NHIF ufanisi wenu unatia mashaka na huenda kugharimu maisha ya watu

Goodluck Mshana

JF-Expert Member
Aug 7, 2011
1,271
1,119
Salamu kwenu wana JF,

Nimeona nikisemee hili humu JF kwani nina imani wahusika wa NHIF baadhi ni members humu. NHIF mmekuwa na utaratibu wa ajabu sana na kero kwa wateja wenu pale ambapo mteja anakosa huduma kwa kutokuwa na kitu kinachoitwa ' Verification Number '.

Hii ni namba ambayo hutolewa na NHIF makao makuu na hazitolewi hospitalini! Ni jambo la kuudhi na kusikitisha sana juzi niliposhuhudia mgonjwa wa Figo pale Muhimbili anakosa huduma kwakuwa hana hiyo number.

Hivyo alilazimika kufunga safari hadi headquarters NHIF. Nilitafakari mgonjwa huyu ambaye hata hakuwa na mtu wa kumuagiza huku akiwa hoi kajichokea. Huu sio uuwaji? Maana kama mtu anakatwa mshahara wake ama kwa namna yoyote ile tunatarajia apate huduma nzuri asiweze jutia pesa yake. Lakini kwa NHIF ni tofauti!

Jana usiku nikiwa TMJ hospital nahangaika kuhakikisha mtoto wangu anapata huduma ya haraka baada ya kuonesha kuwa na joto kali likiashiria homa au infection pia nilikosa huduma ya 'BIMA'!! Maelezo ya mtoa huduma ni kukosekana kwa Verification Number!! Huu ni upuuzi kabisa.

Naambiwa mpaka makao makuu ndio nitapewa hiyo namba then ndio huduma itaendelea?! Kweli? Muda huo ni saa sita usiku...sasa mtuambie makao makuu yapi yapo wazi muda huo kuweza ku verify hizo namba! Ni kwa bahati tu nilikuwa na emergency money mtoto wangu akapata huduma kwa cash!

Kitu ambacho sio sahihi kabisa maana ikifika mwisho wa mwezi huwa mnakata pesa zenu bila kupewa verification namba na wateja wenu! This mess should stop!

Lipo swala la kukosa mtandao wakati wa ku upload ama ku dowland taarifa za vipimo kwa wagonjwa. Endapo mtandao upo down basi mgonjwa atasubiri mpaka mtandao ukae sawa! Hapo pia kuna risk ya kupoteza uhai! Kwanini msiwaze kutengeneza Mobile Application (Apps) ambayo itakuwa user friendly kwa mawakala wenu kwenye kila hospitali?!

Hata kama mtandao upo chini bado wanaweza kutumia simu zao kutoa huduma na ku print out majibu ama taarifa zozote za kimatibabu. Hata hicho mnachoita verification number kingeweza kupatiwa ufumbuzi kwa kuingiza ID number kwenye App na ku update information.

NHIF mmebeba jukumu kubwa sana la kulinda afya za watanzania. Kwa kuendelea na mizaha hii kwenye maisha ya watu ipo siku tutapoteza watanzania wenzetu. Tuumize akili kuweza kuwa na huduma za kasi na kisasa.

Tuache umakini wa kukata kwenye mishahara tu...ongezeni umakini kwenye utoaji huduma! Habari ya centralization sio afya kwenye shirika lililomakini na lenye kutaka ufanisi kwenye utendaji wake!

Goodluck Mshana
 
Salamu kwenu wana JF,

Nimeona nikisemee hili humu JF kwani nina imani wahusika wa NHIF baadhi ni members humu. NHIF mmekuwa na utaratibu wa ajabu sana na kero kwa wateja wenu pale ambapo mteja anakosa huduma kwa kutokuwa na kitu kinachoitwa ' Verification Number '.

Hii ni namba ambayo hutolewa na NHIF makao makuu na hazitolewi hospitalini! Ni jambo la kuudhi na kusikitisha sana juzi niliposhuhudia mgonjwa wa Figo pale Muhimbili anakosa huduma kwakuwa hana hiyo number. Hivyo alilazimika kufunga safari hadi headquarters NHIF. Nilitafakari mgonjwa huyu ambaye hata hakuwa na mtu wa kumuagiza huku akiwa hoi kajichokea. Huu sio uuwaji? Maana kama mtu anakatwa mshahara wake ama kwa namna yoyote ile tunatarajia apate huduma nzuri asiweze jutia pesa yake. Lakini kwa NHIF ni tofauti!

