Nguvu ya Maamuzi juu ya Maisha Yako ya Kitajiri hapa Duniani

Mkuu achana na habari ya kudhani bila mtaji huwezi fanya kitu. Ngoja nikupe mfano hapo hapo kwenye hiyo biashara ya ufugaji wa kuku. Kwani kuna ubaya gani wewe ukianza kuchukua order na kusupply hao kuku / vifaranga kwa wahitaji kwa kuingia ubia na wanaozalisha vifaranga halafu baada ya kula commission zako za kutosha na wewe ukaanzisha yako?. Hii ni njia rahisi ya wewe usiekuwa na mtaji ukaanza kwa kufanya marketing ya wenzako kwanza baadae ikakusaidia hata wewe kuwa na uzoefu wa kutosha kwenye hiyo field.

Shida yetu sisi ni kutaka vitu vikubwa kana kwamba ionekane kama tulikuwepo miaka 20 iliyopita. Ni vizuri kuanzia chini then ukapanda juu.
Sasa huko si ndio kuajiliwa kwanza ambako wewe umekataa. Kumbe ukubaliane sasa na wale wanaojiliwa kwanza ili kutafuta mtaji. Mpaka uingie huo ubia unadhan ni kuamka tu unapewa tenda?
 
Sasa huko si ndio kuajiliwa kwanza ambako wewe umekataa. Kumbe ukubaliane sasa na wale wanaojiliwa kwanza ili kutafuta mtaji. Mpaka uingie huo ubia unadhan ni kuamka tu unapewa tenda?

Ninachokiongelea hapa mkuu, ni wewe kuchukua hatua (kufanya maamuzi) ya kuanza kuishi kwenye ndoto zako. Hata ukisoma vizuri hoja yangu kule juu, sikukwambia kwa wewe ulieajiriwa uache kazi. Nilisema anza na ufanye uamuzi wa kufanya ulitakalo.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Ahsante Water Bearer Kwa Maneno Yako. Kwamba "MAAMUZI" Kama Silaha Ya Maisha Na Wahenga Husema "Penye Nia Pana Njia"...
Nikurejeshe Kidogo: Umesema Ukitaka Kupata Pesa Kiasi Fulani.. Ni Maamuzi. Ukitaka Kuishi Maisha Ya Juu Kiasi Gani Ni Maamuzi...
Nikupe Wewe Hongera Kwa Kufika Hapo Ulipofikia..

Lakini Pia Kwako Na Kwa Ndugu Mwana Jf, UZINGATIE, JEURI YA MIPANGO NI PESA KAMA JEURI YA TAJIRI, NA JEURI YA MASIKINI NI NGUVU ZAKE, MUDA, NA JUHUDI Ambayo Umeigusia Kidogo Kwenye Maneno Yako Uzingatie Pia MAAMUZI SIYO UTIMILIFU.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Mkuu, nakuelewa sana lakini tatizo linabakia palepale, MTAJI.

Ukitaga kuwa mfugaji unahitaji MTAJI

Ukitaka kuwa IMPORTER au EXPORTER wa aina yoyote ile, unahitaji MTAJI.

Ukitaka kuanzisha duka la rejareja, supermarket, car wash centre, berber shop, unahitaji MTAJI.

Kbla ya hapo unahitaji BUSINESS PLAN

Ukiwa huna hata TIN numba unahitaji kujiandikisha na pia biashara isajiliwe kule BRELA.

Hivyo mtu kam ayupo kazini anahitaji extra mile kufanya uamuzi wa kuwa na biashara ya pembeni kwanza kabla ya kuacha ajira rasmi.

Hivyo inahitajika MKAKATI au Strategy kabla ya kuamua kuwa mjasirimali na pia akiba ya kutosha hata kama unaamua tu kwamba liwalo na liwe utoke kwenye ajira, yaani uwe na AKIBA YA KUTOSHA BENKI.

