Nguvu ya Maamuzi juu ya Maisha Yako ya Kitajiri hapa Duniani

The Retired Planner

Senior Member
Sep 22, 2015
188
241
Wasalaaaaaaam Wanajamvi

Leo nimeona nifunguke kwa upande huu, kama “heading” yangu inavyosema ili kusaidia wanajamvi wenzangu kuondokana na hali hii ngumu ya kimaisha ambayo kwayo sisi watanzania tulio wengi tumekuwa tukilalamika kila uchwao ya kwamba “ “MAISHA HAYASOGEI”

Nianze kwa kusema, wengi wetu tumekua tukisikia kelele za wadau mbalimbali kuhusu kujikwamua kiuchumi kwa kufanya Biashara au ajasiriamali na kuondokana na dhana ya KUAJIRIWA. Sikawii kusema wengi tumekuwa tukiyatupilia mbali mawazo hayo kwa sababu 1 au 2 hivi; utasikia mtu akisema

1. Mtaji wa hiyo Biashara/Ujasiriamali nautolea wapi wakati mimi ndio kwanza nimemaliza chuo/shule au;

2. Niache kazi (Kuajiriwa) wakati bado sijajipanga?, natafuta mtaji kwanza halafu baadae nianzishe Biashara yangu

Ngaja niseme hivi wadau, tunajicheleweshea wenyewe hayo maisha mazuri ya asali na maziwa. Mafanikio yangu ama yako yapo kwenye maamuzi yako binafsi. Ni mimi au wewe wa kuamua sasa nahitaji kuwa na pesa kwa kiasi gani.

Ajira tulizonazo zinatusaidia tu kupata pesa ya kuendesha maisha tena yale ya kawaida sana. Mwezi haujaisha lakini kamshahara kako kamekatika siku nyingi sana kutokana na majukumu tuliyonayo kifamilia na kijamii kwa ujumla na kama ofisi yako haina yale magumashi wanayopigaga wenzetu, basi madeni yanaanzia hapo mpaka mshahara mwingine utakapokuja. Mwisho wa siku mshahara wako unakuwa ni nusu kulipia madeni na nusu kukusogeza tena kwenye nusu nyingine ya mwezi ujao.

Hali hii ya maisha itaendelea hivyo mpaka pale utakapofanya MAAMUZI wewe mwenyewe(kwa ku‘resign’) ama kwa kusaidiwa na mwajiri wako (kwa maana ya kufukuzwa kazi). Kwani hata mwajiri wako akikuongeza mshahara bado matumizi yako pia huongezeka. Hivyo hali huendelea kuwa ile ile.

Maamuzi ya kile unachokihitaji kwa maisha bora ukijumlisha na jitihada stahiki kwenye hayo maamuzi, amini usiamini utaona ni kama ndoto kwenye maisha yako. Nina mifano kadhaa ya marafiki zangu ambao walifukuzwa kazi na kwa kupitia hali hiyo walijua hakuna namna nyingine ya haraka ya kuendelea kuwaingizia kipato ili familia zao zisione hilo “gap”. Basi WAKAAMUA kungia kwenye Biashara na kufanya yale mambo ambayo kabla walikuwa wakiyapenda na kufikiria kuyafanya lakini kwa sababu ya Ajira zao walishindwa na kudhani walistahili kutafuta mtaji kwanza.

Hivi leo hakuna hata mmoja ambaye utamwambia arudi kuajiriwa akakuelewa unampigia stori gani. Kimsingi walifanya MAAMUZI na wanayaona matunda ya MAAMUZI yao. Haya sasa tuachane na hizi stori nyingi, nashauri kuanzia muda huu ambao umemaliza kusoma hizi hadithi ambazo wengine watadhani ni zile za aina ya kusadikika, Ufanye UAMUZI.

Sijakwambia uache kazi (kwa wewe uliye kazini kwa sasa), na kwa wewe ambae ulikuwa unatafuta kazi achana na mawazo hayo, naomba vile vitu ambavyo ulikuwa unafikiria kuvifanya na ukadhani vinahitaji mtaji ili kuviaanza vianze sasa. Kinachohitajika hapa ni MAAMUZI na sio Mtaji.

Kama unadhani haiwezekani, mimi nakwambia INAWEZEKANA na naomba unitafute kwa ushauri zaidi endapo unadhani unahitaji ushauri zaidi. Tanzania hii ni yetu na ninakuomba kwa moyo wote kabisa tuijenge kwa pamoja.


MAAMUZI + JITIHADA = MAFANIKIO
 
Mkuu, nakuelewa sana lakini tatizo linabakia palepale, MTAJI.

