Nguvu ya msemo "HAPA KAZI TU" imeishia wapi?

Nguvu ya msemo "HAPA KAZI TU" imeishia wapi?

Sigara Kali

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2017
Posts
3,711
Reaction score
8,765
Wakati utawala wa awamu ya 5 chini ya Magufuli ulikuja na kauli mbiu ya 'HAPA KAZI TU'

Watu maeneo mbali mbali nchini walitumia hii kauli mbiu kwa kasi sana,mitaani ukikutana na watu ni kusema hapa kazi tu hata wale wasio na kazi walijinasibu na hapa kazi tu.

Rais mwenyewe wakati anaanza kila hotuba yake lazima aweka kibwagizo cha "Chini ya serikali yangu ni kazi tu"

Wanyonge wakafurahia na kuwa na natumaini ya unafuu wa maisha hivyo wakazidi kuipamba kauli ya hapa kazi tu wakati kazi zenyewe hakuna.

Lakini siku za hivi karibuni naona hii kauli mbiu kupotea na sasa kila mtu analia na kauli ya "Hali ngumu kiuchumi/Maisha" watu wasiojulikana,Ukosefu wa Uhuru wa kutoa maoni dhidi ya serikali,kuokotwa kwa maiti kwenye fukwe za bahari ,wawekezaji wa nje kulia na Sera mbovu za uwekezaji nchini,watumishi wa umma kutoongezewa mishahara na Shida nyingine nyingi.

Neno HAPA KAZI TU linazidi kupotea kuanzia mitandao hadi mitaani
Nani atashabikia kusema HAPA KAZI TU ili hali hajui mlo wa siku ataupataje,ajira hakuna ,wenye ajira wanakatishwa tamaa ,Nani atafurahia HAPA KAZI TU.

N.B Chini ya utawala wa Magufuli na CCM tusitegemee maendeleo ya kiuchumi na nchi kiujumla
OVA[emoji41] [emoji41] [emoji41]
 
Umenifanya nikumbuke enzi hizo chuo mwaka wa kwanza nasoma Business Law, hapa naona hii kauli ilikua INVITATION TO TREATY. Jamaa alituita kumpigia kura kwa kauli ilokua na hamasa ya utendaji kazi na kuleta maendeleo na tukaingia mkenge bila kuchunguza kama alikua na sera to implement huu msemo.

Makosa si yake bali ni ya waTZ tuliomchagua. Alichotaka kashapata. 2020 we have another chance to amend our mistakes but I bet kwa mwendo huu ikifika 2019 zile 50M kila kijiji zinatoka na atachaguliwa tena.
 
Hapa kazi tu...!
Ilikuwa na kauli wanayotoa wale wageni katika kazi...

Wengine tulikuwa tunawatazama tu..
 
mr kipara Bhana alikuwa anaomba kura kwa huruma kupata uraisi kafungua makucha.

2020 akishinda atakuwa katili zaidi kwakuwa hana chakupoteza.
 
Umenifanya nikumbuke enzi hizo chuo mwaka wa kwanza nasoma Business Law, hapa naona hii kauli ilikua INVITATION TO TREATY. Jamaa alituita kumpigia kura kwa kauli ilokua na hamasa ya utendaji kazi na kuleta maendeleo na tukaingia mkenge bila kuchunguza kama alikua na sera to implement huu msemo.
Makosa si yake bali ni ya waTZ tuliomchagua. Alichotaka kashapata. 2020 we have another chance to amend our mistakes but I bet kwa mwendo huu ikifika 2019 zile 50M kila kijiji zinatoka na atachaguliwa tena.
Ndio siasa hizo mkuu.
 
Juzi niliingia supermarket moja hapa Dodoma (iliyoko kwenye kituo cha mafuta karibu na taa za kuongozea magari njia panda airport) nilishangaa kuambiwa kipande cha sabuni ya kuogea aina ya Detol ni sh. 3,000! Ajabu kweli kweli.
 
Tanzania ya viwanda sijui imepotelea wapi..si isikii kabisa!!
 
Watu wameshituka na ndio maana hata ile kauli yake ya niombeeni inaelekea kufa sasaivi
 
Wakati utawala wa awamu ya 5 chini ya Magufuli ulikuja na kauli mbiu ya 'HAPA KAZI TU'

Watu maeneo mbali mbali nchini walitumia hii kauli mbiu kwa kasi sana,mitaani ukikutana na watu ni kusema hapa kazi tu hata wale wasio na kazi walijinasibu na hapa kazi tu.

Rais mwenyewe wakati anaanza kila hotuba yake lazima aweka kibwagizo cha "Chini ya serikali yangu ni kazi tu"

Wanyonge wakafurahia na kuwa na natumaini ya unafuu wa maisha hivyo wakazidi kuipamba kauli ya hapa kazi tu wakati kazi zenyewe hakuna
Lakini siku za hivi karibuni naona hii kauli mbiu kupotea na sasa kila mtu analia na kauli ya "Hali ngumu kiuchumi/Maisha" watu wasiojulikana,Ukosefu wa Uhuru wa kutoa maoni dhidi ya serikali,kuokotwa kwa maiti kwenye fukwe za bahari ,wawekezaji wa nje kulia na Sera mbovu za uwekezaji nchini,watumishi wa umma kutoongezewa mishahara na Shida nyingine nyingi
Neno HAPA KAZI TU linazidi kupotea kuanzia mitandao hadi mitaani
Nani atashabikia kusema HAPA KAZI TU ili hali hajui mlo wa siku ataupataje,ajira hakuna ,wenye ajira wanakatishwa tamaa ,Nani atafurahia HAPA KAZI TU.

N.B Chini ya utawala wa Magufuli na CCM tusitegemee maendeleo ya kiuchumi na nchi kiujumla
OVA[emoji41] [emoji41] [emoji41]

Ni baada ya watanzania wenye akili ya kutafakari mambo kwa kina kugundua kuwa maisha ya 80% ya watz ni mabaya kuliko kipindi chochote kilichowahi kutokea ktk taifa hili .....maana maisha ya watz yanazidi kuwa duni, aliyekuwa anapata milo miwili sasahv anapata mmoja tu tena kwa shida sana, maelfu ya watz wamepoteza ajira ktk sekta mbalimbali serikalini na mashirika ya umma(uhakiki wa vyeti) kwa kupunguzwa kazi (migodini) na biashara kufungwa,ahadi ya tz ya viwanda(viwonder) na ajira za kumwaga bado ni ndoto za halinacha!

Hivyo hapa kazi tu watz wanaishuhudia kwy kuzibiti uhuru wa habari/ kuongea(kufungiwa kwa vyombo vya habari nk nk), kudhibiti vyama vya upinzani na wakosoaji(kamatakamata na,utekekaji na majaribio ya mauaji) hivyo imepoteza mvuto na watz wengi wamekata tamaa....
 
Back
Top Bottom