NHIF wafunguka bei mpya za matibabu

NHIF wafunguka bei mpya za matibabu

Mimi na familiya yangu ni watumiaji wa NHIF tangu ilipoanzishwa.

Kabla hata ya kupunguza hizo gharama zilizokuwepo kwa 60% bado kulikuwa na huduma nyingine tulikuwa tuna top up. Mathalani katika hospital ukilazwa, NIHF walikuwa wanalipa Tsh 5,000 kwa kitanda kwa siku. Lakini bei halisi ya kitanda katika hospital hiyo ni Tsh 10,000/- . Hivyo pamoja na kwamba hiyo hospital inahudumia wanachama wa NHIF, lakini ukitaka kulazwa wanakuambia u top up 5,000/-. Hili NHIF wanalijua vizuri kwasababu nilishakwenda ku report, na wakakili kwamba bei zao elekezi ziko chini wanatakiwa kuzi review.

Hivyo kwa baadhi ya vipimo na hata madawa. Unakuta kuna dawa ya India inauzwa Tsh 3,000/- na dawa hiyo imetengenezwa UK, inauzwa Tsh 15,000/-. Lakini watoa huduma wanakupata dawa ya India ya 3,000/- kwasababu ndiyo NHIF wamekubali kurefund ambayo kimsingi ni substandard.

NHIF kupuguza gharama za matatibu kwa watoa huduma ni mwiba mkali kwa sisi wanachama. Kitakachotokea ni kwamba Private hospitals nyingi zitaanza kukataa wagonjwa wa NHIF. Na zile zitakazokubali kutibu wanachama wa NHIF basi watapewa huduma substandard au kama mwanacahama atataka huduma standard basi itabidi a top up difference.

Kama kweli huduma za afya zimepungua hivyo kwa 60%, kwanini basi hata sisi wachangiaji tusipunguziwe kuchangia NHIF kwa 60%?! na badala yake tunaendelea kukatwa pesa ile ile? Huu uamuzi waliofanya NHIF ni wizi na dhuluma ya mchana kweupe kwa sisi wanachama.
 
Ninachoshangaa juu ya Mwandishi wa habari Dr. Buguzi ambae alianzisha mjadala huu wa bei za huduma katika magazeti kuenda kinyume na ueledi katika uandishi wa habari. Nilitarajia kutokana na kuwa daktari na pia kuwa mtaalam katika fani ya uandishi wa habari kuweka dhana ya utafiti na uchambuzi mbele kabla hajaandika na kupotosha umma huku moyoni mwake akijua ukweli halisi wa mabadiliko ya bei za huduma za NHIF.
Mfano; Anawaaminisha wananchi na wanachama kwa ujumla kuwa bei ya huduma ya upasuaji wa aina zote kwa wanachama wa NHIF katika hospitali ngazi zote ni Tsh. 150,000.00.
Hii taarifa ameitoa wapi? ameifanyia uchunguzi/ utafiti kabla hajaindika? amewasiliana na wahusika wa NHIF kujua ukweli wake? ameipitia bei iliyotolewa kwa watoa huduma za afya waliosajiliwa na NHIF?
Haya ni miongoni mwa maswali machache najiuliza kuhusu uandishi wa Taarifa hii kwa ujumla iliyotolewa na huyu Daktari- Mwandishi.
Mwandishi wa habari muongo huwa hafiki mbali kwa kuwa uongo haudumu. Na kuna "dalili zote kuonesha unatumika kwa maslahi ya kikundi fulani"
Ninachokushauri ndugu yangu mwandishi, Fanya utafiti na uchambuzi, sawazisha (Balance) ujumbe wako kwa pandende zote mbili na usipotoshe umma kwa maslahi yako binafsi au maslahi ya kikundi chochote.
Mwisho kabisa, tembelea hospitali zote kubwa nchini uone mchango wa Serikali katika kuwapatia huduma za afya wananchi kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
Mimi ni Mwanachama wa Mfuko huu, naomba udumu zaidi ili kusaidia matibabu ya wananchi wa Tanzania.