Ukitaga kuwa mfugaji unahitaji MTAJI

Ukitaka kuwa IMPORTER au EXPORTER wa aina yoyote ile, unahitaji MTAJI.

Ukitaka kuanzisha duka la rejareja, supermarket, car wash centre, berber shop, unahitaji MTAJI.

Kabla ya hapo unahitaji BUSINESS PLAN

Ukiwa huna hata TIN numba unahitaji kujiandikisha na pia biashara isajiliwe kule BRELA.

Hivyo mtu kama yupo kazini anahitaji extra mile kufanya uamuzi wa kuwa na biashara ya pembeni kwanza kabla ya kuacha ajira rasmi.

Hivyo inahitajika MKAKATI au Strategy kabla ya kuamua kuwa mjasirimali na pia akiba ya kutosha hata kama unaamua tu kwamba liwalo na liwe utoke kwenye ajira, yaani uwe na AKIBA YA KUTOSHA BENKI.

Hii akiba ya kutosha benki haihusiani na MTAJI wa biashara unaoutafuta.
 
Mkuu, nakuelewa sana lakini tatizo linabakia palepale, MTAJI.

Ukitaga kuwa mfugaji unahitaji MTAJI

Ukitaka kuwa IMPORTER au EXPORTER wa aina yoyote ile, unahitaji MTAJI.

Ukitaka kuanzisha duka la rejareja, supermarket, car wash centre, berber shop, unahitaji MTAJI.

Kbla ya hapo unahitaji BUSINESS PLAN

Ukiwa huna hata TIN numba unahitaji kujiandikisha na pia biashara isajiliwe kule BRELA.

Hivyo mtu kam ayupo kazini anahitaji extra mile kufanya uamuzi wa kuwa na biashara ya pembeni kwanza kabla ya kuacha ajira rasmi.

Hivyo inahitajika MKAKATI au Strategy kabla ya kuamua kuwa mjasirimali na pia akiba ya kutosha hata kama unaamua tu kwamba liwalo na liwe utoke kwenye ajira, yaani uwe na AKIBA YA KUTOSHA BENKI.

Hii akiba ya kutosha benki haihusiani na MTAJI wa biashara unaoutafuta.
Mkuu, shida yetu waTz ndio iko hapo. Tunafikiri kuwa na mtaji kwanza baada tu ya kufikiria wazo la kufanya na kushindwa kuanza jambo kwa kisingizio cha mtaji. Sikatai kabisa ya kwamba kufanya hayo yote yanahitaji mtaji, lakini je ni lazima kuanza kwa ukubwa huo?. mfano mdogo tu kwenye hilo la kuku wa kufuga

kabla sijaanza kufuga kuku, nilifikiria ni jinsi gani nitapata pesa kwa ajili ya kununua wale kuku 10 wa kuanzia. Je nimefanya jitihada gani kuhakikisha napata ile TZS 20,000 ya kununulia wale kuku 10 wa kuanzia na kumwomba jirani yangu achanganye na wale wake na mimi kujitoa kufanya usafi kwenye mabanda yake kuhakikisha wanakua na kuzaaa matunda niliyoyatarajia?. Hapa ndipo wengi tunapoanzia kufeli
 
Mkuu, shida yetu waTz ndio iko hapo. Tunafikiri kuwa na mtaji kwanza baada tu ya kufikiria wazo la kufanya na kushindwa kuanza jambo kwa kisingizio cha mtaji. Sikatai kabisa ya kwamba kufanya hayo yote yanahitaji mtaji, lakini je ni lazima kuanza kwa ukubwa huo?. mfano mdogo tu kwenye hilo la kuku wa kufuga

kabla sijaanza kufuga kuku, nilifikiria ni jinsi gani nitapata pesa kwa ajili ya kununua wale kuku 10 wa kuanzia. Je nimefanya jitihada gani kuhakikisha napata ile TZS 20,000 ya kununulia wale kuku 10 wa kuanzia na kumwomba jirani yangu achanganye na wale wake na mimi kujitoa kufanya usafi kwenye mabanda yake kuhakikisha wanakua na kuzaaa matunda niliyoyatarajia?. Hapa ndipo wengi tunapoanzia kufeli

Lakini mku, si kil mtu anataka kuwa mfugaji.

Katika zama hizi kuna maeneo mengi ya ujarisimali na hayo yanatofautiana kwenye startup Capital.

Hivyo mtu anaweza kuwa na ideas nyingi lakini akawa anakwama hapo - wapi atapata mtaji.

Mfano tu ni duka la kawaida tu la rejareja je linahitaji mtaji kiasi gani?
 
Mkuu, nakuelewa sana lakini tatizo linabakia palepale, MTAJI.

