisha rais kwamba atashitakiwa.
Mtu wa namna gani huyu, Tundu Lisu uzalendo wako uko wapi. Ni nini umuhimu wa sheria yako kwa nchi yetu?
You are a good lawyer who doesn't care when the isue is for public interest.
Kwa hili kama hauko upande wetu, kutetea maslahi ya nchi yetu ni bora ukae kimya utuachie tu pale tutakapoishia.
Mungu wetu ni wakili wa haki namba 1 atatutetea na tutashinda kwa imani.
Uzalendo ni pamoja na kuwasikiliza wengine, tangu miaka nenda rudi WAPINZANI wanaililia mikataba hii ijadiliwe Bungeni na hasa kitaifa ili na sisi wa darasa la saba tuione tena itafasiriwe kwa kiswahili, lakini CCM walikataa kata kata.
Kwa namna yoyote ile unavyotaka kujinasua kwenye mtego ni lazima uwe makini mno kujinasua vinginevyo ukikurupuka vibaya unaweza ukajimalizia hapo hapo.
Sasa process za kujitegua kwenye mtengo ndiyo zile za kuwashirikisha wabunge werevu wa sheria, wanasheria nguli nchini kabla ya kumpa adhabu kibaka wetu tuliyemkamata ili tumbane kote kote hasa kwenye sheria za mikataba ambako wengi hatujui. (tu weupe pee)
Wengi tunaikubali move ya Rais wetu, lakini je hakuna kingine ambacho kingefanywa ili impact yake isiwe kikwazo kipya kwetu.
Hata mimi nyumbani kwangu kuna wezi wanaendelea kuniibia kuku wangu kila mara, pamoja na kuwa wameniibia kwa miaka mingi lakini hawachoki ndiyo kwanza wanazidi kuwaiba zaidi.
Sasa nimeapa siku nikimkamata mwizi wangu live sitajali kwamba huyo ni siku yake ya kwanza kaniibia ama ni jirani yangu hapana, ni
RUNGU la kichwa, awe hai ama mfu hilo sintajali kwa kweli maana nimeumia kwa miaka mingi mno.
Hoja, Je huu utakuwa ndiyo uamuzi pekee niliopanga kuuchukua? hakuna alternative solution naweza nikaitumia badala ya hii ya Rungu la Kichwa kwa huyu mwizi wangu?