 
NHIF ikumbuke jinsi ilivyotushurutisha kujiunga nayo. Kuna hosp ukienda na kadi ya NHIF haijalishi ni ya rangi gani una treatiwa kama unatibiwa bure. Kuna sehemu 'special' na madaktari 'special' kwa ajili yako. Hatukatai hosp binafsi si za kuamini likija suala la malipo anafanya bima ya umma. Hata juzi nimeona dk mmoja US alikuwa anagushi bills akiandika kufanyia wagonjwa operation kumbe uongo na amejipatia millions of dollar kiudanganyifu sembuse Bongo. Umakini unahitajika kwenye mali ya umma lakini wateja wenu tunataka kuendelea kupata huduma with respect. Wengine tunakatwa ela ndefu hadi unatamani bora kungekuwa na option ya bima gani unataka. Mimi nanunua miwani akati wenye kadi za Jubilee wanapata kutumia bima. Siyo fair
 
Nataka kujiunga na NHIF nitumie Njia gani ya kujiunga
 
Huyu Raisi ashaharibu nchi yetu kabisa ndani ya Mwaka mmoja life plus huduma za kijamii zishaanza kudidumia.
kwa upande wa Afya tutegemee watumia BIMA wakifa kwa uzembe wa Mfuko huu!

Ndomaana naamin kuwa zile taarifa za kusguka kwa Uchumi ni kweli kabisa na hakika tutashuhudia Mambo yakizidi kuwa magumu kila kukicha
E.g. kwa mtumishi wa Umma ukitaka kwenda nje ya nchi -usumbufu kibao mpaka upate kibali teyar ushachoka wakati ulikuwa unajigharamia mwenyewe nauli na kila kitu.

Kodi unapanda lakin life linakuwa tait kwasababu yakukurupuka Ovyo kwa maamuzi sahihi.
Eg. Kuvunjiwa nyumba haadhi ya wananchi halafu wanajengewa tena upya?
Kuhamia serkali Dodoma kwa bajeti ambayo ilikuwa bado haijapangwa kwa mwaka huu hjvyo inaonyesha baadhi ya hiduma zitaminywa ili kufanikisha ujenzi wa nyumba hizo
 
Iliyobaki tutunze afya kwa gharama yoyote ile. Ngoja nikafanye mazoezi mie
 
Hizo zinazo tolewa ni dun sssa wataweza? kilamwez wanakata wafanyakaz ila Huduma ni dun bora wafute huu mfuko
 
Safi sana NHIF Kwa kutukumbuka sisi wanyonge.
Hebu fafanua jinsi ulivyokumbukwa, maana nijuavyo mimi hiyo hela ya matibabu haulipi wewe bali mfuko. Na kiwango chako cha kukatwa na mfuko kiko palepale. Fafanua tafadhali.
 
Muhimu Afya kwa wote .unafikiri ni mdau gani atakubali kupunguziwa ulaji wake.na zaidi hapo mdau muhimu ni mwanachi ambae tayari anakwenda kufaidika punguzo la upasuaji toka laki 6 mpaka laki na nusu.
Mwananchi hapunguziwi chochote hapo.
Yete anakatwa mshahara wake vile vile.

Hapo anae punguziwa ni NHIF (serikali).

Ukimsoma vizuri Zanzibar-ASP utaova mwananchi huyo mnyonge ndio anaenda kuongezewa mzigo kwa kuondolewa ndugu wategemezi, kuondolewa huduma ya kurudi kea daktari (follow up).

Wanaenda kuvurunda hii huduma ya bima ya afya.

Watu wataenda kulipia BIMA za kampuni binafsi. Sasa sijui huko wataziuwa hizo kampuni!
 
Back
Top Bottom