NHIF kwa hili hamtutendei haki Toto afya card

ibanezafrica

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,261
6,543
Eti ukimlipia mtoto kadi ya matibabu wanakupa risiti tu halafu unaambiwa kadi ufuate baada ya siku tisini na kwamba mtoto ataweza kuanza kutibiwa kwa kadi hiyo baada ya hizo siku tisini yaani miezi mitatu, hili limekaje?

Kwanini sasa pesa mnachukua? Mimi mwananchi masikini ninapojibana na kuwakatia watoto wangu bima ni kusudio langu ije inisaidie pindi ikitokea ugonjwa sasa mnaponiambia hadi siku tisini zipite sidhani kama ni kutenda haki.

Tuombe Wizara husika wajaribu kulifuatilia na kurekebisha kasoro hii. Huenda vikwazo hivi ndio vinafanya bado wazazi wengi washindwe kujiunga na mpango huo ambao ni mzuri isipokua wenye masharti magumu.

Tuombe NHIF pamoja na Wizara tusaidiwe wananchi kwa hili, mbona ukienda fungua account bank wanakupa ATM card yako kwa wakati muafaka?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ni sheria ya bima za afya mkuu, hata mtumishi akianza kukatwa kwa mara ya kwanza lazima akae miez mitatu ndipo apeleke ombi la kutengenezewa kadi, yaani lazima michango mitatu ya mwezi au miezi mitatu kwanza.
 
... lengo ni kuhakikisha hakuna anayekimbilia kukata bima baada ya tatizo la ugonjwa kutokea; sio utaratibu wa bima yoyote huo. Risks ndizo zinakatiwa bima na sio issues. Ajali ya gari imeshatokea ndio unaenda kukata bima, sivyo bima ilivyo! Unatakiwa uikate kabla ya ajali yaani wakati huna uhakika kama ajali itatokea au haitatokea.

Ikiruhusiwa bima (NHIF au mfuko mwingne wowote) zikatwe baada ya ugonjwa kutokea mfuko utafilisika kwa sababu kila mtu ataenda kukata bima baada ya kujiridhisha kuwa ni mgonjwa. This means atakacholipa ndicho kitakachotumika kumtibu na pengine huenda kisitoshe unadhani sustainability ya mfuko itakuwaje?

Sustainability ya bima ya afya inataka wagonjwa wawe wachache sana kuliko wazima. Wanachama wazima wasiougua mara kwa mara ndio husaidia ku-top kwa wengine wagonjwa wa mara kwa mara na gharama nyingine za uendeshaji wa mfuko including mishahara, kodi, n.k.

Logic yake ndio hiyo!
 
... sawa Boss; tupatie wewe sababu za msingi.
Mtu akilipa apewe kadi mbona magari ukikata bima wanatoa Leo Leo na maisha yanasonga kama kawaida!?
Ni roho za binadam zimejaa kutu!

Wangeweza kutoa kadi siku hiyo halafu wakaifunga kwa siku kadhaa ili mteja asubili kwa siku chache then ifunguliwe lakini akiwa na kadi yake mkononi ili kuondolea usumbufu
 
... lengo ni kuhakikisha hakuna anayekimbilia kukata bima baada ya tatizo la ugonjwa kutokea; sio utaratibu wa bima yoyote huo. Risks ndizo zinakatiwa bima na sio issues. Ajali ya gari imeshatokea ndio unaenda kukata bima, sivyo bima ilivyo! Unatakiwa uikate kabla ya ajali yaani wakati huna uhakika kama ajali itatokea au haitatokea.

Ikiruhusiwa bima (NHIF au mfuko mwingne wowote) zikatwe baada ya ugonjwa kutokea mfuko utafilisika kwa sababu kila mtu ataenda kukata bima baada ya kujiridhisha kuwa ni mgonjwa. This means atakacholipa ndicho kitakachotumika kumtibu na pengine huenda kisitoshe unadhani sustainability ya mfuko itakuwaje?

Sustainability ya bima ya afya inataka wagonjwa wawe wachache sana kuliko wazima. Wanachama wazima wasiougua mara kwa mara ndio husaidia ku-top kwa wengine wagonjwa wa mara kwa mara na gharama nyingine za uendeshaji wa mfuko including mishahara, kodi, n.k.

Logic yake ndio hiyo!
Andiko lako linaonyesha kuna shida ....yaani stability ya mfuko uwe na wanachama wachache wasiouguaugua hovyo..!

Mfumo huu kumbe hautotukomboa watanzania hasa wa hali ya chini

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
... lengo ni kuhakikisha hakuna anayekimbilia kukata bima baada ya tatizo la ugonjwa kutokea; sio utaratibu wa bima yoyote huo. Risks ndizo zinakatiwa bima na sio issues. Ajali ya gari imeshatokea ndio unaenda kukata bima, sivyo bima ilivyo! Unatakiwa uikate kabla ya ajali yaani wakati huna uhakika kama ajali itatokea au haitatokea.

Ikiruhusiwa bima (NHIF au mfuko mwingne wowote) zikatwe baada ya ugonjwa kutokea mfuko utafilisika kwa sababu kila mtu ataenda kukata bima baada ya kujiridhisha kuwa ni mgonjwa. This means atakacholipa ndicho kitakachotumika kumtibu na pengine huenda kisitoshe unadhani sustainability ya mfuko itakuwaje?

Sustainability ya bima ya afya inataka wagonjwa wawe wachache sana kuliko wazima. Wanachama wazima wasiougua mara kwa mara ndio husaidia ku-top kwa wengine wagonjwa wa mara kwa mara na gharama nyingine za uendeshaji wa mfuko including mishahara, kodi, n.k.

Logic yake ndio hiyo!
Kwa lugha rahisi ni kwamba Bima zinataka faida.

Yaani unatakiwa ukate Bima halafu usiugue kabisa.
 
Watu wengi wanaenda hospitali kwa pale wanapoumwa hawajui kuwa dharula zipo mda wote.

Ikitokea issue inahitajika labda surgery kwa cash inaweza fika 1M sasa pale ndio anashauliwa ungekuwa na bima mambo yangeenda vizuri.

Hapo sasa ndio swala la mleta mada linaanza kuwa anataka akate ili imsaidie mda ule wakati makampuni nao wanataka wateja wa kudumu bila kujali unaumwa au hauumwi.
 
Kwa lugha rahisi ni kwamba Bima zinataka faida.

Yaani ukate Bima halafu usiugue kabisa.
Nafikiria kama hawa wanajiweka kibiashara kwanini mfuko huu usisimamiwe na wizara ikishirikiana na hospital kuu za rufaa na zile za mikoa na wilaya?
Maana hao ndio hasa watakaotekeleza majukumu yao bila kuitolea macho faida kubwa.watatoa huduma sababu ni tasnia inayoongozwa na wito

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Changamoto kubwa tanzania ni ajira, wengi ambao wameajiriwa na waajiri wao wanapeleka michango yao huko hawafikirii sana kuhusu hili.

Sasa mimi natafuta hela ambayo mwezi huu sio sawa na mwezi ujao uhakika wa kuwasilisha michango yangu kwa usawa ule ule kila onapohitajika ni ngumu sana.
 
Nafikiria kama hawa wanajiweka kibiashara kwanini mfuko huu usimamiwe na wizara ikishirikiana na hospital kuu za rufaa na zile za mikoa na wilaya?
Maana hao ndio hasa watakaotekeleza majukumu yao bila kuitolea macho faida kubwa.watatoa huduma sababu ni tasnia inayoongozwa na wito

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Mkuu msingi wa Bima uko hivyo.

Wachangie wengi, halafu watumiaji wawe wachache. Kumbuka mtumiaji anaweza kutumia pesa nyingi kuliko aliyochangia ( maana yake atatumia pesa za wachangiaji wengine )

Hivyo Kila mtu akitumia huo mfuko wa BIMA unakufa.
 
Back
Top Bottom