Ngorongoro inaangamia, tuache Siasa kwenye ukweli

Utalii wa utamaduni kwa namna unavofanyika sasa NCA ni greenwashing ya nguvu.
Watu wanaigiza maisha ya Maasai pale "Kanjiro" (staged cultural experience).
Kingine utitiri wa lodge na camps unaathiri biashara ya utalii!
Hizo cultural na campsites za utalii zifungwe.
 
Wanabodi JF!,

Nawasalimia popote pale mlipo!
Naomba niende kwenye Mada hii kuhusu NGORONGORO CONSERVATION AREA AUTHORITY.(NCAA).

Nimefuatilia mijadala mbalimbali ambayo imekuwa ikiendelea kwenye social platforms,takriban muda wa wiki moja na ushei sasa.

Kuna wachangiaji ambao wamegawanyika katika pande mbili tofauti.

Upande mmoja ni wale wanaoitetea jamii ya wamaasai kuendelea kuishi wao pamoja na shughuli zao za ufugaji.

Pamoja na kuendelea kuongezeka ndani ya eneo la hifadhi hiyo kama ilivyo kwa sasa.

Kundi la pili ni wale ambao wanatetea uhifadhi maliasili ya wanyama pori na Ikolojia viumbe hai,vilivyo ndani ya eneo hilo muhimu na maarufu Duniani kwa utalii.

Mimi ninasimama upande wa watetezi wa Mazingira na Maliasili za wanyama pori na uoto wa asili,katika hifadhi ya Ngorongoro.

Ni ukweli usiopingika kwamba eneo hilo limekuwa likikaliwa na jamii ya kabila la kifugaji la wamaasai kwa asili.

Lakini inapokuja suala la uchumi wa kitaifa na pato la taifa kama nchi.
Eneo hilo na mengineyo mengi nchini yanayohusiana na utalii,yanabakia kuwa muhimu kwa upatikanaji wa fedha za kigeni.
Ambazo huingia na kuchangia maendeleo ya nchi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu na afya ya jamii.

Na hivyo kulifanya eneo hilo kutazamwa kwa maslahi mapana ya kitaifa na kimataifa.

Ikizihusu pia taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa zinazojihusisha na utunzaji mazingira na viumbe hai Duniani.
Ikiwemo UNESCO.

Kuna kundi la watu wamechangia kwa kumshambulia Moja kwamoja #Maulidkitenge.
Kwa ile tu kunyoosha ukweli wake na kutoa maoni yake baada kile alichokishuhudia kule Ngorongoro.

Pia kuna waliochangia kwa kuwa wanatokana na jamii husika zinazokabiliwa na kadhia ya moja kwa moja ya kutakiwa kuhamishwa toka Ngorongoro hifadhini.


Lakini pia kuna wachangiaji ambao wameligeuza suala hili kuwa kama mtaji wao wa kisiasa zaidi.

Na hii niseme kuwa ni kwa maslahi binafsi ya wanasiasa hao.

Na hapa kuna wanasiasa wa pande zote mbili za kisiasa Toka upinzani na chama tawala CCM.

Mimi nachangia kama mtanzania ambaye nimefanyia kazi katika eneo hilo,kwa ukaribu na kwa muda mrefu sasa.

Nimeziona athari zinazoikumba hifadhi ya Ngorongoro katika kila hatua.

Kuongezeka kwa idadi ya wakazi na muingiliano wa shughuli za kiutalii.Ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.

Kwa ujumla ni tatizo ambalo linahitaji ufumbuzi au utatuzi wa mapema.kabla halijageuka na kuzaa mgogoro mkubwa baadae.
Endapo tu,halitachukuliwa maamuzi sahihi na kwa wakati stahiki.

Ebu tujiulize kwa kina!

Kama idadi ya wafugaji wa kimasaai ndani ya hifadhi ya Ngorongoro inaongezeka kwa kasi.
Kama ilivyo kwa watanzania wote.

Je inakuwaje kuhusu upatikanaji wa huduma muhimu za kijamii kama,Elimu, Zahanati na maji kwa matumizi ya binadamu na mifugo yao?

Katika eneo zima la Ngorongoro. Je kama wakipewa huduma zote na miji yao kutambulika kisheria...kutakuwa na kitu kinaitwa hifadhi ya Ngorongoro?

