Ni binadamu mjinga tu ndie atainua kinywa na kusema CHADEMA inakufa

Ujinga ni kujifariji kwa matumaini hewa. Nasema haya kama mtu ninayeamini kwa dhati umuhimu wa Chadema na vyama vingine vya upinzani. Lakini kutamani kuwa na upinzani ni kitu kimoja. Kuwa na upinzani usio na mwelekeo ni kitu kingine. Kuwa na upinzani wenye mwelekeo lakini unakandamizwa pia ni kitu kingine. Na kuwa na upinzani wenye mwelekeo lakini unakandamizwa lakini wanaokandamizwa wanategemea miujiza au kujihadaa kuwa "chama hakifi" sidhani kama ni wazo la busara.

Katika makala yako ndefu hakuna sehemu yoyote ya kumpa matumaini "mtu asiyejua kinachoendelea ndani ya Chadema" kuwa who is next kwenye hiyo hama hama. Lakini kibaya zaidi, hakuna anayejua nani wa kumwamini.

Adui mkubwa kabisa wa Chadema kwa wakati huu ni huko kujipa matumaini hewa. Hii hama hama sio tu inapunguza idadi ya wabunge na madiwani wenu bali pia ina athari za kisaikolojia kwa wafuasi wenu. Sintoshangaa kuona kampeni za Chadema katika uchaguzi mkuu wa 2020 zikizorota kulinganisha na 2015 au 2010 kwa sababu kuna kuvunjika moyo miongoni mwa wafuasi wa chama chenu japo ninyi makada mkiambiwa hayo mnakuwa wakali kama pili pili.

Uhai wa Chadema unategemea pia mechanisms za ndani ya chama hicho kuwa hai. Sio kila kifo husababishwa na kitu cha nje. Chadema ina tatizo kuhusu demokrasia japo jina la chama ni cha DEMOKRASIA na Maendeleo." Mnaweza kukwepa hoja ya uchaguzi mkuu, mnaweza kujidanganya kuwa "kwani Nyerere aliongoza CCM miaka mingapi" lakini athari zake mtaziona huko mbeleni.

Kuna tuhuma alizotoa Waitara kuhusu viti maalum. Wako wapi hao wakinamama waliozawadiwa viti maalum zaidi ya kuwaona baadhi yao huko insta wakiuza sura?

Badala ya makada kama wewe Yericko, Malisa, na wengineo "kuuweka mtu-kati" uongozi wa chama chenu na kusiaitiza haja ya kuthamini foot soldiers mnaohangaikia chama chenu mtaani na mtandaoni, mpo bize kujihadaa kuwa "ni ujinga kudhani Chadema itakufa."

By the way, kufa kwa chama cha siasa sio lazima kumaanishe imezikwa kaburini. Kunaweza kutokea kwa namna ya KANU huko Kenya au hata NCCR-Mageuzi (ya Mrema 1995 vs ya leo).

Mnachopaswa kuhangaikia muda huu ni kuwaondoa mamluki waliojazana kwenye chama chenu kabla hawajafanikisha madhara makubwa zaidi.

Na kosa mlilofanya 2015 kumpokea "Lowassa na watu wake" litawagharimu mno maana kuna idadi kubwa tu ya watu waliokuja na Lowassa ambao wapo kwenu kimwili lakini kiroho wapo CCM.

Mwisho, ushauri wangu muhimu kabisa kwenu ni hii: DO NOT EVER DARE TO UNDERESTIMATE DHAMIRA YA JIWE KUUA UPINZANI. Mkidhani kuwa "ah hawezi huyu" mtarudia kusoma bandiko hili kwa majonzi baada ya election ya 2020. Kwa taarifa tu, dhamira ya Jiwe ni kuhakikisha Chadema haipati mbunge hata mmoja kwenye uchaguzi huo. Hilo linatekelezwa kwa njia kuu mbili: Moja, hawa wanaonunuliwa (kuna watano hivi - wawili kutoka mkoa mmoja - ninaofahamu kuwa wapo njiani kuelekea CCM). Mbili, hujuma zinazoendelea ndani ya vyama hivyo ambazo zitashika kasi zaidi mwakani na ambazo zinaratibiwa na CCM na kitengo na lundo la mamluki lililomo ndani ya CDM.

Matarajio ya Jiwe ni kwamba laiti Chadema ikishindwa kupata mbunge hata mmoja katika uchaguzi mkuu huo basi itaelekea ICU kuanza safari ya kifo cha taratibu.

Badala ya kutuambia "Chadema haitokufa" basi angalau mtupe moyo kuwa "wale wasaliti wote wa kuhama Chadema kwenda CCM wamekwisha, tumebaki tunaokipenda chama kwa dhati." Can you do that?
Nakushukuru kwa mchango wako mkuu, kila wazo na maoni ya wadau wa siasa tunayachukua, na hili nimelichukua.... Shukrani sana.
 
Angalia video hizi
 

Attachments

  • HUYU_NDIO_NABII_ELIA_MTOTO_HALISI_WA_BUYUNGU.3gp
    3.3 MB · Views: 13
  • HII_NDIO_CHADEMA_IMARA_KATA_YA_BUKILILO_JIMBO_LA_BUYUNGU.mp4
    13.4 MB · Views: 11
  • ELIA_MICHAEL_GWARAMA.mp4
    9.2 MB · Views: 10
Mmeanza lini kufanyia kazi ushauri?

Nafasi ya katibu mkuu Chadema ipo wazi tangu kuondoka kwa Dr Slaa hivi inashindikana hata kujaza nafasi hiyo?

Sasa ni wakati mumueleze waziwazi kama anampenda sana Vicent Mashinji basi amteuwe kuwa personal secretary wake.

Mwisho kabisa you should apologize kwa Cuf, Cuf ya wajinga ni upande wa Tanganyika, lakini Wazanzibar wale ni waalimu wa siasa, na ndio maana huu mradi wa manunuzi haulipi Zanzibar kule wanakupiga kipapai hawataki mchezo wale watu.
 
Laana ya kumtukana Dr Slaa na kumuita dr Mihogo haitawaacha salama chadema.

Je Lowasa ni asset or liability ?? ---
Hii kauli yako inajitokeza kila mahali. Sijajua umeiset automatic au ipo manual! Nani asiyekula mihogo? Alisema mwenyewe kuwa alijiuzulu bila kujipanga na anaishi kwa kuka mihogo! Mbona la kuuza duka la mboga na matunda kwa mhindi hulisemei? Mbona lile la kufika bei na kulipiwa deni lake la benki na hata kuhongwa ubalozi huliongelei? Au yote yalitokea kwa kutukanwa na wanacdm? Usisahau kuwa alikuwa na kadi ya ccm iliyokuwa current kuliko ya wenye ccm yao! Ndumilakuwili na wanafiki cdm sio sahihi kwao na ndio maana wanajichekecha wenyewe na kujitupa huko jalalani!
 
Mmeanza lini kufanyia kazi ushauri?

Nafasi ya katibu mkuu Chadema ipo wazi tangu kuondoka kwa Dr Slaa hivi inashindikana hata kujaza nafasi hiyo?

Sasa ni wakati mumueleze waziwazi kama anampenda sana Vicent Mashinji basi amteuwe kuwa personal secretary wake.

Mwisho kabisa you should apologize kwa Cuf, Cuf ya wajinga ni upande wa Tanganyika, lakini Wazanzibar wale ni waalimu wa siasa, na ndio maana huu mradi wa manunuzi haulipi Zanzibar kule wanakupiga kipapai hawataki mchezo wale watu.
Hahahaaa we jamaa wewe!!
 
Sio Kifo ndugu but a major set back, people should never hide behind a smoke screen, things are falling apart in Chadema, it’s time the party should look inwards, seal all the weak areas, go back to the drawing board, and work in rejuvenating the party, with New Blood and New strategy.