Jana usiku nikiwa TMJ hospital nahangaika kuhakikisha mtoto wangu anapata huduma ya haraka baada ya kuonesha kuwa na joto kali likiashiria homa au infection pia nilikosa huduma ya 'BIMA'!! Maelezo ya mtoa huduma ni kukosekana kwa Verification Number!! Huu ni upuuzi kabisa. Naambiwa mpaka makao makuu ndio nitapewa hiyo namba then ndio huduma itaendelea?! Kweli? Muda huo ni saa sita usiku...sasa mtuambie makao makuu yapi yapo wazi muda huo kuweza ku verify hizo namba! Ni kwa bahati tu nilikuwa na emergency money mtoto wangu akapata huduma kwa cash! Kitu ambacho sio sahihi kabisa maana ikifika mwisho wa mwezi huwa mnakata pesa zenu bila kupewa verification namba na wateja wenu! This mess should stop!

Lipo swala la kukosa mtandao wakati wa ku upload ama ku dowland taarifa za vipimo kwa wagonjwa. Endapo mtandao upo down basi mgonjwa atasubiri mpaka mtandao ukae sawa! Hapo pia kuna risk ya kupoteza uhai! Kwanini msiwaze kutengeneza Mobile Application (Apps) ambayo itakuwa user friendly kwa mawakala wenu kwenye kila hospitali?! Hata kama mtandao upo chini bado wanaweza kutumia simu zao kutoa huduma na ku print out majibu ama taarifa zozote za kimatibabu. Hata hicho mnachoita verification number kingeweza kupatiwa ufumbuzi kwa kuingiza ID number kwenye App na ku update information.

NHIF mmebeba jukumu kubwa sana la kulinda afya za watanzania. Kwa kuendelea na mizaha hii kwenye maisha ya watu ipo siku tutapoteza watanzania wenzetu. Tuumize akili kuweza kuwa na huduma za kasi na kisasa. Tuache umakini wa kukata kwenye mishahara tu...ongezeni umakini kwenye utoaji huduma! Habari ya centralization sio afya kwenye shirika lililomakini na lenye kutaka ufanisi kwenye utendaji wake!

Goodluck Mshana
Kuna kipindi wana chama wote waliambiwa wafanye uhakiki wa kadi zao sasa sijui kama ulifanya na ndiyo hiyo verification number iliyokuwa Inahitajika.

Kama hukufanya uhakiki may be ndiyo maana ulipata hiyo shida.
 
Kuna baadhi ya magonjwa huwezi pata huduma kupitia bima...yaani hii kwakweli hata siwaelewi,mtu anachangia,then akipata maradhi anaambiwa tatizo halipo kwenye bima?...hili NHIF mliangalie kwa mapana.
 
System iko Corrupted hiyo...Yaani uende makao makuu ( HQ)kupewa verification Number?

Thus why wengine tuamua kujiumiza kwa kulipa cash kuliko unakatwa hela halafu mambo ya ajabu yanajitokeza hivi...

Sasa kama niko Namtumbo huku nitakuja Dsm ?
 
Kuna kipindi wana chama wote waliambiwa wafanye uhakiki wa kadi zao sasa sijui kama ulifanya na ndiyo hiyo verification number iliyokuwa Inahitajika.

Kama hukufanya uhakiki may be ndiyo maana ulipata hiyo shida.
Nilifanya Uhakiki nina green card ambayo makato yake ni makubwa zaidi...
 
Nilifanya Uhakiki nina green card ambayo makato yake ni makubwa zaidi...
OK basi kuna tatizo mahali.Sasa aliyepo mkoani wilani naye inakuwaje kupata hiyo verification number.

Pole sana ndugu kwa usumbufu huo..nadhani kuna mahali kuna MTU hajawajibika au kuna kadi feki wanazitoa ktk system ujue zilikuwa nyingi sana
 
Hamisi Kigwangala sijui kama atakuelewa.
Anaweza asikubali maana madaktari huwa wanaamini wao ni nusu Mungu,nusu mtu.Wanaamini huwa hawakosei,na wanaamini kuwa wanajitosheleza hivyo hawahitaji ushauri.Wakisikia maoni tofauti na wao na we ukiwa so daktari,watakubandika moja wapo ya magonjwa ya akili ili waendelee kubaki sahihi.
 
Ili NHIF iwe na ufanisi,ni lazima wakurugenzi wasiwe madaktari.Madaktari wanatakiwa kuwa chini ya usimamizi ili mambo yaende
 
Back
Top Bottom