Ukitaga kuwa mfugaji unahitaji MTAJI

Ukitaka kuwa IMPORTER au EXPORTER wa aina yoyote ile, unahitaji MTAJI.

Ukitaka kuanzisha duka la rejareja, supermarket, car wash centre, berber shop, unahitaji MTAJI.

Kbla ya hapo unahitaji BUSINESS PLAN

Ukiwa huna hata TIN numba unahitaji kujiandikisha na pia biashara isajiliwe kule BRELA.

Hivyo mtu kam ayupo kazini anahitaji extra mile kufanya uamuzi wa kuwa na biashara ya pembeni kwanza kabla ya kuacha ajira rasmi.

Hivyo inahitajika MKAKATI au Strategy kabla ya kuamua kuwa mjasirimali na pia akiba ya kutosha hata kama unaamua tu kwamba liwalo na liwe utoke kwenye ajira, yaani uwe na AKIBA YA KUTOSHA BENKI.

Hii akiba ya kutosha benki haihusiani na MTAJI wa biashara unaoutafuta.
maamuzi yako na akili yako ndo mtaji namba 1 wa kukufanya ufike mahali unataka boss
 
Lakini mku, si kil mtu anataka kuwa mfugaji.

Katika zama jizi kuna maeneo mengi ya ujarisimali na hayo yanatofautiana kwenye startup Capital.

Hivyo mtu anaweza kuwa na ideas nyingi lakini akawa anakwama hapo - wapi atapata mtaji.

Mfano tu ni duka la kawaida tu la rejareja je linahitaji mtaji kiasi gani?
@ Richard inategemea na mtu binafsi anataka afanye nini. Lakini point ya msingi hapa ni kwamba lazima uanze chini ili uweze kujua zaidi kile kitu unachokifanya. Wengi tunataka kuanza kama tulikuwepo miaka 10 iliyopita. Hiyo sio sahihi hata kidogo. Anza mdogo mdogo tu na ndipo utakapopata kuijua zaidi biashara unayofanya au huo ujasiriamali unaofanya.

Na kama ulivyosema kuwa ideas zipo nyingi, basi anza na ile ambayo haikuhitaji start up capital kubwa ili ujitengenezee mtaji zaidi kwa ajili ya zile ideas zinazohitaji mtaji mkubwa.

Cha msingi hapa ni kufanya MAAMUZI ya kuanza. Just start...................!
 
Shida iko wapi mkuu?
Katika mafanikio ni lazima uanze na wazo upo sahihi bila kuzingatia neno mtaji
baada ya hapo ni raslimali
hapa unajiangalia utafanya nini? utafanya nini? kwa muda upi? na focus kundi lipi? maana raslimali watu ndio ya kufocus zaidi
umeliongelea hili sana thanks lakini tukirudi kwa ulimwengu wa sasa kile ukisemacho sicho hicho
ni bora uniambie kabla hujaacha kazi anza kutafuta maarifa yakuongoze
hao rafiki zako walikuwa na maarifa tayari yaliyowasongesha hapo walipofika


sikatai kuanza zero kwa kujitoa nguvu yako hapa ni mtaji nguvu ndio utakuongoza mpaka mafanikio LAKINI KITU KIKUBWA KABLA YA PESA
NI MAARIFA

KWANINI NASEMA HIVYO



biashara nyingi zinahitaji kulelewa na wewe binafsi hasa kipindi cha mwanzo mfano upo kwangu mimi mwenyewe niliwekeza ten million katika biashara yangu lakini ikaibiwa

nilichojifunza kwanza nilikuwa mbali nayo pili pesa nilienda nje ya hesabu bussiness plan ni kiongozi tu mara nyingi ni nje unapoingia field

let say huna kazi umeibiwa umerudi zero na hapo ndipo unapotegemea huoni ni tatizo kubwa hilo

lakini ukiwa na maarifa kuongoza kila kitu ni rahisi na haya nilipoyapata kiukweli im different kimtazamo

MAARIFA + MAAMUZI+ UWAJIBIKAJI=MAFANIKIO
 
Mtaji unachukua nafasi kubwa sana hata kama unalikwepa suala hilo. Mf. Kufuga kuku wa biashara huwez kufugia kwenye nyumba ya kupanga vinginevyo kuna hela ya Ziada ya kumlipa mwenye nyumba. Banda la kuku linahitaji pesa, dawa, chakula. Mtaji haukwepeki. We labda shauri jinsi ya kupata huo mtaji hata wa hiyo biashara ndogo.
 
Mkuu, nakuelewa sana lakini tatizo linabakia palepale, MTAJI.

Ukitaga kuwa mfugaji unahitaji MTAJI

Ukitaka kuwa IMPORTER au EXPORTER wa aina yoyote ile, unahitaji MTAJI.

