shumanice
Member
- Jul 21, 2011
- 64
- 25
Wadau habari za leo. Nilikuwa na jaribu kuangalia website za timu mbali mbali hapa bongo lakini cha ajabu nimekuta vilabu vyetu vingi havina website. Sasa nikawa najiuliza viongozi wa hizi timu wanajua umuhimu wa kuwa na website au hawajui? Na je huwa wanafuatilia habari za timu nyingine kama vile za ulaya kuona wenzao wanaendeshaje timu?
Kwa karne ya sasa habari nyingi za vilabu hujulikana kwa njia ya mtandao, mimi ninaamini kuwa kila timu inahabari nyingi sana za kuandika kwenye kurasa za internet. Nawapongeza viongozi wa Azam FC kwa kuliona hili ningependa kuona viongozi wengine wa vilabu vyetu wakiiga mfano huu.
Leo kocha yeyote akitaka kufuatilia habari za mchezaji yeyote hutumia njia ya mtandao, tunataka kuuza wachezaji wetu nje lakini habari zao hazipo!!! Je tutafuka namna hii???
Kwa karne ya sasa habari nyingi za vilabu hujulikana kwa njia ya mtandao, mimi ninaamini kuwa kila timu inahabari nyingi sana za kuandika kwenye kurasa za internet. Nawapongeza viongozi wa Azam FC kwa kuliona hili ningependa kuona viongozi wengine wa vilabu vyetu wakiiga mfano huu.
Leo kocha yeyote akitaka kufuatilia habari za mchezaji yeyote hutumia njia ya mtandao, tunataka kuuza wachezaji wetu nje lakini habari zao hazipo!!! Je tutafuka namna hii???