NHIF wafunguka bei mpya za matibabu

NHIF wafunguka bei mpya za matibabu

kalulukalunde

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2016
Posts
1,056
Reaction score
1,086
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umesema katika kuhakikisha changamoto zinazojitokeza katika utekelezaji wa bei mpya ya gharama za matibabu, wameweka kipindi cha mpito cha miezi sita ili kufanyia kazi. Katika kipindi hicho cha Julai hadi Desemba mwaka huu, watapokea maoni kutoka kwa watoa huduma na kuboresha zaidi ili kuondoa changamoto zitakazojitokeza katika kipindi cha utekelezaji wa bei mpya.

Aidha umetoa ufafanuzi wa kuondolewa kwa wategemezi wa mwanachama wa mfuko huo kuwa ilitokana na udanganyifu, uliokuwa ukifanyika na kueleza wazazi bado wanapatiwa bima hiyo.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kutokea malalamiko kwa baadhi ya watoa huduma kutokana na mfuko huo kupunguza gharama zake, jambo lililowafanya wanachama wa mfuko huo, kukosa kufanyiwa baadhi ya vipimo na kukosa huduma mbalimbali.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo, Bernard Konga alisema kuanzia Julai mwaka huu, mfuko huo ulianza kutekeleza matumizi ya bei mpya za huduma ya matibabu kwa watoa huduma wake, waliosajiliwa na kutoa huduma kwa wanachama wa mfuko.

Alisema maboresho ya bei za matibabu ni utaratibu wa kawaida wenye lengo la kuboresha upatikanaji wa huduma bora za matibabu kwa wanachama wake na kurekebisha changamoto, zinazojitokeza katika baadhi ya bei zilizokuwa zikitumika awlai.

Alisema maboresho hayo, yamefanywa kwa kuzingatia mambo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kubadilika kwa bei ya gharama za matibabu nchini, maoni ya wadau wakiwemo wanachama na watoa huduma, kubadilika kwa miongozo ya tiba na matumizi ya teknolojia mpya katika tasnia ya huduma za matibabu.

Konga alisema kwa kuzingatia dhana ya utawala bora na ushirikishwaji wadau, mchakato huo uliwashirikisha wadau wote muhimu wakiwemo watoa huduma binafsi kupitia Chama chao cha Watoa Huduma Binafsi (APHFTA), ambao walitoa mchango wao wa maboresho ya bei na huduma na kuridhia utekelezaji wake.

Alisema maboresho hayo yaliridhiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto yenye dhamana ya kusimamia mfuko huo.

Alisema maboresho yaliyofanyika, yamehusisha kuongeza huduma zinazolipiwa na mfuko kama dawa, vitendanishi, vipimo na huduma ambazo hazikuwepo kwenye ulipaji wa baadhi ya huduma.

“Kwa kiasi kikubwa sehemu kubwa ya maboresho ya bei zinazotumika hivi sasa, yametokana na ushauri na maoni ya wadau wote na kwa kiasi kikubwa zinatarajia kuongeza uwezo wa kifedha na vituo zaidi ya asilimia tisini na tano ambavyo vinahudumia watanzania wengi zaidi, tofauti na bei zilizokuwa zinatumika awali,”alisema.

Alisisitiza kwamba maboresho ya bei za huduma, hayahusishi kubadilika kwa kiwango cha uchangishaji bali kuhakikisha kwamba wanachama wanapata huduma bora na watoa huduma wanapata malipo stahiki.

Awali, Ofisa Mtendaji Mkuu wa APHFTA, Dk Samwel Ogillo alisema uamuzi wa mfuko huo, unafanya bei za huduma za afya zikiwemo dawa na uchunguzi, zifanane katika hospitali zote nchini. Alisema hatua hiyo italeta mabadiliko makubwa kwa ngazi za chini za huduma za afya, ambazo zinakaribia asilimia 95 ya watoa huduma wa afya binafsi.

“Kabla ya uamuzi huo, ilituchukua miezi sita kufanya majadilano na serikali ili kutekeleza utaratibu huo mpya ulioanza mwezi Julai,” ilisema sehemu ya taarifa ya Ogillo.

Akizungumza na gazeti hili jana, Kaimu Mkurugenzi wa Masoko wa NHIF, Angela Mziray alisema wategemezi wanaowatambua sasa ni wale wanaotambulika serikalini. Alisema hatua hiyo ilifikiwa baada ya kubainika kuwapo kwa udanganyifu kwa baadhi ya watoa huduma na baadhi ya wanachama, ambao walifikia hatua ya kuuza uanachama wa bima hiyo.

Alisema walitambua hilo baada ya kubaini mara nyingine kuwa unaweza kukuta mwanachama ni mswahili, lakini mtegemezi wake ni mwenye asili ya Asia, jambo lililofanya mfuko huo kuibiwa sana.

