Ngeleja: Zitto ni Mbunge halali wa CHADEMA

Ngeleja: Zitto ni Mbunge halali wa CHADEMA

amakyasya

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2013
Posts
3,480
Reaction score
918
Amekanusha baadhi ya watu wanaodai kuwa ni mbunge wa mahakama.
Source : Mwananchi leo
My take : Je, Ngeleja amekuwa msemaji wa CHADEMA siku hizi?
=============================================


William%20Ngereja-July14-2014.jpg

Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (pichani), amesema Zitto Kabwe, bado ni mbunge halali wa Jimbo la Kigoma Kaskazini licha ya kubatizwa jina kuwa ni mbunge wa mahakama.

Alisema hayo alipokuwa akijibu hoja za baadhi ya wananchi jimboni kwake waliotaka kufahamu iwapo Zitto bado ni mbunge kutokana na baadhi ya wafuasi wa Chadema kudai kutomtambua.

"Mimi siyo msemaji wa Chadema, lakini nazungumza kama mbunge wenu ili kuwaondolea mkanganyiko mlio nao ni kuwa Kabwe (Zitto) bado mbunge na ataendelea kuwa mbunge hadi mahakama itakapokuwa imetoa maelekezo mengine," alisema Ngeleja na kushangiliwa na umati wa watu waliofurika katika mkutano huo.

Mkutano huo ulifanyika katika Kijiji cha Nyantakubwa, Kata ya Kasungamile, ikiwa ni sehemu ya ziara ya siku 10 ya kutembelea jimbo lake kwa lengo la kusikiliza kero na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Ngeleja, ambaye kitaaluma ni mwanasheria, aliwatahadharisha wapigakura wake kuwa makini na uzushi wa kila kinachozungumzwa kuepuka kupotoshwa na inapobidi kuuliza ili kupata jibu sahihi kama walivyofanya, kwa vile hiyo ni sehemu ya wajibu wake.

Wakati wa ziara yake juzi akiwapo katika Kitongoji cha Igalagalilo, Kijiji cha Chamabanda, Kata ya Katunguru, ambako alipokewa kwa maandamano makubwa. Wakati wa mkutano, baadhi ya wajumbe walithubutu kuimba "Rais mtarajiwa" bila kutafuna maneno wakimuita "jembe lao".

Tayari amefanya ziara katika Kata za Nyamatongo, Busisi, Nyamazugo, Nyampulukano, Chifunfu na Kasenyi, ambako alifanya mikutano ya hadhara, huku baadhi wakidai kukerwa na baadhi ya wanachama kuanza kupitapita wakifanya kampeni za ubunge kabla ya muda.

SOURCE: NIPASHE
 
Ndio wa Mahakama....hilo halina ubishi kwani hata mgambo wa City wanalijua
Wewe mbululu, tangu lini mahakama zikachagua wabunge? Yaani chadema imekuwa zaidi ya wananchi au zitto alipigiwa kura na chama chenu?
 
William Ngeleja Mbunge wa sengerema amesema kuwa Zitto Kabwe ni Mbunge halali wa CHADEMA licha ya kuwa kuna waliombatiza kuwa ni mbunge wa mahakama.
Source : Nipashe gazeti la leo.
My take : Ngeleja amejunga lini na CHADEMA hadi kuwa msemaji wa chama?
 
Zitto si ni mtu wao ccm,lakini ajue kuwa alinusurika 2010 kukwaa ubunge kwao.bila ktumia mbinu za kisayansi alienda kahama na geita akakutana na wazee wa chadema na kuwaambia kuwa kule jimboni kwangu upepo sio mzuri ikabidi awatume kigoma waende jimboni kwake eti waombe wazee Wa kule eti wanamwomba kijana wao ajee agombee sehemu kti ya hizo mbili. Ndio wale wazee kushtuka na kusema tunataka kumtosa kumbe ni lulu na hata hivyo alipita kwenye tundu la sindano sasa kipindi ichi hapati baada ya kumjua ni kibaraka Wa ccm ndiyo by by.
 
Sawa,ni mbunge wa CHADEMA ila sio mwanachama wa CHADEMA.
Alipata ubunge akiwa mwanachama ila kwa sasa sio mwanachama maana hatimizi majukumu ya uanachama
 
Zitto ni Mfadhili Mkuu wa ACT na Mwkt mtarajiwa wa Taifa, kwa sasa anachokifanya ni kung`ang`ania uanachama wa Chadema japo si mwanachadema na hajawahi kuwa na dhamira ya kweli kuipenda Chadema bali maslahi ndo yalikuwa mbele zaidi, Ili tu aendelee kupata maslahi ya kukijenga ACT.

Nawasilisha
 
Mleta mada sijui anaharaka gani, unaleta vitu nusu nusu hapa jamvini unadhani wote tunapitia hayo magazeti, km ulikuwa unakimbizwa ungeweka link pekee ukaacha tutiririke. Samahani hivi hilo gazeti la mwananchi ndio lile lililoandika habari ya Mhe. Ballali
 
wabunge wa mahakama hawa hapa
1. zitto
2. kafulila
3. hamad
 
Mambo ya chadema yanamhusu nini Ngeleja? Ngeleje azungumzie mambo ya chama chake. Yeye ni miongoni mwa watu waliojitangaza kugombea Urais, pamoja na mawakala kama yeye ndani ya chama chake. Mmmmmmmmh, watu hata Urais wa nyumba zao hawajaweza, watawezaje kuongoza nchi?_
 
Na Meya Bw Matata, alimtimua naibu meya last week baada ya kuzidiana kete za ulaji. Huo msala sijui ccm Mwanza wameumalizaje.
 
Watu wa madili wote hao wala sishangai hata nukuta!
 
Back
Top Bottom