Ni changamoto/misukosuko gani ulishawahi pitia kisa mapenzi?

Ni changamoto/misukosuko gani ulishawahi pitia kisa mapenzi?

stritglow

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2018
Posts
622
Reaction score
1,752
Hakuna kitu kisichokuwa na changamoto duniani, mapenzi/mahusiano ni mojawapo wa vitu hivyo.

Kwenye mapenzi watu wanapitia vitu vingi sana, mengine yanafurahisha, mengine yanaumiza.

Unakuta mtu anajitunza lakini mpenzi wake anamsaliti waziwazi, mwingine anasomesha halafu anakuja kukimbiwa, mwingine ana-struggle kumpatia mpenzi wake vitu anavyohitaji lakini hata ha-appreciate. Mwingine anapenda asipopendwa halafu hataki kuachia kwahiyo anaumia daily. Wengine wametishiwa kuuawa n.k . Hizi ni changamoto chache tu watu wanapitia kwenye mahusiano mbalimbali.

N.B: Sio changamoto zote ni za maumivu, zingine zinafurahisha pia.

Kwahiyo ni changamoto/misukosuko gani ulishawai pata kisa mapenzi?
 
  • Thanks
Reactions: THT
Jana nimeenda kwa mchepuko wangu wakati nacheza na mwanangu,maana nimezaa nae kidume,nikachukua video fupi.
Mzee nikarudi zangu home huku nikiwa nimesahau kufuta ile kitu.
Mara wife akaomba simu nikampa huku akiwa na binti yangu wa grade3 ghafla nikasikia sauti yangu na mwangu tukicheza huku akiita baba baba, lahaulaaa moyo ukapasuka paap. Wife kaniuliza huyu mtoto wa nani? mzee jibu sina
Kinachoendelea Mungu anajua.....
 
Jana nimeenda kwa mchepuko wangu wakati nacheza na mwanangu,maana nimezaa nae kidume,nikachukua video fupi.
Mzee nikarudi zangu home huku nikiwa nimesahau kufuta ile kitu.
Mara wife akaomba simu nikampa huku akiwa na binti yangu wa grade3 ghafla nikasikia sauti yangu na mwangu tukicheza huku akiita baba baba, lahaulaaa moyo ukapasuka paap. Wife kaniuliza huyu mtoto wa nani? mzee jibu sina
Kinachoendelea Mungu anajua.....
Si ungesema wa rafiki yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nimeenda kwa mchepuko wangu wakati nacheza na mwanangu,maana nimezaa nae kidume,nikachukua video fupi.
Mzee nikarudi zangu home huku nikiwa nimesahau kufuta ile kitu.
Mara wife akaomba simu nikampa huku akiwa na binti yangu wa grade3 ghafla nikasikia sauti yangu na mwangu tukicheza huku akiita baba baba, lahaulaaa moyo ukapasuka paap. Wife kaniuliza huyu mtoto wa nani? mzee jibu sina
Kinachoendelea Mungu anajua.....
Kama nakuona ulivopata BP ghafla... Umejinasuaje sasa?
 
Kama nakuona ulivopata BP ghafla... Umejinasuaje sasa?
Mkuu wife alitaka kuua watoto wote watatu pamoja na yeye pia cha kushukuru watoto wawili walikuwa kwa bibi yao hivyo ikawa ngumu,lakin asubuhi na mapema kawafuata lakini mda huo dada yao alikuwa kashaenda shule
 
Mkuu wife alitaka kuua watoto wote watatu pamoja na yeye pia cha kushukuru watoto wawili walikuwa kwa bibi yao hivyo ikawa ngumu,lakin asubuhi na mapema kawafuata lakini mda huo dada yao alikuwa kashaenda shule
Daah!maisha haya nawapongeza walio amua kubaki single maisha yao yote...bora na wao kabisaa...kwakweli ni haki kuhisi kufa..
 
Jana nimeenda kwa mchepuko wangu wakati nacheza na mwanangu,maana nimezaa nae kidume,nikachukua video fupi.
Mzee nikarudi zangu home huku nikiwa nimesahau kufuta ile kitu.
Mara wife akaomba simu nikampa huku akiwa na binti yangu wa grade3 ghafla nikasikia sauti yangu na mwangu tukicheza huku akiita baba baba, lahaulaaa moyo ukapasuka paap. Wife kaniuliza huyu mtoto wa nani? mzee jibu sina
Kinachoendelea Mungu anajua.....
Kama nakuona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daah!maisha haya nawapongeza walio amua kubaki single maisha yao yote...bora na wao kabisaa...kwakweli ni haki kuhisi kufa..
Mkuu nilichanganyikiwa,baada kumweleza ukweli kuwa mtoto ni wangu alilia sana kisha akatoka nikamuuliza unaenda wapi sikujibiwa,baada ya dk kama 20 hivi akarudi mda huo mimi niko room ya watoto,ghafla nikasikia mayowe mzee nikakurupuka fasta nikaingia ndani cha kwanza ilikuwa ni kukagua tumbo lipo salama ama la nikakuta lipo salama,mara akaanza kuniambia nakufa na wewe ndio sababu,akaanza kumwamsha mtoto na kumwambi amka unione kwa mara ya mwisho mama yako,mwanangu mimi nakuita hutaki mama yako nakufa, dah nikajua huyu atakuwa kanywa sumu tu kwanini aseme anakufa na kwnn amkazanie mtoto kuamka ili amuage?
Nilichozingatia ni kumwangalia mdomoni nikiona dalili za mapovu tu fasta namkimbiza hospt lakini haikuwa hivyo
 
Demu umemwimbisha katiki ile unatengeneza mazingira ya kunjunjika ghafra anakuacha kwenye mataa simu wala text hazijibiwi lakini pia kakupiga mzinga wa fedha kadhaa.
 
Back
Top Bottom