We cannot afford to loose Chadema as a strong opposition party.
 
duh,mbowe anautajiri wa bilioni 800 hadi trilioni 1.5? ina mzana anamkaribia MO Dewji wa Simba ambye kwa mujibu wa forbes anautajiri wa trilioni 2,hapohapo chama chake hakina ofisi na hana mpango wa kujenga
 
ndugu yeriko,ukiachana na namna ccm ilivyona mali kwa maana ya vitega uchumi,pamoja na kwamba inawezekana vikawa ni vya kukwapua(mali za wananchi zilizomilikishwa kinguvu kwa ccm) nyinyi chadema mnavitega uchumi gani au rasilimali gani ambazo zitawapa uhakika wa kuwa na ukwasi wa kutosha kiasi cha kuweza hata kumudu jeuri ya CCM na serikali yao?
 
Ndugu Yericko, tusiombee Kifo Chadema, Hivyo mumefikiria na kujitayarisha vizuri, iwapo Lissu atapewa hifadhi ya Mkimbizi wa Kisiasa, NA tunavyojua suala hilo litawavunja nguvu sana vijana wengi wa Chadema. FOR MANY TANZANIAS LISSU IS BETTER A MARTY THAN A POLITICAL REFUGEE
 
Ili mche uwe na afya na ukuwe vizuri ni lazima upogolewe kwa kuondoa mapandikzi,hivyo ndivyo ilivyo kwa chadema wakati ccm ikidhani kuwa INA idhohofisha chadema kumbe ndo wanazidi kukistawisha, hakuna kipindi ambacho wananchi wengi wamerudisha imani yao kwenye upinzani kama kipindi hiki ,kwani wanshuhudia ccm ikifanya mambo yakijinga kabisa kukimbizana na viongozi uchwara wanaojali matumbo yao kwa kutaka madaraka ili wanufaike wao na family zao na wala sio kwa maslahi ya watanzania wengi ambao kwao kupata elimu imekuwa kama jambo LA anasa viongozi wanchi hii wameivuruga elimu sana, wananchi hawapati huduma nzuri za maji toka nchi imepata Uhuru serikali imeshindwa kabisa kumaliza kero ya maji kwa wananchi wake ambao bado sana changia maji na wanyama pori, upande wa
tiba ndio usiseme maelfu wanakufa kwa sababu ya huduma mbovu za afya, ccm imebaki kuwafanya watanzania kama wajinga sana, sana imba wimbo was kuwatoa wananchi kwenye Lindi LA umskini kumbe in hadaa tu,, watumia mabilion ya hela kununua viongozi wajinga toka upinzani badala ya kuwa boreshea huduma nzuri ili wapate angalau maji safi na salama ya kunywa, wanarudia uchaguzi wakijinga kabisa huku wakijilipa posho kwa ajili ya kampeni kwa billions of money huku wapo watanzania ambao haya kula mlo mmoja wa uhakika hawana.
Eti apo ndo use me kuwa wananchi wanaunga mkono ccm , ccm ambayo imegeuka adui ya wasema kweli utadhani no uadui wa simba na mwana mbuzi, ccm inayo tumia vyombo vya dola kupora haki za watanzania ya kuchagua viongozi wanao wapenda
Eti ccm , ccm imetuletea umaskini mkubwa ndani ya nchi hii wameiba vya kutosha na sasa wameshaona wananchi wamedhamiria kuwatoa kwa njia ya sanduku LA kura wamegeukia vyombo vya dola viwasaidie kukumbatia ujinga wao. Iko Sikh inakuja na wala haiko mbali wote hao walio kula jasho LA watanzania watavitapika tena kwa kuingizwa vidole mdomoni, acha wacheke Leo lakini lazima kesho watalia.
Mungu bariki wana mabadiliko ya kweli.
 
Kujifariji kijinga kijinga hakuwezi kumaliza matatizo yaliyoko CDM pambaneni na maboriti katika malango yenu kabla ya vibanz vya jirani.
Mtajifariji, mtachekwa na mtaendelea kupata tabu sana!
Wanakataa kwamba chadema hakuna matatizo.
 
Back
Top Bottom