Alisema udanganyifu huo, ulifanyika hasa kwa wagonjwa wenye magonjwa makubwa, kama vile figo ambapo mgonjwa hutumia zaidi ya Sh milioni moja kwa wiki kusafisha damu.

Alisema lakini wazazi na hata mtoto wa ndugu yako, ambaye unamlea ili aweze kupata kazi hiyo, inabidi kupeleka nyaraka zinazoonesha kumuasili mtoto huyo.

Awali, baadhi ya baadhi ya wagonjwa walilalamikia mfuko huo kwa kupunguza baadhi ya vipimo, kama kutahiri watoto wa kiume, kipimo cha kupima kirusi cha Human Papiloma (HPV) kinachosababisha saratani ya shingo ya kizazi.

Mmoja wa wagonjwa hao, Fatuma Njaidi alisema “NHIF inatuibia, mimi nakatwa asilimia tatu ya mshahara wangu wa milioni mbili lakini nimelazimika kulipia vipimo vya masuala ya uzazi kama Chlamydia, Mycoplasma na vipimo vingine vya homoni kama Anti Mullerian(AMH) na Ukimwi, kwa nini bima isinilipie?" NHIF imefanya mabadiliko ya bei kwa watoa huduma za afya ikipunguza gharama kwa zaidi ya asilimia 60 ili kufanikisha mpango wa huduma ya afya kwa wote (UHC), lakini pia umeongeza gharama za vipimo katika baadhi ya huduma.

Mfuko huo sasa utakuwa ukiwalipa madaktari bingwa Sh 15,000 badala ya Sh 30,000 za awali na madaktari wa kawaida watalipwa Sh 7,000 badala ya Sh 10,000. NHIF pia imeshusha malipo ya gharama za matibabu zikiwamo za upasuaji ambao awali ungegharimu Sh 600,000 sasa utalipiwa Sh 150, 000.

Habari Leo
 
Safi sana NHIF Kwa kutukumbuka sisi wanyonge.
 
Hiyo habari kwenye gazeti la Habari leo imejaa uongo, ushabiki na Propaganda nyingi kuliko Ukweli na Uhalisia. Ni habari ya upande mmoja sana.
Hii ndio inayopelekea watu wengi kutokununua gazeti la Habari Leo.

Ukweli ni kwamba, wadau hawakushirikishwa ipasavyo katika kufikia uamuzi huo. Ni uamuzi wa kibabe sana kutoka juu serikalini kwenda Bima ya Afya ili Pesa za mfuko wa Bima Afya ziende kuhudumia vituo vya Afya vya serikalini kuliko kutumika katika kutoa huduma bora kwa wachangiaji wa mfuko huo popote pale walipo.
 
Kwa mfano,
1/Unapopunguza wategemezi wa mchangiaji wa mfuko wa Bima ya Afya, unamsaidia nani? Ni mwananchi gani wa chini asiyetegemewa na ndugu zake wa karibu mbali na mke/mume, watoto na wazazi wake?

2/Unapopunguza gharama za kumwona Daktari, unamsaidia nani? Unategemea kuna mgonjwa anayetumia Bima ya Afya ataonwa na Daktari bingwa katika Private Hospital au Big hospitals?

3/Unapoondoa kabisa gharama za kurudi tena kumwona Daktari, unategemea kuna mgonjwa atapewa follow up? Akirudi tena hospitali nani atamhudumia bure?

4/Unapopunguza gharama za kufanyiwa Operesheni, unategemea kuna hospitali kubwa au private itampanga mgonjwa wa Bima afanyiwe operesheni?
Ni Hospitali gani bora ya Private iko tayari kumfanyia mgonjwa Operesheni kwa shilingi Laki na Nusu? Kama Standard Surgical Operation inahitaji at least Medical Personnel 7, Proper observation mashine 3, Electricity supply, Water Supply, Oxygen Supply, Dawa za Nusu kaputi kuu 4, Dripi za maji na Dawa 4, Sterilization Procedures, Sterilized materials(Vyombo, Mikasi, Sindano, Gloves, Pamba, Gauze nk)
 
ili kuboresha huduma wangehakikisha kuwa malipo yanalipwa sawa regardless ametibiwa wapi!!unakuta discrepancy kubwa kutokana na mahali alipotibiwa !!lakini sioni mantili hiyo kwa sababu vituo vyote vimesajiriwa na madaktari wote wamesajiriwa na baraza moja!!there is no need wagonjwa kupiga foleni hospitali Fulani wakati daktari Wa aina hiyo wangeweza kuwapata katika vituo mbalimbali na wakahudumiwa vile vile kama referral hospital au hospital za wilaya!!
 
Kwa mfano,
1/Unapopunguza wategemezi wa mchangiaji wa mfuko wa Bima ya Afya, unamsaidia nani? Ni mwananchi gani wa chini asiyetegemewa na ndugu zake wa karibu mbali na mke/mume, watoto na wazazi wake?

2/Unapopunguza gharama za kumwona Daktari, unamsaidia nani? Unategemea kuna mgonjwa anayetumia Bima ya Afya ataonwa na Daktari bingwa katika Private Hospital au Big hospitals?

3/Unapoondoa kabisa gharama za kurudi tena kumwona Daktari, unategemea kuna mgonjwa atapewa follow up? Akirudi tena hospitali nani atamhudumia bure?

4/Unapopunguza gharama za kufanyiwa Operesheni, unategemea kuna hospitali kubwa au private itampanga mgonjwa wa Bima afanyiwe operesheni?
Ni Hospitali gani bora ya Private iko tayari kumfanyia mgonjwa Operesheni kwa shilingi Laki na Nusu? Kama Standard Surgical Operation inahitaji at least Medical Personnel 7, Proper observation mashine 3, Electricity supply, Water Supply, Oxygen Supply, Dawa za Nusu kaputi kuu 4, Dripi za maji na Dawa 4, Sterilization Procedures, Sterilized materials(Vyombo, Mikasi, Sindano, Gloves, Pamba, Gauze nk)



kama ni hivo basi wamechemka ile mbaya!!!kwa njia nyingine wanataka wagonjwa wrote Wa NHIF watibiwe katika hospitali za serikali tu na huko ni kudidimiza huduma za afya na kuweka ubaguzi !!!
 
Kwa mfano,
1/Unapopunguza wategemezi wa mchangiaji wa mfuko wa Bima ya Afya, unamsaidia nani? Ni mwananchi gani wa chini asiyetegemewa na ndugu zake wa karibu mbali na mke/mume, watoto na wazazi wake?

2/Unapopunguza gharama za kumwona Daktari, unamsaidia nani? Unategemea kuna mgonjwa anayetumia Bima ya Afya ataonwa na Daktari bingwa katika Private Hospital au Big hospitals?

3/Unapoondoa kabisa gharama za kurudi tena kumwona Daktari, unategemea kuna mgonjwa atapewa follow up? Akirudi tena hospitali nani atamhudumia bure?
ni shida mkuu.

4/Unapopunguza gharama za kufanyiwa Operesheni, unategemea kuna hospitali kubwa au private itampanga mgonjwa wa Bima afanyiwe operesheni?
Ni Hospitali gani bora ya Private iko tayari kumfanyia mgonjwa Operesheni kwa shilingi Laki na Nusu? Kama Standard Surgical Operation inahitaji at least Medical Personnel 7, Proper observation mashine 3, Electricity supply, Water Supply, Oxygen Supply, Dawa za Nusu kaputi kuu 4, Dripi za maji na Dawa 4, Sterilization Procedures, Sterilized materials(Vyombo, Mikasi, Sindano, Gloves, Pamba, Gauze nk)
 
Kama chanzo ni Habari Leo basi kuna propaganda za kitoto...ukweli huwaga haufichiki
 
Kama Ni Kweli Basi NHIF hazitakubaliwa Kabisa Hospitali za Private.. na Kwa Waliopo Nazo Basi wataziondoa Muda Si Mrefu
 
Nje ya mada.Nina mzazi wangu mzee ninataka kumkatia bima ya afya nimeenda NHIF wakaniambia hawana huduma hiyo niende kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya.Ni kweli hii?
 
Hiyo habari kwenye gazeti la Habari leo imejaa uongo, ushabiki na Propaganda nyingi kuliko Ukweli na Uhalisia. Ni habari ya upande mmoja sana.
Hii ndio inayopelekea watu wengi kutokununua gazeti la Habari Leo.

Ukweli ni kwamba, wadau hawakushirikishwa ipasavyo katika kufikia uamuzi huo. Ni uamuzi wa kibabe sana kutoka juu serikalini kwenda Bima ya Afya ili Pesa za mfuko wa Bima Afya ziende kuhudumia vituo vya Afya vya serikalini kuliko kutumika katika kutoa huduma bora kwa wachangiaji wa mfuko huo popote pale walipo.
Muhimu Afya kwa wote .unafikiri ni mdau gani atakubali kupunguziwa ulaji wake.na zaidi hapo mdau muhimu ni mwanachi ambae tayari anakwenda kufaidika punguzo la upasuaji toka laki 6 mpaka laki na nusu.
 
Muhimu Afya kwa wote .unafikiri ni mdau gani atakubali kupunguziwa ulaji wake.na zaidi hapo mdau muhimu ni mwanachi ambae tayari anakwenda kufaidika punguzo la upasuaji toka laki 6 mpaka laki na nusu.
Wewe kichwani upo timamu? Katika laki sita, bima ya afya watalipa laki na nusu tu hizo pesa zingine laki nne na nusu uongeze mwenyewe.