Ukizingatia kuwa jiografia ya eneo kubwa la Ngorongoro ni lenye kiwango cha chini cha mvua katika msimu wa mwaka mzima na hivyo suala la upatikanaji wa maji inakuwa moja ya changamoto kubwa kuwaathiri wakazi hao pamoja na mifugo yao.

Jambo linaloilazimu mamlaka ya hifadhi kuwasaidia ili kuwanusuru na maafa hayo.

Je, serikali inalo fungu la kuendelea kuwahudumia kwa muda woote,pamoja na idadi yao kuzidi kuongezeka kila uchao?


Je, watetezi wa wafugaji hao wanaelewa kwamba.

Kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na kupelekea kubadilika kwa mifumo ya maisha katika jamii nyingi.

Na jamii ya wamaasai wakiwa mojawapo ya wahanga wa mabadiliko hayo.
Kutokana na baadhi yao kupoteza kiasi kikubwa cha mifugo yao kutokana na maradhi au tabia nchi.

Imewalazimu pia kuanza kula vyakula ambavyo hapo awali havikukubalika kama chakula rasmi na ilikuwa ni marufuku kwao kuvila.
Ikiwemo Nyama Pori,Samaki na kuku.

Baada ya maisha kuwabadilikia na vijana wengi wa kimaasai kuingia mijini na kuchanganyika na jamii zingine katika jitihada za kutafutia maisha.

Leo hii wamekuwa walaji wakubwa wa vyakula vingi ambavyo hapo awali haikuwa kwenye orodha yao ikiwemo Chips Mayai nk.

Na ni katika mtindo huo,tabia hizi zinaambukizwa taratibu hadi huko kwenye asili zao.
Ngorongoro ikiwa muhanga mojawapo ya eneo husika.

Mifugo Tegemezi .

Tofauti na mifugo kama Ng'ombe,Punda,Mbuzi na kondoo inayofugwa na wamaasai hao wa Ngorongoro (na idadi yao pia ikiongezeka kwakasi).ambayo kiasili wanakula majani sambamba na wanyama wengine wa porini.

Kuna wanyama kama Mbwa ambao wafugaji wanawafuga na kuwategemea kama nyenzo muhimu kwa ulinzi wa mifugo yao,nyakati za usiku dhidi ya wanyama pori walao nyama kama Simba,Chui na Fisi.

Je! wao hao mbwa ambao kila kaya,lazima inawamiliki kwa idadi ya wastani usiopungua mbwa watano kila kaya.

Je, Wanakula nini kila siku ilhali chakula cha maasai wa asili ni mchanganyiko wa maziwa na mahindi almaarufu kama Roshoroo.?
Ambacho si chakula kinacholiwa na hao mbwa wa asili ya wamaasai.

Ikumbukwe kuwa nyama ya mbuzi ambayo huchinjwa na maasai hao mara chache katika maboma yao,huwa ni kidogo kuliko mahitaji rasmi ya kutosheleza jamii husika wakiwemo watoto wadogo.

Jambo ambalo hupelekea mgawanyo usio sawia kati ya wanaume
(Morani na wazee) na upande wa wanawake (kina mama,vikongwe na watoto wadogo).

Hapo humlazimu mbwa kujitafutia riziki zao na watoto wao.
Kwa mbinu asilia za kuwinda wanyama pori kama vile Sungura,Swala, watoto wa nyumbu na punda.

Na saa ingine hadi watoto wachanga wa Twiga.
Tukio ambalo mimi binafsi, niliwahi kulishuhudia na kulitolea taarifa pale Seneto gate kwa maaskari wa Ngorongoro.

Je, Hatujiulizi kwamba kuna idadi ngapi? au kiasi gani cha wanyamapori kinapotea kila mwaka kwa kuliwa na idadi kubwa ya mbwa wanaomilikiwa na wamaasai.?

Wakati tukiwatetea wamasai wa Ngorongoro,pia vema tuelewe kwamba,wao wanaishi pale ndiyo.
Lakini Ngorongoro inabeba maisha ya watanzania wengi kutokana na pato linaloingizwa kupitia sekta pekee ya utalii.

Na hivyo tunapotetea haki ya wamaasai wakaazi wa Ngorongoro kutohamishwa.