Hii akiba ya kutosha benki haihusiani na MTAJI wa biashara unaoutafuta.
Mtaji wa kwanza ni fikla zako.jaribu kutazama hii.nimejenga nyumba na nimeweka fensi ya ukuta ktk eneo langu,mawazo yakaniijia why nipande majani na miti ya kimvuli pekee?nikaachana na majani na miti na nikatengeneza vitalu vya mboga mboga humo ndani ndo bustani yangu ya kupumzikia,baada ya muda nikaweka bango getini kwa nje ''TUNAUZA MBOGA MBOGA KILA SIKU''KARIBUNI..na mala wateja majirani wakaanza kua wanakuja kununua mboga kila siku,habari zikaenda mtaa mpaka mtaa,na pesa hyo kidogo kidogo nikafikia kupata mtaji wa kuanzisha biashara mtaani.na mpaka sasa nina duka la kuuza Gas na vifaa vyake,mdogo mdogo huku nikimuomba MUNGU..over
 
Mtaji wa kwanza ni fikla zako.jaribu kutazama hii.nimejenga nyumba na nimeweka fensi ya ukuta ktk eneo langu,mawazo yakaniijia why nipande majani na miti ya kimvuli pekee?nikaachana na majani na miti na nikatengeneza vitalu vya mboga mboga humo ndani ndo bustani yangu ya kupumzikia,baada ya muda nikaweka bango getini kwa nje ''TUNAUZA MBOGA MBOGA KILA SIKU''KARIBUNI..na mala wateja majirani wakaanza kua wanakuja kununua mboga kila siku,habari zikaenda mtaa mpaka mtaa,na pesa hyo kidogo kidogo nikafikia kupata mtaji wa kuanzisha biashara mtaani.na mpaka sasa nina duka la kuuza Gas na vifaa vyake,mdogo mdogo huku nikimuomba MUNGU..over

Sawasawa mkuu, ideas start at home.

Hiyo ndiyo njia pekee na rahisi kabisa kuanzisha biashara au kuwa mjasirimali.
 
Mtaji unachukua nafasi kubwa sana hata kama unalikwepa suala hilo. Mf. Kufuga kuku wa biashara huwez kufugia kwenye nyumba ya kupanga vinginevyo kuna hela ya Ziada ya kumlipa mwenye nyumba. Banda la kuku linahitaji pesa, dawa, chakula. Mtaji haukwepeki. We labda shauri jinsi ya kupata huo mtaji hata wa hiyo biashara ndogo.
bila kuwa na wazo huwezi kuchemsha akili ya jinsi ya kutafuta mtajii. Sasa bila wazo utajuaje kuhusu kiasi cha mtaji mimnimum ili uweze kuanza? Nikikuuliza mtaji kiasi gani unahitaaji utaishia tu kusema milioni 50. Nikikuuliza why milioni 50 hutakuwa na jibu. Naomba usome kwa makini nilichoandika kwenye sentensi hii ukielewe kabla hujaweka msisitizo kwamba tatizo ni mtaji. Ukisema tatizo mtaji inamaana una huna goal.Na huwezi kuachive kitu bila goal. Goal inaanza kutokana na wazooo
 
bila kuwa na wazo huwezi kuchemsha akili ya jinsi ya kutafuta mtajii. Sasa bila wazo utajuaje kuhusu kiasi cha mtaji mimnimum ili uweze kuanza? Nikikuuliza mtaji kiasi gani unahitaaji utaishia tu kusema milioni 50. Nikikuuliza why milioni 50 hutakuwa na jibu. Naomba usome kwa makini nilichoandika kwenye sentensi hii ukielewe kabla hujaweka msisitizo kwamba tatizo ni mtaji. Ukisema tatizo mtaji inamaana una huna goal.Na huwezi kuachive kitu bila goal. Goal inaanza kutokana na wazooo
Nakubaliana na wewe asilimia100. Watu wengi wana mawazo lakini implementation inakua ngumu. By the way mi sikupingi kabisa na ni kweli kwamba lazima ianze"fikra". Lakini mtaji huwezi kuutupilia mbali

Sent from my HUAWEI G730-U00 using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Wasalaaaaaaam Wanajamvi

Leo nimeona nifunguke kwa upande huu, kama “heading” yangu inavyosema ili kusaidia wanajamvi wenzangu kuondokana na hali hii ngumu ya kimaisha ambayo kwayo sisi watanzania tulio wengi tumekuwa tukilalamika kila uchwao ya kwamba “ “MAISHA HAYASOGEI”

Nianze kwa kusema, wengi wetu tumekua tukisikia kelele za wadau mbalimbali kuhusu kujikwamua kiuchumi kwa kufanya Biashara au ajasiriamali na kuondokana na dhana ya KUAJIRIWA. Sikawii kusema wengi tumekuwa tukiyatupilia mbali mawazo hayo kwa sababu 1 au 2 hivi; utasikia mtu akisema

1. Mtaji wa hiyo Biashara/Ujasiriamali nautolea wapi wakati mimi ndio kwanza nimemaliza chuo/shule au;

2. Niache kazi (Kuajiriwa) wakati bado sijajipanga?, natafuta mtaji kwanza halafu baadae nianzishe Biashara yangu

Ngaja niseme hivi wadau, tunajicheleweshea wenyewe hayo maisha mazuri ya asali na maziwa. Mafanikio yangu ama yako yapo kwenye maamuzi yako binafsi. Ni mimi au wewe wa kuamua sasa nahitaji kuwa na pesa kwa kiasi gani.

Ajira tulizonazo zinatusaidia tu kupata pesa ya kuendesha maisha tena yale ya kawaida sana. Mwezi haujaisha lakini kamshahara kako kamekatika siku nyingi sana kutokana na majukumu tuliyonayo kifamilia na kijamii kwa ujumla na kama ofisi yako haina yale magumashi wanayopigaga wenzetu, basi madeni yanaanzia hapo mpaka mshahara mwingine utakapokuja. Mwisho wa siku mshahara wako unakuwa ni nusu kulipia madeni na nusu kukusogeza tena kwenye nusu nyingine ya mwezi ujao.

Hali hii ya maisha itaendelea hivyo mpaka pale utakapofanya MAAMUZI wewe mwenyewe(kwa ku‘resign’) ama kwa kusaidiwa na mwajiri wako (kwa maana ya kufukuzwa kazi). Kwani hata mwajiri wako akikuongeza mshahara bado matumizi yako pia huongezeka. Hivyo hali huendelea kuwa ile ile.

Maamuzi ya kile unachokihitaji kwa maisha bora ukijumlisha na jitihada stahiki kwenye hayo maamuzi, amini usiamini utaona ni kama ndoto kwenye maisha yako. Nina mifano kadhaa ya marafiki zangu ambao walifukuzwa kazi na kwa kupitia hali hiyo walijua hakuna namna nyingine ya haraka ya kuendelea kuwaingizia kipato ili familia zao zisione hilo “gap”. Basi WAKAAMUA kungia kwenye Biashara na kufanya yale mambo ambayo kabla walikuwa wakiyapenda na kufikiria kuyafanya lakini kwa sababu ya Ajira zao walishindwa na kudhani walistahili kutafuta mtaji kwanza.

Hivi leo hakuna hata mmoja ambaye utamwambia arudi kuajiriwa akakuelewa unampigia stori gani. Kimsingi walifanya MAAMUZI na wanayaona matunda ya MAAMUZI yao. Haya sasa tuachane na hizi stori nyingi, nashauri kuanzia muda huu ambao umemaliza kusoma hizi hadithi ambazo wengine watadhani ni zile za aina ya kusadikika, Ufanye UAMUZI.

Sijakwambia uache kazi (kwa wewe uliye kazini kwa sasa), na kwa wewe ambae ulikuwa unatafuta kazi achana na mawazo hayo, naomba vile vitu ambavyo ulikuwa unafikiria kuvifanya na ukadhani vinahitaji mtaji ili kuviaanza vianze sasa. Kinachohitajika hapa ni MAAMUZI na sio Mtaji.

Kama unadhani haiwezekani, mimi nakwambia INAWEZEKANA na naomba unitafute kwa ushauri zaidi endapo unadhani unahitaji ushauri zaidi. Tanzania hii ni yetu na ninakuomba kwa moyo wote kabisa tuijenge kwa pamoja.


MAAMUZI + JITIHADA = MAFANIKIO
Ha ha maisha ya kiafrika bhana. Sisi waafrika Bro akipata Kazi ukoo mzima unamuona mungu. Akisema ajiajili na kuwanyima msaada ha ha utasimamgwa mpaka ushangae. Cha muhimu ili tuweze kutoboa inatakiwa kuwa wewe Kama wewe
 
Nakubaliana na wewe asilimia100. Watu wengi wana mawazo lakini implementation inakua ngumu. By the way mi sikupingi kabisa na ni kweli kwamba lazima ianze"fikra". Lakini mtaji huwezi kuutupilia mbali

Sent from my HUAWEI G730-U00 using JamiiForums mobile app
Basi hilo wazi bado ni high level akijaingia kwenye sub conscious mind. Ushakuwa na wazu yaani ukitembea barabarani unaliwaza nakulifanyia imagization. Ukilal unaliota. Ukifika stejii hela itapatikana tu..teh teh
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Mmmh bila capital inawezekana vp labda ungefafanua ila mawazo ni mazuri kwani kazi za kuajiriwa zina mwisho tena unaweza ukawa mwisho mbaya maana kazini hakuna anayeishi kwa mshahara ni wizi mtupu umejaa
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Mkuu achana na habari ya kudhani bila mtaji huwezi fanya kitu. Ngoja nikupe mfano hapo hapo kwenye hiyo biashara ya ufugaji wa kuku. Kwani kuna ubaya gani wewe ukianza kuchukua order na kusupply hao kuku / vifaranga kwa wahitaji kwa kuingia ubia na wanaozalisha vifaranga halafu baada ya kula commission zako za kutosha na wewe ukaanzisha yako?. Hii ni njia rahisi ya wewe usiekuwa na mtaji ukaanza kwa kufanya marketing ya wenzako kwanza baadae ikakusaidia hata wewe kuwa na uzoefu wa kutosha kwenye hiyo field.

Shida yetu sisi ni kutaka vitu vikubwa kana kwamba ionekane kama tulikuwepo miaka 20 iliyopita. Ni vizuri kuanzia chini then ukapanda juu.
Nakuunga mkono ndugu. Shida ya yetu vijana ni uoga na kutotumia akili. Mara ya kwanza hata mm nilikuwa nafikiri kwamba mtaji ndio kitu cha kwanza lakin baada ya struggle za kutosha nmegundua kwamba shida ni wazo la utafanya nini,wapi, na nani, lini na kwa muda gani. Mfano mm nikiwa na digrii yangu nilifanyakazi ya ukondakta wa daladala hii baada ya kutafuta ajira bila kupata. Na kila siku nilkuwa sikosi kusave 30,000/ na kila wkend nlkuwa naweka benk sio chin ya 200,000/. Sasa kuna wasomi wangap wanachagua kaz na hawana kazi zaid ya kulia hakuna ajira hakuna mtaji
 
Mmmh bila capital inawezekana vp labda ungefafanua ila mawazo ni mazuri kwani kazi za kuajiriwa zina mwisho tena unaweza ukawa mwisho mbaya maana kazini hakuna anayeishi kwa mshahara ni wizi mtupu umejaa

Hili wazo la kuanzisha biashara bila mtaji weng hawaelewi. Ni hivi kwa mfano ww unataka kuwa na kiwanda cha kutengeneza bidhaa mbali mbali kama bakhresa lakin mtaji hauna. So 1. unawza anza kwa kujifunza kutengeza sabuni hizi z kawaida ,kuoka mikate,keki na biskuti. Then ukaanza kutengeneza kwa kiwango kidogo ukawa unasupply kwa tenda mashulen,makanisani kama wanasherehe au hata hospital binafsi. Baadae ukiwa na soko la uhakika na hauna hela za kununua malighafi zaid unaweza kuchukua kwa wanaouza jumla yaanitoka kwa wauzaji iliokuwa unajumua kwan muda wote uliokuwa unafanya kazi hivyowanakujua na wanajua biashara yako n hapa ndio utajua kwamba UAMINIFU NI MALI NA NI MTAJI.
2. Unaweza kuanza kwa kuajiriwa kwanza kwenye sekta yoyote na lengo lako likiwa ni kutafuta mtaji na sio vingnevyo. Sasa unakuta mtu ameajiriwa na anamilki gar ya kutembelea ya zaid ya 10 milion na bado anasema mtaji hakuna wkat gar hiyo ya 10 mil kwa mwaka anaigharamia zaid ya 5 mil nyingne kwa mafuta na service
 
Sasa huko si ndio kuajiliwa kwanza ambako wewe umekataa. Kumbe ukubaliane sasa na wale wanaojiliwa kwanza ili kutafuta mtaji. Mpaka uingie huo ubia unadhan ni kuamka tu unapewa tenda?
Kuajiriwa sio kubaya wala sio dhambi shida ni kujua kwann unaajiriwa. Coz weng wanajiriwa kwasababu wamesomea hicho kitu au kwasababu wanataka mshahara waishi vizur. Mfano mm nnarafiki zangu wao n madaktari waliajiriwa hosp ya serikal kwa miaka miwil na sasa waliisha acha kaz hosp ya serikal na wameanzisha kituo chao na wanafanya vizur sana na chaa ajabu wanawapa kaz za partime madaktari wenzao toka hosp ya serikal na wanawalipa wao. So mtaji sio shida shida unafanya shughul gan then unapataje hiyo capitalya kufanya hicho kitu. Weng tukiajiriwa cha kwanza gar,bata,totoz zote ulizozikosa basi lazma zijue hela unayo. Pia ishu ya kuwahi kujenga nyumba basi nyumba hii ikusaidie kupata mkopo ambao utakuboost kwenye biashara yako.
 
Mmmh bila capital inawezekana vp labda ungefafanua ila mawazo ni mazuri kwani kazi za kuajiriwa zina mwisho tena unaweza ukawa mwisho mbaya maana kazini hakuna anayeishi kwa mshahara ni wizi mtupu umejaa
Dah hepu pitia thread zote. Kwani mtaji huwa unapatikanaje? Mtaji unatafutwa hivi utapata tu mtaji kwa kuweka miguu juu unasema huna mtaji. teh teh teh. come on guys...Tusiwe wavivu kutafakariii...Kitu cha kwanza ni kujua unahitaji mtaji kiasi gani ili kukamilisha wazo lako. Sasa hapo ndo unaanza mbinu mbali mbali. Unaweza ukafanya saving ili uanze at least mahali fulani. Au unaweza kuomba support kwa ndugu marafiki na familia. Njia nyingine ni kwenda na wazo lako kwa watu wenye hela zao. Na wazo si wazo tu ili mradi eti lipo kichwani au sababu ya wewe kutaka kulima nyanya ni maneno uliyosikia kwamba nhyanya zinawatoa watu yaani unatakiwa uwe na a clear business plan sio kusema tu mimi nataka kulima nyanya halafu unaita ni wazo. Wazo linaandikwa chini na plan yake vizuri kabisa. Kama hujaliandika chini hilo si wazo una hallucinate tu..teh teh teh. Njia nyingine ni kujaribu kutafuta mkopo kwa ndugu na jamaa sasa hii inategemea uaminifu wako upo vipi. Kama unawafanyiaga usalnii basi hawawezi kukuchukulia serious. Lakini best way ya kuanza ni kuanza kidogo kidogo kwa kiasi kile ambacho umedunduliza mwenyewe. Huwezi kulaza damu kwa hela ambayo umeidunduliza mwenyewe kwa jasho kwa hiyo utapambana tu huku ukijifunza taratibu. Kama hujawahi fanya biashara ya milioni usikurupuke kutamani kufanya biashara ya milioni 20. Anza na milioni moja kwanza. Kwa mfano wewe ungesema wazo lako ni lipi ingesaidia zaidi..
 
Ha ha maisha ya kiafrika bhana. Sisi waafrika Bro akipata Kazi ukoo mzima unamuona mungu. Akisema ajiajili na kuwanyima msaada ha ha utasimamgwa mpaka ushangae. Cha muhimu ili tuweze kutoboa inatakiwa kuwa wewe Kama wewe
bora ya lawama muda mwingine kama unajua kile unachokitaka. Maana ukifanikiwa na wao wataona nmatunda yake watasau maneno maneno yote waliyokusema..
 
Mkuu, hapa assumption iliyopo ni kwamba tayari unakila kitu ( maarifa endapo wewe ni mwanafunzi ndio umetoka chuo au ni mwajiriwa tayari unajua nini unataka kufanya, lakini pia hata idea ya nini unataka kufanya unayo) shida ni muda gani uanze kufanya ndio linakuja suala la , oooh sina mtaji, oooh sina mtaji.

Hivi vitu havitasogea kama kila siku tutalalamika kuwa hatuna mtaji. Technology imekuja kwa mapana zaidi, kuna njia mbadala nyingi sana za kuitumia hii technology kuweza kukufikisha wapi unataka kuwa
Asante mkuu tupo pamoja mimi nadhani kitu kingine kikubwa ni kuamini kile ulichonacho pasipo kulinganisha ni kiasi gani maana shida ya wengi hakuna ubunifu kwa kile kidogo ulichonacho

mfano kazini kwetu tulizungukwa na migahawa mingi sana lakini akajitokeza mama mmoja upishi ukawa wa kitofauti sana kama ule wa nyumbani wengi tunajua vyakula vya vibandani lakini huyu alipata wateja wengi sana
kisa tu usafi katika upishi na ule ubora wa chakula chake lakini alikuwa akiuza 2000 kwa plate na alikuwa akiuza wakati wenzake wote 1500 kwa plate
 
Asante mkuu tupo pamoja mimi nadhani kitu kingine kikubwa ni kuamini kile ulichonacho pasipo kulinganisha ni kiasi gani maana shida ya wengi hakuna ubunifu kwa kile kidogo ulichonacho

mfano kazini kwetu tulizungukwa na migahawa mingi sana lakini akajitokeza mama mmoja upishi ukawa wa kitofauti sana kama ule wa nyumbani wengi tunajua vyakula vya vibandani lakini huyu alipata wateja wengi sana
kisa tu usafi katika upishi na ule ubora wa chakula chake lakini alikuwa akiuza 2000 kwa plate na alikuwa akiuza wakati wenzake wote 1500 kwa plate

well said mkuu, wandugu tubadilikeni!
 
Mkuu, nakuelewa sana lakini tatizo linabakia palepale, <b>MTAJI.<br /></b><br />Ukitaga kuwa mfugaji unahitaji MTAJI<br /><br />Ukitaka kuwa IMPORTER au EXPORTER wa aina yoyote ile, unahitaji <b>MTAJI</b>.<br /><br />Ukitaka kuanzisha duka la rejareja, supermarket, car wash centre, berber shop, unahitaji <b>MTAJI.<br /></b><br />Kbla ya hapo unahitaji <b>BUSINESS PLAN</b><br /><br />Ukiwa huna hata TIN numba unahitaji kujiandikisha na pia biashara isajiliwe kule BRELA.<br /><br />Hivyo mtu kam ayupo kazini anahitaji extra mile kufanya uamuzi wa kuwa na biashara ya pembeni kwanza kabla ya kuacha ajira rasmi.<br /><br />Hivyo inahitajika <b>MKAKATI</b> au <b>Strategy </b>kabla ya kuamua kuwa mjasirimali na pia akiba ya kutosha hata kama unaamua tu kwamba liwalo na liwe utoke kwenye ajira, yaani uwe na <b>AKIBA YA KUTOSHA BENKI.</b><br /><br />Hii akiba ya kutosha benki haihusiani na <b>MTAJI</b> wa biashara unaoutafuta.
 
Mkuu, nakuelewa sana lakini tatizo linabakia palepale, <b>MTAJI.<br /></b><br />Ukitaga kuwa mfugaji unahitaji MTAJI<br /><br />Ukitaka kuwa IMPORTER au EXPORTER wa aina yoyote ile, unahitaji <b>MTAJI</b>.<br /><br />Ukitaka kuanzisha duka la rejareja, supermarket, car wash centre, berber shop, unahitaji <b>MTAJI.<br /></b><br />Kbla ya hapo unahitaji <b>BUSINESS PLAN</b><br /><br />Ukiwa huna hata TIN numba unahitaji kujiandikisha na pia biashara isajiliwe kule BRELA.<br /><br />Hivyo mtu kam ayupo kazini anahitaji extra mile kufanya uamuzi wa kuwa na biashara ya pembeni kwanza kabla ya kuacha ajira rasmi.<br /><br />Hivyo inahitajika <b>MKAKATI</b> au <b>Strategy </b>kabla ya kuamua kuwa mjasirimali na pia akiba ya kutosha hata kama unaamua tu kwamba liwalo na liwe utoke kwenye ajira, yaani uwe na <b>AKIBA YA KUTOSHA BENKI.</b><br /><br />Hii akiba ya kutosha benki haihusiani na <b>MTAJI</b> wa biashara unaoutafuta.
Watanzania sijui uoga utatuisha lini?
 
  • Thanks
Reactions: SDG

Similar Discussions

Back
Top Bottom