Hata kama ulikimbi shule hata kusoma hujui?
 
si kweli kwamb
Kwa mfano,
1/Unapopunguza wategemezi wa mchangiaji wa mfuko wa Bima ya Afya, unamsaidia nani? Ni mwananchi gani wa chini asiyetegemewa na ndugu zake wa karibu mbali na mke/mume, watoto na wazazi wake?

2/Unapopunguza gharama za kumwona Daktari, unamsaidia nani? Unategemea kuna mgonjwa anayetumia Bima ya Afya ataonwa na Daktari bingwa katika Private Hospital au Big hospitals?

3/Unapoondoa kabisa gharama za kurudi tena kumwona Daktari, unategemea kuna mgonjwa atapewa follow up? Akirudi tena hospitali nani atamhudumia bure?

4/Unapopunguza gharama za kufanyiwa Operesheni, unategemea kuna hospitali kubwa au private itampanga mgonjwa wa Bima afanyiwe operesheni?
Ni Hospitali gani bora ya Private iko tayari kumfanyia mgonjwa Operesheni kwa shilingi Laki na Nusu? Kama Standard Surgical Operation inahitaji at least Medical Personnel 7, Proper observation mashine 3, Electricity supply, Water Supply, Oxygen Supply, Dawa za Nusu kaputi kuu 4, Dripi za maji na Dawa 4, Sterilization Procedures, Sterilized materials(Vyombo, Mikasi, Sindano, Gloves, Pamba, Gauze nk)
1.NHIF haijashusha gharama ya kumwona daktari bingwa kutoka 30,000/= hadi 15,000.Ukweli ni kwamba gharama za kumwona daktari bingwa hutofautiana kulingana na ngazi ya hospitali.Kwa hospitali za taifa na za rufaa za kanda gharama za kumwona daktari bingwa( specialist) ni sh.25,000 na super specialist ni 35,000/= . Hospitali kubwa zote za serikali na zile za binafsi zipo katika ngazi hii na madaktari hao wanalipwa bei hii.Kwa utafiti uliofanyika bei hizi zipo juu kidogo ya gharama zinazotozwa kwa wagonjwa wa private(wasiotumia bima). Hiyo consultation ya shilingi 15,000/= kwa daktari bingwa ni kwa hospitali za ngazi ya mkoa(regional refferal Hospitals kama vile Amana,Mt Meru,Sekou Toure nk) na hapo awali ilikuwa shilingi elfu mbili-2,000 sawa na ongezeko la zaidi ya asilimia 750%.Hivyo hospitali itakayolalamika iulize ipo ngazi gani kwa mujibu wa vigezo vya wizara ya afya.
Hata hivyo ni kweli kwamba gharama za kumwona daktari zimeshushwa katika vituo vinavyoitwa specialised clinics.hizi ni kliniki nogondogo za madaktari bingwa.nyingi huzunguka maeneo jirani na hospitali kubwa kubwa.Vituo hivyo vimepewa ngazi sawa na hospitali za rufaa za mkoa na hivyo kushuka kutoka 30,000/= hadi 15000 kwa daktari bingwa.
2.NHIF haijafuta gharama za kurudi tena hospitali.gharama hizo ni sawa na zile za kumwona daktari.
3.kuhusu gharama za upasuaji inategemea ni upasuaji wa aina gani. baadhi ya huduma zimeongezeka bei, nyingine zimeshuka kidogo na nyingine zimebaki katika bei ya awali.kuna huduma za mpya za upasuaji wa moyo ambazo ni gharama kubwa hadi kufikia shilingi milioni 15.ukiweka gharama za wodini na matibabu mengine gharama ni kubwa sana na inalipwa na NHIF.Msingi wa lalamiko kuhusu bei za upasuaji ni kwamba NHIF imekuongeza wigo wa upasuaji katika ngazi za mikoa na wilaya.Hapo awali NHIF ilikuwa hailipii upasuaji huo katika ngazi za wilaya, vituo vya afya na mkoa.Huduma hizo gharama yake ni chini kuliko katika ngazi ya kanda na taifa.
NB: NHIF ni shirika la umma na ina wajibu wa kuhakikisha inadumu(sustainability) katika kuwahudumia wananchi.Ni lazima ihakikishe gharama za huduma zinakuwa ni "halisi".
 
Filosofi ya bima ya afya ni mzuri sana. Changamoto ni kwamba watu wengi sio waaminifu. Bima ina hitaji utmost good faith from either party
 
Serikali la sasa hivi limejaa uongouongo tu! Hiyo hela kubwa wanayotukata inaenda wapi? Waache ujinga!
 
Back
Top Bottom