Pia ni vema tukumbuke na madhara yanayoweza kupatikana endapo jamii hiyo itaachwa kuzagaa na kuongezeka bila udhibiti sahihi kwa manufaa ya wengi nchini.

Na kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.

Hapo sijaongelea kero zinazowasibu wakazi hao kwa uduni wa maisha kutokana na kutoruhusiwa kulima mazao ya chakula kisheria.

Na hivyo kupelekea baadhi ya familia zinazoishi pembezoni mwa shughuli za kitalii,kugeuka omba omba mabarabarani jambo linaloiwekea Tanzania taswira mbaya kimataifa.

Pindi watalii hao wanaporudi makwao na kusimulia walichokiona ikiwemo pamoja na picha za video na mgando.

Tuacheni siasa na malumbano yasiyo na tija.

Watanzania tubadilike linapokuja suala la ukweli na tuache tabia ya kutanguliza maslahi binafsi mbele.

Maendeleo hayana chama.
Ngorongoro siyo hifadhi
 
Usipotoshe umma,hapa hatuongelei suala la Loliondo!

Hapa tunaiongelea tarafa ya Ngorongoro pekee.

Wewe nadhani huielewi jiografia ya eneo husika zaidi ya kuchangia bila uelewa.

Pia hakuna mmasai alietishiwa kuangamizwa,zaidi ya kutakiwa kuhamishiwa na kupewa fidia katika maeneo mbalimbali ya nchi hii.

Je huko wanakopelekwa unataka kuniambia wananchi wa huko wanaangamia?

Je unazo taarifa kwamba zoezi la kuwahamisha lilikwisha anza kutekelezwa,na hivi tunavyoongea na kuandika.
Wale waliokwishahama leo hii wanaendelea na maisha yao kwa uhuru na hawatamani tena Ngorongoro.!
Kwanini tusiwahamishe wapemba kwenda Madascar ili kuokoa visiwa vile ambavyo ni vivutio vikubwa vya watalii ?
 
Hizo cultural na campsites za utalii zifungwe.
Halafu wewe utachangia pato mbadala toka entry fees & Concessions zinazolipwa na hizo Camps!

Au unadhani ni camp za sanaa huko Bagamoyo?
 
Ngorongoro siyo hifadhi
Ni hifadhi mseto kati ya Binadamu,Mifugo yake na Wanyamapori na Ikolojia ya Mimea na Uoto wa Asili.

Jikite kwenye hoja zaidi,acha vioja vya kizwazwa.@PTER au PETER

Hoja hapa ni nini kifanyike kuinusuru Ngorongoro.

Suala hapa ni uteketevu wa Ngorongoro kutokana na shughuli za kibinadamu.

View attachment IMG_2778.JPG
 

Attachments

  • IMG_2412.JPG
    7.3 MB · Views: 7
Mimi sihitaji kusoma tafiti ya mtu wakati binafsi nina miaka zaidi ya thelathini nikiwa katika eneo husika.

Hao watafiti huja kuandika kwa kuhoji watu kwa kipindi fulani na kuondoka lakini mimi ninielewa eneo hilo kuanzia Loduare mpaka Wasso kule Loliondo.

Ninaijua milima yote na nimeipanda kwa miguu yangu ukiwemo huo wa Le Magurut

Nimezitembelea crater zote kuanzia Ngorongoro, Olmoti na Empakai.

Nimepanda mpaka kileleni mwa mlima pekee wenye volcano hai...Oldoinyo Lengai.

Nimetembelea na kufanya kazi katika ziwa pekee lenye mazalia ya flamingo Lake Natron.

Nimewatembelea mpaka machifu maarufu wa Ngorongoro akiwemo marehemu Birkaa na Ole Mereiya.

Utafiti gani zaidi nauhitaji #Lukubuzo ramsis!

Labda watafiti ndio wanitafute ili niwatafiti.
Sema ulizurula bila kazi huko! na posho mawazo! lkn siyo eti umetembelea!!! bila lengo?? hao wamasai wafunzwe kuishi na wanyama kwa amani tu!! wakitunza mazingira baaasi!!