Ukitaka kuanzisha duka la rejareja, supermarket, car wash centre, berber shop, unahitaji MTAJI.

Kbla ya hapo unahitaji BUSINESS PLAN

Ukiwa huna hata TIN numba unahitaji kujiandikisha na pia biashara isajiliwe kule BRELA.

Hivyo mtu kam ayupo kazini anahitaji extra mile kufanya uamuzi wa kuwa na biashara ya pembeni kwanza kabla ya kuacha ajira rasmi.

Hivyo inahitajika MKAKATI au Strategy kabla ya kuamua kuwa mjasirimali na pia akiba ya kutosha hata kama unaamua tu kwamba liwalo na liwe utoke kwenye ajira, yaani uwe na AKIBA YA KUTOSHA BENKI.

Hii akiba ya kutosha benki haihusiani na MTAJI wa biashara unaoutafuta.
Ukimchunguza sana bata huwezi Kuala. Mambo mengine hujiseti unapokuwa ndani ya biashara. Ukitaka uwe na kila kitu utasubiri sana.
 
Katika mafanikio ni lazima uanze na wazo upo sahihi bila kuzingatia neno mtaji
baada ya hapo ni raslimali
hapa unajiangalia utafanya nini? utafanya nini? kwa muda upi? na focus kundi lipi? maana raslimali watu ndio ya kufocus zaidi
umeliongelea hili sana thanks lakini tukirudi kwa ulimwengu wa sasa kile ukisemacho sicho hicho
ni bora uniambie kabla hujaacha kazi anza kutafuta maarifa yakuongoze
hao rafiki zako walikuwa na maarifa tayari yaliyowasongesha hapo walipofika


sikatai kuanza zero kwa kujitoa nguvu yako hapa ni mtaji nguvu ndio utakuongoza mpaka mafanikio LAKINI KITU KIKUBWA KABLA YA PESA
NI MAARIFA

KWANINI NASEMA HIVYO



biashara nyingi zinahitaji kulelewa na wewe binafsi hasa kipindi cha mwanzo mfano upo kwangu mimi mwenyewe niliwekeza ten million katika biashara yangu lakini ikaibiwa

nilichojifunza kwanza nilikuwa mbali nayo pili pesa nilienda nje ya hesabu bussiness plan ni kiongozi tu mara nyingi ni nje unapoingia field

let say huna kazi umeibiwa umerudi zero na hapo ndipo unapotegemea huoni ni tatizo kubwa hilo

lakini ukiwa na maarifa kuongoza kila kitu ni rahisi na haya nilipoyapata kiukweli im different kimtazamo

MAARIFA + MAAMUZI+ UWAJIBIKAJI=MAFANIKIO

Mkuu, hapa assumption iliyopo ni kwamba tayari unakila kitu ( maarifa endapo wewe ni mwanafunzi ndio umetoka chuo au ni mwajiriwa tayari unajua nini unataka kufanya, lakini pia hata idea ya nini unataka kufanya unayo) shida ni muda gani uanze kufanya ndio linakuja suala la , oooh sina mtaji, oooh sina mtaji.

Hivi vitu havitasogea kama kila siku tutalalamika kuwa hatuna mtaji. Technology imekuja kwa mapana zaidi, kuna njia mbadala nyingi sana za kuitumia hii technology kuweza kukufikisha wapi unataka kuwa
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Mtaji unachukua nafasi kubwa sana hata kama unalikwepa suala hilo. Mf. Kufuga kuku wa biashara huwez kufugia kwenye nyumba ya kupanga vinginevyo kuna hela ya Ziada ya kumlipa mwenye nyumba. Banda la kuku linahitaji pesa, dawa, chakula. Mtaji haukwepeki. We labda shauri jinsi ya kupata huo mtaji hata wa hiyo biashara ndogo.
Mkuu achana na habari ya kudhani bila mtaji huwezi fanya kitu. Ngoja nikupe mfano hapo hapo kwenye hiyo biashara ya ufugaji wa kuku. Kwani kuna ubaya gani wewe ukianza kuchukua order na kusupply hao kuku / vifaranga kwa wahitaji kwa kuingia ubia na wanaozalisha vifaranga halafu baada ya kula commission zako za kutosha na wewe ukaanzisha yako?. Hii ni njia rahisi ya wewe usiekuwa na mtaji ukaanza kwa kufanya marketing ya wenzako kwanza baadae ikakusaidia hata wewe kuwa na uzoefu wa kutosha kwenye hiyo field.

Shida yetu sisi ni kutaka vitu vikubwa kana kwamba ionekane kama tulikuwepo miaka 20 iliyopita. Ni vizuri kuanzia chini then ukapanda juu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom