nguvu ya bangi

mpigilie

JF-Expert Member
Sep 14, 2011
310
136
Kuna mzee mmoja alikua anawasumbua sana vijana waliokua wanavuta bangi karibu na nyumba yake na kutishia kuwaitia polisi. Basi wale wavuta bangi wakapanga mikakati ya kumkomoa yule mzee ili asiwasumbue tena.
Mmoja wao akatoa wazo la kuisukuma nyumba ya yule mzee ili isogee mbali na eneo wanalovutia bangi,wote waliunga mkono lile wazo.
Basi wote wakavua mashati na kuanza kazi ya kusukuma nyumba ya yule mzee. Wakati wanasukuma akatokea mtoto akayachukua yale mashati ya wavuta bangi na kuyasogeza mbali kidogo bila wavuta bangi kumuona.
Walipochoka kusukuma nyumba,kuangalia mashati yao wakaona yako mbali na ile nyumba,basi wakaanza kupongezana "LEO TUMEMKOMOA NA KESHO TUTAENDELEA KUISUKUMA MPAKA ITOKE MTAANI KWETU"


Bangi nibangue...
 
Back
Top Bottom