MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,194
* Sasa kutumika kuungoa uongozi
* Milioni 50/- za hongo zawatesa
* Ujumbe wa Dk. Slaa wapondwa
NA SHAABAN MDOE, ARUSHA
HALI si shwari ndani ya uongozi wa CHADEMA wilayani Arusha, baada ya kuzuka mvutano, wanachama wakitaka uchaguzi ufanyike ili kuwaondoa viongozi walio madarakani. Imeelezwa kuwa viongozi wa kata 18 wilayani humo walikaa kikao na kukubaliana viongozi wa mkoa waitishe uchaguzi, wakidai waliopo madarakani si halali. Akizungumza baada ya kumalizika kikao hicho, kwenye hoteli ya Palson, mjini hapa, Mwenyekiti wa kata ya Kati, Shubeti Rashid, alisema viongozi wote wa wilaya wamekuwa wakikaimu nafasi walizonazo kwa muda mrefu. "Wanakaimu nafasi hizo kwa zaidi ya mwaka mmoja unaotakiwa kikatiba," alisema. Aliwataja viongozi wanaokaimu nafasi hizo kuwa, Mwenyekiti wa chama hicho wa wilaya, Derick Magoma, Katibu wa uenezi wa wilaya, Gabriel Lucas, Mwenyekiti wa baraza la wanawake, Joyce Mukya, Katibu wake Margaret Olotu na wajumbe wanne wa kamati ya utendaji wilaya. Rashid alisema kukaimiwa kwa nafasi hizo kwa kipindi kirefu kumetokana na sababu za maslahi binafsi kabla ya kuelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Alisema licha ya uchaguzi kutangazwa miezi minne iliyopita ulifutwa bila maelezo. Uchaguzi ulitangazwa miezi minne iliyopita lakini kuna tetesi watu walihongwa sh. milioni 50 ili uahirishwe kwa kuwa walidai wanachama waliokuwa wakigombea nafasi hizo ni mamluki na wasingekuwa na faida katika kuwawakilisha wanachama," alisema Rashid.
Alisema viongozi wa kata 18 wameweka maazimio kadhaa, likiwemo la kutoa siku saba ili uongozi wa chama hicho mkoa utoe tamko kuhusu uchaguzi.
Rashid alisema uongozi ukishindwa watatumia nguvu ya umma kuitisha uchaguzi.
Naye Mwenyekiti wa chama hicho kata ya Terati, Gerald Josephat, alisema nguvu ya umma itakayotumika itahusisha maandamano ili kushinikiza viongozi wasio halali kutoka madarakani kupisha uchaguzi ufanyike. Alisema pia watazifunga ofisi za mkoa hadi uchaguzi utakapoitishwa. Viongozi hao waliutaka uongozi wa mkoa kuhakikisha chama hicho kinakuwa na ofisi ya wilaya, kwani ni aibu kwa chama chenye wabunge watatu kukosa ofisi, licha ya kupokea ruzuku ya sh. 800,000 kila mwezi ambazo zingeweza kulipia kodi ya pango.
Walisema wabunge hao kwa umoja wao kama wasingekuwa na maslahi binafsi wangeweza kuchagia kupatikana ofisi na mahitaji mengine kama njia ya kukijenga chama hicho. Viongozi hao waliponda maagizo ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, aliyoyatoa kupitia ujumbe mfupi wa maneno, akiwataka waache kujadili mambo hayo. Kwa mujibu wa viongozi hao, ujumbe huo unaonyesha nia ya kuficha maovu na unaweza kisambaratisha chama hicho. Kikao hicho kimefanyika wakati Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe, akiwepo jijini hapa na kuna tetesi atakutana na viongozi hao kujadili suala hilo.
Source: Gazeti la Uhuru, Juni 27, 2011
DALILI ZA MVUA NI MAWINGU; CDM MKAE CHONJO!
* Milioni 50/- za hongo zawatesa
* Ujumbe wa Dk. Slaa wapondwa
NA SHAABAN MDOE, ARUSHA
HALI si shwari ndani ya uongozi wa CHADEMA wilayani Arusha, baada ya kuzuka mvutano, wanachama wakitaka uchaguzi ufanyike ili kuwaondoa viongozi walio madarakani. Imeelezwa kuwa viongozi wa kata 18 wilayani humo walikaa kikao na kukubaliana viongozi wa mkoa waitishe uchaguzi, wakidai waliopo madarakani si halali. Akizungumza baada ya kumalizika kikao hicho, kwenye hoteli ya Palson, mjini hapa, Mwenyekiti wa kata ya Kati, Shubeti Rashid, alisema viongozi wote wa wilaya wamekuwa wakikaimu nafasi walizonazo kwa muda mrefu. "Wanakaimu nafasi hizo kwa zaidi ya mwaka mmoja unaotakiwa kikatiba," alisema. Aliwataja viongozi wanaokaimu nafasi hizo kuwa, Mwenyekiti wa chama hicho wa wilaya, Derick Magoma, Katibu wa uenezi wa wilaya, Gabriel Lucas, Mwenyekiti wa baraza la wanawake, Joyce Mukya, Katibu wake Margaret Olotu na wajumbe wanne wa kamati ya utendaji wilaya. Rashid alisema kukaimiwa kwa nafasi hizo kwa kipindi kirefu kumetokana na sababu za maslahi binafsi kabla ya kuelekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Alisema licha ya uchaguzi kutangazwa miezi minne iliyopita ulifutwa bila maelezo. Uchaguzi ulitangazwa miezi minne iliyopita lakini kuna tetesi watu walihongwa sh. milioni 50 ili uahirishwe kwa kuwa walidai wanachama waliokuwa wakigombea nafasi hizo ni mamluki na wasingekuwa na faida katika kuwawakilisha wanachama," alisema Rashid.
Alisema viongozi wa kata 18 wameweka maazimio kadhaa, likiwemo la kutoa siku saba ili uongozi wa chama hicho mkoa utoe tamko kuhusu uchaguzi.
Rashid alisema uongozi ukishindwa watatumia nguvu ya umma kuitisha uchaguzi.
Naye Mwenyekiti wa chama hicho kata ya Terati, Gerald Josephat, alisema nguvu ya umma itakayotumika itahusisha maandamano ili kushinikiza viongozi wasio halali kutoka madarakani kupisha uchaguzi ufanyike. Alisema pia watazifunga ofisi za mkoa hadi uchaguzi utakapoitishwa. Viongozi hao waliutaka uongozi wa mkoa kuhakikisha chama hicho kinakuwa na ofisi ya wilaya, kwani ni aibu kwa chama chenye wabunge watatu kukosa ofisi, licha ya kupokea ruzuku ya sh. 800,000 kila mwezi ambazo zingeweza kulipia kodi ya pango.
Walisema wabunge hao kwa umoja wao kama wasingekuwa na maslahi binafsi wangeweza kuchagia kupatikana ofisi na mahitaji mengine kama njia ya kukijenga chama hicho. Viongozi hao waliponda maagizo ya Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, aliyoyatoa kupitia ujumbe mfupi wa maneno, akiwataka waache kujadili mambo hayo. Kwa mujibu wa viongozi hao, ujumbe huo unaonyesha nia ya kuficha maovu na unaweza kisambaratisha chama hicho. Kikao hicho kimefanyika wakati Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe, akiwepo jijini hapa na kuna tetesi atakutana na viongozi hao kujadili suala hilo.
Source: Gazeti la Uhuru, Juni 27, 2011
DALILI ZA MVUA NI MAWINGU; CDM MKAE CHONJO!