Kama hujui kule australia!! watu wanaishi na Kangaroo mitaani na mazingira yana hifadhiwa vizuri mnoo!! Bongo tukijaa pomoni!!! wanyama wataenda wapi?? hawawezi kufa wote!! eti sababu tumejaa!!

itabidi tuishi nao tu kwa amni!! Masai ni sehemu ya hifadhi! India wanaishi na tembo majumbani mwao na wanakuja kufanya kazi za kulipwa!! nenda Austaralia Wanaishi na kanga roo mitaani kwa nini tusijifunze kutoka kwa hao???

Kwani weusi hifadhi mliizijua? si mmefundishwa tu na wakoloni?? jinsi ya kulinda hifadhi??? sasa mnajifanya kujua zaidi ya wakoloni waliowafundisha??? acheni ujuaji wa kizamani waacheni wakae ila wafundishwe jinsi ya kutunza mazingira!!

Mtwara mikindani watu wanaishi na swala, chui, nyati nk na hakuna madhara! kwanini isiwe kwa wamasai, igeni mazuri kwa Mkoloni mabaya yaacheni jamani hee!!!

humo humo ndani ya wanyama wanaweza kuendeleza kilimo kizuri cha hifadhi mazingira na wanyama wamo wakipita hivi! na mvua za kutosha, na sisi tumezungukwa na maji ya kutosha!! twaweza kuwapelekea maji kutoka ziwa victoria! na wakaishi
 
acha iangamie watu wanakula pesa yetu kifisadi wanaachwa hao wamasai kulisha tumifugo imekua nongwa hivi mnataka Tabaka la chini wafe njaa huku wanasiasa ni mchuzi tuu binafsi naona sawa tu wamasai wainjoy
 
Sema ulizurula bila kazi huko! na posho mawazo! lkn siyo eti umetembelea!!! bila lengo?? hao wamasai wafunzwe kuishi na wanyama kwa amani tu!! wakitunza mazingira baaasi!!

Kama hujui kule australia!! watu wanaishi na Kangaroo mitaani na mazingira yana hifadhiwa vizuri mnoo!! Bongo tukijaa pomoni!!! wanyama wataenda wapi?? hawawezi kufa wote!! eti sababu tumejaa!!

itabidi tuishi nao tu kwa amni!! Masai ni sehemu ya hifadhi! India wanaishi na tembo majumbani mwao na wanakuja kufanya kazi za kulipwa!! nenda Austaralia Wanaishi na kanga roo mitaani kwa nini tusijifunze kutoka kwa hao???

Kwani weusi hifadhi mliizijua? si mmefundishwa tu na wakoloni?? jinsi ya kulinda hifadhi??? sasa mnajifanya kujua zaidi ya wakoloni waliowafundisha??? acheni ujuaji wa kizamani waacheni wakae ila wafundishwe jinsi ya kutunza mazingira!!

Mtwara mikindani watu wanaishi na swala, chui, nyati nk na hakuna madhara! kwanini isiwe kwa wamasai, igeni mazuri kwa Mkoloni mabaya yaacheni jamani hee!!!

humo humo ndani ya wanyama wanaweza kuendeleza kilimo kizuri cha hifadhi mazingira na wanyama wamo wakipita hivi! na mvua za kutosha, na sisi tumezungukwa na maji ya kutosha!! twaweza kuwapelekea maji kutoka ziwa victoria! na wakaishi
Kuna ile wanyama kuwafuata watu maeneo yao na wakajifunza kuishi na binadamu kwa utulivu na amani (hiyo ndo mifano ya huko Australia na India).
Ukija Tanzania, NCA mle binadamu ndo wanawafuata wanyamapori kwa wingi ambao ni hatari sana.
Kuhusu kilimo maeneo ya hifadhi sijui unaongea kwa kumaanisha au unatania. Ulizia ongezeko la human-wildlife conflicts na crop damages maeneo yaliyo jirani na hifadhi kama Karatu, Naitolia, Makuyuni, Mugumu, n.k. Hasara ni kubwa kuliko.
 
Naunga mkono hoja, Masai wahame wasisubiri itumike nguvu watapata hasara wao maana hizi operesheni zitafanyika kijeshi na usiku

Wataumia heri wahame kwa amani kuelekea ambako wameelekezwa itakuwa busara na watapata muda mzuri wa kusettle maana pamoja na kuhama wanapewa na fidia.

Muda huu wangeutumia vizuri kujadili wanakohamia na kiasi Cha fidia instead of kulazimisha kubaki hapo wakati serikali imeshaamua, hawawezi kubaki kirahisi inaweza kucheleweshwa kuhama Ila watahama tu Sasa kwa nini usihame mapema ?

Nawashauri huu muda wapiganie kupata eneo zuri wasiingiliwe na wengine, wapewe eneo ambalo watahamia wao na watatambulika kwa kuwa wao pekee ndio watakaa hapo na kuform jamii yao Kama walivyoishi mbugani.

Ila wakiendelea kukaidi basi hakuna shida maana watajikuta hata hawapati Mia na watahamishwa kwa nguvu na kuumizwa na kuhamia kusiko na huduma wakati Wana muda mzuri wa kujadili haya yote kabla.

Kiburi si maungwana na mwanye nguvu mpishe.
Wawape Kimamba Morogoro itawafaa sana maana waarabu na wahindi wamepakimbia.
 
Serikali itenge eneo la kuwahamisha hao watu.

Baada ya kutenga hilo eneo wamasai watangaziwe muda wa kuondoka hapo Ngorongoro.

Baada ya deadline serikali itumie nguvu kuwaondoa kwa kuwapiga tanganyika jeki

Then ziingie greda zivunje vunje makazi na miuondo mbinu yote iliyobaki, uoto wa asili uchukue nafasi yake
Haya yote yameshafanyika naona tunaenda mbele na kurudi nyuma tu, toka enzi ya magu 2016 wanajua kwamba hapo hawapaswi kukaa.

Wameshaambiwa wahame na wameshatengewa eneo wilayani pangani na barabara imechongwa na hadi vituo vya misitu askari wamewekwa ili kuzuia malighafi zisipite kuelekea wilaya nyingine maana pale wanaungana na wilaya nyingine ikikamilika kuchonga barabara.

Hao wanaopinga ni matajiri waliowekeza ng'ombe, watu hawaelewi namna Masai wanavyofuga. Mtu anaweka ng'ombe hata elfu Saba kwa mwenzie wanakubaliana tu wanaochunga wanakuwa wanahama mapori kufuata malisho na wanajua wapo wapi.

So unakaa na Masai mjini kumbe mwenzio hana zizi Ila ana ng'ombe sasa wakiambiwa wahame wanaopiga kelele ni Hawa wa mjini wanaosikiliza bei akitaka kuchinja anasubiri bei iwe juu
 
Haya yote yameshafanyika naona tunaenda mbele na kurudi nyuma tu, toka enzi ya magu 2016 wanajua kwamba hapo hawapaswi kukaa.

Wameshaambiwa wahame na wameshatengewa eneo wilayani pangani na barabara imechongwa na hadi vituo vya misitu askari wamewekwa ili kuzuia malighafi zisipite kuelekea wilaya nyingine maana pale wanaungana na wilaya nyingine ikikamilika kuchonga barabara.

Hao wanaopinga ni matajiri waliowekeza ng'ombe, watu hawaelewi namna Masai wanavyofuga. Mtu anaweka ng'ombe hata elfu Saba kwa mwenzie wanakubaliana tu wanaochunga wanakuwa wanahama mapori kufuata malisho na wanajua wapo wapi.

So unakaa na Masai mjini kumbe mwenzio hana zizi Ila ana ng'ombe sasa wakiambiwa wahame wanaopiga kelele ni Hawa wa mjini wanaosikiliza bei akitaka kuchinja anasubiri bei iwe juu
#Bondposr
Umesema ule ukweli ambao niliulizwa kisha nikashindwa kulijibu.
 
Haya yote yameshafanyika naona tunaenda mbele na kurudi nyuma tu, toka enzi ya magu 2016 wanajua kwamba hapo hawapaswi kukaa.

Wameshaambiwa wahame na wameshatengewa eneo wilayani pangani na barabara imechongwa na hadi vituo vya misitu askari wamewekwa ili kuzuia malighafi zisipite kuelekea wilaya nyingine maana pale wanaungana na wilaya nyingine ikikamilika kuchonga barabara.

Hao wanaopinga ni matajiri waliowekeza ng'ombe, watu hawaelewi namna Masai wanavyofuga. Mtu anaweka ng'ombe hata elfu Saba kwa mwenzie wanakubaliana tu wanaochunga wanakuwa wanahama mapori kufuata malisho na wanajua wapo wapi.

So unakaa na Masai mjini kumbe mwenzio hana zizi Ila ana ng'ombe sasa wakiambiwa wahame wanaopiga kelele ni Hawa wa mjini wanaosikiliza bei akitaka kuchinja anasubiri bei iwe juu
Leteni sheria ya kuanzishwa kwa Ngorongoro kama national park. Achemi kelele na maneno matupu.
 
Leteni sheria ya kuanzishwa kwa Ngorongoro kama national park. Achemi kelele na maneno matupu.
Hujui Kuna marekebisho yanaendelea bungeni? Yaani nyie wakati mnaendelea kurukaruka na lubega wenzenu wadeal kisheria siku ya siku mtakosa vyenu. Ndio maana tunawapa ushauri Kama watanzania wenzetu.

Haujiulizi hizi kelele zimeanzia wapi? Why kelele imeanzia bungeni? Shauri yenu hamjasikia msimamo wa serikali kupitia Waziri Mkuu? Haya.

Tunawashauri mnaleta kuvimba fuvu shauri yenu bana. Masai ni masai tu.
 
Mkuu
Unahitaji kueleweshwa kidogo kuhusiana na hili.

Hapa haiongelewi Ngorongoro ya Loliondo,huko ndio kuna mwarabu.

Bali inaongelewa tarafa ya Ngorongoro ambalo ni eneo linaloihusu Crater ya Ngorongoro na vijiji kadhaa vya kuizunguka hiyo crater.
Kwangu mimi iitishwe sensa wale wamasai waliokuwa ngorongoro kuanzia 1960 hadi 1970 wabaki ili kulinda sifa ya ngorongoro ya wanyama kuishi na binadamu wengine wote waondoke. Idadi ibaki ya 8000 tu.
 
Hujui Kuna marekebisho yanaendelea bungeni? Yaani nyie wakati mnaendelea kurukaruka na lubega wenzenu wadeal kisheria siku ya siku mtakosa vyenu. Ndio maana tunawapa ushauri Kama watanzania wenzetu.

Haujiulizi hizi kelele zimeanzia wapi? Why kelele imeanzia bungeni? Shauri yenu hamjasikia msimamo wa serikali kupitia Waziri Mkuu? Haya.

Tunawashauri mnaleta kuvimba fuvu shauri yenu bana. Masai ni masai tu.
Mswada gani? Unajua kweli hatua za kutungwa kwa sheria? Acha mihemko ya kukosa posho za NCAA.
 
Hata mimi pia nimesoma mistari michache tu nimemuelewa. Kusema kweli suala la Ngorongoro wala halihitaji uwe na madigirii kuona kwamba hifadhi inaharibika.
Kikubwa majibu yamepatikana tayari, maasai wanaondoka ngorongoro, keep my reply.
 
Kikubwa majibu yamepatikana tayari, maasai wanaondoka ngorongoro, keep my reply.
Badilini kuwa national park. Sidhani kama kuna mahali wamasai wameng'ang'ana kukaa kwenye national park. Ngorongoro ilikuwa hivyo toka kuanzishwa kwake. Kwa hiyo wakati wa kufanya mabadiliko, historia uzingatiwe na serikali isijipendelee kupitia NCAA. Basically wadau wote wameshiriki kutifikisha kwenye hili sakata. Na sisi hatuondoki kirahisi hivyo.
 
Kama wakipatiwa huduma zote za kijamii basi ujue Neno la hifadhi litakufa kabisaa... wakati mnajua toplist ya nchi zinaongiza kwa utalii duniani, tanzania nayo imekuwa ya kwanza kwahyo kwa mimi nachoomba wamasai waendelee kujirecord na tik tok watoboe maisha waache kuwinda wanyama na kugoma kutoka kwenye hifadhi
Wamasai kwa asili na tabia huwa hawawindi na kula wanyama wa porini mkuu.. ingekua hivyo basi pengine leo hii hizo mbuga, zisingekuwa na wanyama
 
Back
Top Bottom