Nguvu iliyopo katika kichwa

Nguvu iliyopo katika kichwa

Kichwa kinapanga mabo mengi mazuri, unayaona maisha mazuri kwa kutumia kichwa, inapofika zamu ya mikono kutekeleza inakuwa mizito! mikono ndio chanzo cha umaskini wetu eeh?! maana kufikiri kichwa kinafikiri vizuri tu sasa uthubutu wa miguu na mikono unaweza kuwa tofauti na kichwa, kwa nini?!
 
Lawi 7:12
Kisha akamimina mafuta hayo ya kutia kichwani mwake Haruni; na kumtia mafuta amtakase.

#kichwa kimebeba vingi; ndan ya kichwa tunapata akili ufahamu kumbukumbu; mawazo; maono; mtu hafanyi kiti bila kuwaza kwanza na baadaye kuweka ktk matendo.

Unapowekewa mikono kichwan na kuombewa ina maana kichwa kinatakiwa kusikia hayo yote.
Ina maana kichwa kina kitu cha ziada ndani yake

Ndio maana taji huwa zinakaa kichwan

Hata taji ya Miiba ya Yesu ilikaa kichwa.
Taji inaonesha mamlaka

Kichwa kina mamlaka kubwa; taji ikikaa kichwan ina maana una mamlaka fulan ktk ulimwengu wa roho au duniani

Hata tukienda kanisan kuna kule kunenewa baraka mara nying huwa tunainamisha vichwa ili kupokea baraka.

Kumb 28:13
BWANA atakufanya kuwa kichwa; wala sio mkia; nawe utakua juu tu; wala huwi chini.

Mungu anaposema kichwa maana yake kiongoz; kuwa juu ya vyote; tunajua mtu akiwa na akil tunamuita kichwa.

Kwann kichwa?
Ina maana kichwa kina nguvu zake.
1samwel 16:13

Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta; akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho y BWANA ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile.

# Hayo mafuta alipakwa kichwan kwann isiwe mikonon ndio awe mfalme?

Zab23:5c
Umenipaka mafuta kichwani pangu

#Kichwa kina nguvu yake; kichwa ndio kinakupa muongozo unatawala vipi

Kichwa kikiwa kibovu ina maana hutoweza fanya chochote; sababu akil itakua haina uwezo wa kufikir.

Kwann tukiabudu tuna inamisha kichwa had chin wakati mwngine?

Ni ishara ya kumuheshimu Mungu kuwa akili zetu na vyote vilivyopo vipp chin yake.
Kwa Mungu ukichwa wetu unakua chini sababu yeye yupo juu ya vyote

Mwanzo 17:17a
Ndipo Ibrahimu akaanguka kifudifudi

Kutoka 34:8
Musa akafanya haraka; akainamisha kichwa chake hata nchi; akasujudu

#kichwa kina nafasi yake ktk mwil; kila kiungo tulicho nacho kina mamlaka ya namna moja ama nyingine

#tukiinamisha / kusujudu mbele ya Mungu; pale tunapoinamisha kichwa tunatii mamlaka ya Mungu; ishara ya kuwa sis hata kama ni kichwa tunaye kichwa zaidi yetu hivyo hatuna budi kumuinamia na kumsujudu na kumwambudu.

# tujifunze kujinenea baraka katika vichwa vyetu; tujifunze kuombea vichwa vyetu kwa kujiwekea mikono na kujiombea.

# kumbuka kuiombea mikono kabla hujaibandika ktk kichwa chako.

# Damu ya Yesu ni kila kitu kwa sisi tuaminio; hata kwa wasio amin pia ukitaka kuitumia unaitumia cz haina ubaguzi.

Kwa uchache ni hayo
 
Kichwa kinapanga mabo mengi mazuri, unayaona maisha mazuri kwa kutumia kichwa, inapofika zamu ya mikono kutekeleza inakuwa mizito! mikono ndio chanzo cha umaskini wetu eeh?! maana kufikiri kichwa kinafikiri vizuri tu sasa uthubutu wa miguu na mikono unaweza kuwa tofauti na kichwa, kwa nini?!
Mikono nayo ina nguvu na mamlaka yake.

Kila kitu ulichowekewa na Mungu kimeumbwa kwa kusud na kaz maalum
 
Divine... ameshaongea yote. Ila kuna kipande ngoja tu na me niongezee, who knows....

Kichwa kinabeba baraka, mamlaka, maono, ndoto, maamuzi, mawazo etc

Kichwa ndio kiungo kinachobeba dira ya mwili mzima, kichwa kikiharibika basi mfumo mzima wa mwili unaharibika pia. Kichwa kinaamuru viungo vingine vifanye sawasawa na taarifa iliyopo kichwani. Kichwa ndo muamuzi wa mwisho, kikiamuru miguu tembea itatembea, mikono nyanyuka itanyanyuka n.k. maamuzi yanayofanywa na kichwa ndo yanamtofautisha mtu mwenye akili timamu na asiye na akili timamu. Mtu asiye na akili timamu anapoteza ule uwezo wa kuamuru viungo vingine kufanya kazi na kujiongoza yeye mwenyewe. No wonder kichaa (sijui ni sahihi kumuita hivi) hatambui kama anachokifanya si sahihi, ataondoka na nyumbani pia coz kichwani kwake hakumbuki hata kama ana nyumbani kwake. Me niongelee mume kuwa kichwa cha familia

MUME NI KICHWA
Efeso 5:23
Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa, naye ni mwokozi wa mwili

Kwa sababu Mungu wetu ni Mungu wa utaratibu, basi hata kwenye familia aliweka utaratibu. Hivyo mume ndiye kichwa cha mkewe, kichwa cha familia. Mke ana kazi kuu ya usaidizi na ndo maana Mke tunamuita shingo. Na Mungu amefananisha uhusiano wa mke na mume, kama uhusiano wa Kristo na kanisa. Mume ana wajibu gani

1. MAMLAKA
Mume amtawale na kumuongoza mke na familia yake pasipo ubinafsi wala unyonyaji.

Mathayo 20:25- 28
Lakini Yesu akawaita, akasema, mwajua ya Kuwa wakuu wa mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha

26: Lakini haitokuwa hivyo kwenu, bali mtu yeyote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu.

Kwa sababu wewe ni kichwa, sio ndo busy kumuamrisha mkeo tu kila kitu. Kuna muda inabidi wewe mwenyewe utumike pia. (Mkeo ni msaidizi wako)

2. UPENDO
Mume anatakiwa ampende mkewe kama anavyojipenda yeye mwenyewe. Kuna mtu anayejipenda akajiwazia mabaya, akajiumiza au kujinenea mabaya??? Mke ni mwili wako, je Kuna anayeweza kuuchukia, kuuumiza au kuutesa mwili wake mwenyewe?
Efeso 5:25- 29

25:Enyi waume wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akalitoa kwa ajili yake

28: vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe, ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe

29: Maana hakuna anayeuchukia mwili wake popote, bali huulisha na kuutunza. .....
Mume ameagizwa kumpenda mkewe kama Kristo alivyolipenda kanisa lake

3. HESHIMA, HEKIMA NA UFAHAMU
1 Petro 3:7
Kadhalika ninyi waume kaeni na wake zenu kwa akili na kumpa mke heshima kama chombo kisicho na nguvu. .....

Mume awe na hekima na ufahamu wa kuiongoza familia yake. Obviously kutakuwa na ups and downs za kutosha but mume lazima asimame kwenye nafasi yake, akairudishe ndoa yake kwenye mstari. Ajiheshimu na kumuheahimu mke wakw pamoja na maoni yake. Kushindwa kufanya hivyo ni kuzuia maombi yake yeye mwenyewe.

4. KUITUNZA FAMILIA
Uanaume ni majukumu. Kama Huna kazi au biashara utaitunzaje familia yako

Mwanzo 3:19
Kwa jasho la uso wako utakula chakula

Mwanaume inabidi atoke jasho, kutafuta kipato. Mungu hataki mume legelege, uihudumie na kuitunza familia yako kwa jasho. Mwanaume usiwe mario eti

1 Timotheo 5:8
Lakini mtu yeyote asiyewatunza walio wake, yani wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana imani, tena ni mbaya kuliko asiyeamini


5. ASIYE MWEPESI WA HASIRA
Uanaume haupimwi kwa jinsi unavyozikimbia changamoto, ila kwa jinsi unavyokabiliana nazo pasi kuwa na hasira. Siyo umegombezwa na boss wako huko kazini, basi ukirudi hasira zote kwa mkeo. Ukipatwa na tatizo, kimbilia kwa Mungu then relax kupata ufumbuzi. Usifanye maamuzi ya hasira

Mithali 16:32
Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa. ...

6. MNYENYEKEVU
Tumeshazoea siku zote mke ndiye anayetakiwa kuwa mnyenyekevu kwa mumewe, Lakini mume pia inampasa awe mnyenyekevu. Asiwe mtu wa kujiona bora zaidi ya mkewe au kushindana naye kwa kila kitu. Awe anamshirikisha mkewe vyema

Wafilipi 2:3
Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu. Kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa ni bora kuliko nafsi yake
 
Divine... ameshaongea yote. Ila kuna kipande ngoja tu na me niongezee, who knows....

Kichwa kinabeba baraka, mamlaka, maono, ndoto, maamuzi, mawazo etc

Kichwa ndio kiungo kinachobeba dira ya mwili mzima, kichwa kikiharibika basi mfumo mzima wa mwili unaharibika pia. Kichwa kinaamuru viungo vingine vifanye sawasawa na taarifa iliyopo kichwani. Kichwa ndo muamuzi wa mwisho, kikiamuru miguu tembea itatembea, mikono nyanyuka itanyanyuka n.k. maamuzi yanayofanywa na kichwa ndo yanamtofautisha mtu mwenye akili timamu na asiye na akili timamu. Mtu asiye na akili timamu anapoteza ule uwezo wa kuamuru viungo vingine kufanya kazi na kujiongoza yeye mwenyewe. No wonder kichaa (sijui ni sahihi kumuita hivi) hatambui kama anachokifanya si sahihi, ataondoka na nyumbani pia coz kichwani kwake hakumbuki hata kama ana nyumbani kwake. Me niongelee mume kuwa kichwa cha familia

MUME NI KICHWA
Efeso 5:23
Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa, naye ni mwokozi wa mwili

Kwa sababu Mungu wetu ni Mungu wa utaratibu, basi hata kwenye familia aliweka utaratibu. Hivyo mume ndiye kichwa cha mkewe, kichwa cha familia. Mke ana kazi kuu ya usaidizi na ndo maana Mke tunamuita shingo. Na Mungu amefananisha uhusiano wa mke na mume, kama uhusiano wa Kristo na kanisa. Mume ana wajibu gani

1. MAMLAKA
Mume amtawale na kumuongoza mke na familia yake pasipo ubinafsi wala unyonyaji.

Mathayo 20:25- 28
Lakini Yesu akawaita, akasema, mwajua ya Kuwa wakuu wa mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha

26: Lakini haitokuwa hivyo kwenu, bali mtu yeyote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu.

Kwa sababu wewe ni kichwa, sio ndo busy kumuamrisha mkeo tu kila kitu. Kuna muda inabidi wewe mwenyewe utumike pia. (Mkeo ni msaidizi wako)

2. UPENDO
Mume anatakiwa ampende mkewe kama anavyojipenda yeye mwenyewe. Kuna mtu anayejipenda akajiwazia mabaya, akajiumiza au kujinenea mabaya??? Mke ni mwili wako, je Kuna anayeweza kuuchukia, kuuumiza au kuutesa mwili wake mwenyewe?
Efeso 5:25- 29

25:Enyi waume wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akalitoa kwa ajili yake

28: vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe, ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe

29: Maana hakuna anayeuchukia mwili wake popote, bali huulisha na kuutunza. .....
Mume ameagizwa kumpenda mkewe kama Kristo alivyolipenda kanisa lake

3. HESHIMA, HEKIMA NA UFAHAMU
1 Petro 3:7
Kadhalika ninyi waume kaeni na wake zenu kwa akili na kumpa mke heshima kama chombo kisicho na nguvu. .....

Mume awe na hekima na ufahamu wa kuiongoza familia yake. Obviously kutakuwa na ups and downs za kutosha but mume lazima asimame kwenye nafasi yake, akairudishe ndoa yake kwenye mstari. Ajiheshimu na kumuheahimu mke wakw pamoja na maoni yake. Kushindwa kufanya hivyo ni kuzuia maombi yake yeye mwenyewe.

4. KUITUNZA FAMILIA
Uanaume ni majukumu. Kama Huna kazi au biashara utaitunzaje familia yako

Mwanzo 3:19
Kwa jasho la uso wako utakula chakula

Mwanaume inabidi atoke jasho, kutafuta kipato. Mungu hataki mume legelege, uihudumie na kuitunza familia yako kwa jasho. Mwanaume usiwe mario eti

1 Timotheo 5:8
Lakini mtu yeyote asiyewatunza walio wake, yani wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana imani, tena ni mbaya kuliko asiyeamini


5. ASIYE MWEPESI WA HASIRA
Uanaume haupimwi kwa jinsi unavyozikimbia changamoto, ila kwa jinsi unavyokabiliana nazo pasi kuwa na hasira. Siyo umegombezwa na boss wako huko kazini, basi ukirudi hasira zote kwa mkeo. Ukipatwa na tatizo, kimbilia kwa Mungu then relax kupata ufumbuzi. Usifanye maamuzi ya hasira

Mithali 16:32
Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa. ...

6. MNYENYEKEVU
Tumeshazoea siku zote mke ndiye anayetakiwa kuwa mnyenyekevu kwa mumewe, Lakini mume pia inampasa awe mnyenyekevu. Asiwe mtu wa kujiona bora zaidi ya mkewe au kushindana naye kwa kila kitu. Awe anamshirikisha mkewe vyema

Wafilipi 2:3
Msitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu. Kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa ni bora kuliko nafsi yake
Amen dear sis
 
Katika milango nane ya fahamu saba iko kichwani na hata huo wa nane pia waweza upata kichwani
Nyoka alipewa laana ya kupondwa kichwa lakini pia chochote chenye uhai ili kithibitike pasipo na shaka kuwa kimekufa basi ni kutenganisha kichwa na kiwiliwili
 
Natamani wanadamu wangekuwa wanavitumia vichwa vyao ipasavyo.....nadhani kungekuwa na unafuu mkubwa kwenye hali za maisha yetu.......na tungekuwa na jamii yenye furaha na amani.....
Lakini bahati mbaya waanadamu wa nyakati hizi tumeacha kuvitumia vyema vichwa vyetu na badala yake vimekuwa ni ma gofu ya mashetani na kila mapepo wachafu........na yote hayo yanaonekana kupitia matendo yetu machafu......

Mwanadamu mwenye kutumia kichwa chake inavyotakiwa anawezaje kumkata mwanadamu mwenzie kiungo cha mwili ili yeye awe tajiri kwa kuwa tu huyo kiumbe ana rangi ya mwili tofauti na yeye.....!!??

Mwanadamu mwenye kuutumia vyema kichwa chake anawezaje kumvua chupi na kumuingilia mwanaye wa kumzaa....kwa tamaa za mwili au kupata utajiri...???

Mwanadamu mwenye kukitumia kichwa chake vyema anawezaje kumtoa mama yake kipenzi kafara ili yeye tu apate utajiri....!!???

Mwanadamu mwenye kutumia vyema kichwa chako unawezaje kuthubutu achilia mbali kuwaza kumuingilia mwanamume mwenzio na hata mke wako mpendwa kinyume na maumbile.....kama sio usheitwani nini.....!!!!???

Yapo matendo mengi ya kushangaza na mengine ya kuogofya ambayo yanafanywa na wanadamu waliopoteza udhibiti wa vichwa vyao....na mengine na mabaya kiasi kwamba hayafai hata kuandikika humu maana ni kinyaa....
Ndio maana tunapaswa kufikiri kabla ya kutenda...kwani kupitia fikra zetu ndio tunapata kujua upumbavu wetu na kujisahihisha........na kubaki kwenye mstari.......
Wanadamu tunahesabika wastaarabu na wenye hekima kutokana na matumizi mazuri ya hazina zilizomo kwenye vichwa vyetu.....
Na kupitia kilichomo humo kwenye vichwa vyetu ndio tukapewa utukufu wa kutawala ulimwengu na vyote vilivyomo...........

Lakini kutokana na kuacha kuvitumia vichwa vyetu sawa sawa tumejikuta tukitawaliwa na wanyama kwa kufanya yale yalikuwa yakifanywa na wanyama na mengine hata hata hayafanywi na wanyama.....kama vile kumuingilia mwanamume mwenzake au kumuingilia mwanamke kinyume cha maumbile.......

Wanadamu hatutajua utukufu wetu mpaka pale tutakapo rudi katika mstari....na ili turudi katika mstari ni lazima tuvitumie vyema vichwa vyetu......na kujikomboa kutoka kwenye utumwa wa fikra za kishetani............

It begins with you...,...
Wameacha kutumia akili zao kutokana na fikra zilizopofushwa, zilizoharibika,zilizofunikwa na zilizotiwa uzito..hiyo yote ni kukosa maarifa ya Mungu
Warumi 1:28 na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafate akili zao zisizofaa.
 
Katika milango nane ya fahamu saba iko kichwani na hata huo wa nane pia waweza upata kichwani
Nyoka alipewa laana ya kupondwa kichwa lakini pia chochote chenye uhai ili kithibitike pasipo na shaka kuwa kimekufa basi ni kutenganisha kichwa na kiwiliwili
Naomba unitajie iyo milango 8 ya fahamu.
 
Uko sahihi kabisa ndio maana nikaomba msaada wa wadau wawili mahiri kwenye neno la Mungu....na baadae nitajitahidi kuliweka vema na nikichemsha bado nitakiri kuchemsha
mshana jr Wewe ni mahiri kwenye eneo gani sababu huwa unanimix,ukianzia will.power.jicho la tatu.meditation.etc au wewe upo kwotekwote???
 
Uko sahihi kabisa ndio maana nikaomba msaada wa wadau wawili mahiri kwenye neno la Mungu....na baadae nitajitahidi kuliweka vema na nikichemsha bado nitakiri kuchemsha
Hata upande wa picha,kawaida huwa unatoa msururu wa picha,japo zingine zinatisha,leo umetoa kidunchuuu,kulikoni jr?
 
Wameacha kutumia akili zao kutokana na fikra zilizopofushwa, zilizoharibika,zilizofunikwa na zilizotiwa uzito..hiyo yote ni kukosa maarifa ya Mungu
Warumi 1:28 na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafate akili zao zisizofaa.
Aaamen
 
Back
Top Bottom