Ngeleja kujiuzulu ni lazima

Ngeleja kujiuzulu ni lazima

Mizizi

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2008
Posts
1,275
Reaction score
391
Ngeleja,
Hakuna cha kusubiri, uongozi ni ridhaa. Ili uongoze inatakiwa unaowaongoza waridhie na uongozi wako.

Kwa sasa hakuna mtanzania anaefurahishwa na mwenendo wa wizara unayoiongoza. Hakuna zuri la kufurahisha kwenye wizara yako, hakuja hata kimoja kwako cha kujivunia, hakuna jipya. Umepwaya, umeshindwa, umeanguka. Umemsononesha hata yule aliyekuteua kukupa majukumu hayo!

Nishati ya umeme ni nguzo kuu ya maendeleo ya taifa. Hukufaham umuhim wake, ukafuruhia kupata nafasi hiyo, ukajisahau, sasa umetusababishia janga la kitaifa, huna majibu sahihi ya hatma ya janga hili, huna cha kusubiri, ondoka.

JK ametembea dunia nzima kutafuta wawekezaji, kusini, kaskazini, mashariki na magharibi, imekuwa bure, hasara kwa taifa na upotevu wa bure wa kodi zetu, kwani hakuna uwekezaji kwenye kiza, hakuna uwekezaji kwenye umeme unaotegemea hatma ya mungu kuleta mvua.
Ondoka, umeleta siasa kwenye umeme, huku ukifahamu siasa haziwashi umeme.

Ondoka. Umesababisha mauaji kwa kukata umeme na kusababisha joto kali kwenye maghala ya kuhifadhia mabomu gongo la mboto na kuua halaiki ya watu, kusababisha mayatima, vilema na homeless innocent civilians.

Huna haja ya kuendelea kuwepo. Hila zako zote zimegonga mwamba. Wewe na company yako. Kila uongo umebainika, kuanzia mikataba ya uongo, wamiliki wa kufoji wa dowans, hadi hila dhaifu za kupitisha bajeti yako kwa hongo.

Huna mvuto kwa watanzania kama waziri. Una force tu kuendelea na wizara hiyo. Hakuna kinachoendelea kukuweka hapo, zaidi ya ubinafsi, ung'ang'anizi na ukibaraka.
 
Lakini lazima tujue ya kuwa january makamba naye hawezi nafasi hiyo
 
Maoni yako yanaelekea japo hayana uzito

kwakuwa wewe huathiriki na tatizo la kukatika kwa umeme, si una standby generator na pesa nyingi za kununulia mafuta? Huwezi kuona uzito wa tatizo la wizara hii
 
Jairo aliyekamatwa na mkia kapewa likizo (ya malipo!) kwa hiyo Ngeleja ni salama kabisa - hakuna 'ushahidi' wa kumfukuzisha kazi!
 
Asipoondolewa au kujiondoa kitatokea nini?

Tutaishia kupiga kelele tu
 
Mtamuonea tu Ngeleja wa watu,huyu ni waziri wa tatu wizara hii katika awamu hii,tatizo tunaishi 'kidharura dharura' tu, hata akikabidhiwa nani bila serikali yote kuamua Umeme ni tatizo na kulekeza juhudi na hela kulitatua wizara hii itakuwa siti ya daladala kashuka huyu kapanda huyu.
 
Kwa kawaida Bajeti ikitolewa Shilingi either Waziri au Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anapoteza kazi yake; kwasababu lazima iandikwe upya

Ni Juu ya Rais Kikwete kuamua... Yeye ni Mpole Sidhani kama atamuondoa Ngeleja
 
Kwa trend ya nchi hii Ngeleja ataendelea kula bata mwanzo mwisho
 
Mtamuonea tu Ngeleja wa watu,huyu ni waziri wa tatu wizara hii katika awamu hii,tatizo tunaishi 'kidharura dharura' tu, hata akikabidhiwa nani bila serikali yote kuamua Umeme ni tatizo na kulekeza juhudi na hela kulitatua wizara hii itakuwa siti ya daladala kashuka huyu kapanda huyu.
alivyo pata ndivyo atakavo ondoka
 
Ondoka. Umesababisha mauaji kwa kukata umeme na kusababisha joto kali kwenye maghala ya kuhifadhia mabomu gongo la mboto na kuua halaiki ya watu, kusababisha mayatima, vilema na homeless innocent civilians.
Na akitoka tu akutane na pingu zinamsubiri apelekwe mahakamani akajibu kesi yake hiyo!
 
Asipoondolewa au kujiondoa kitatokea nini?

Tutaishia kupiga kelele tu
Asipojiondoa ataondolewa aliyemuweka.... akishidwa kumuondoa aliyemuweka basi yeye aliyemuweka itabidi ajiondoe na yeye asipojiondoa basi SISI (UMMA) tutamuondoa......... tutampa siku 90
 
Nani amekuambia kuwa huyo ni kiongozi wa wananchi?Huyo aliteuliwa mpaka aliemteua anune ndo atatoka nduki!
 
Ngoja asome hiyo bajeti then tumtoe, nafikiri serikali ya CCM tuanze kuiwajibisha sisi wenyewe sababu viongozi wake ni weak. hatuwezi kukaa gizani 18 hrs per day then waziri anakuja na mipango lukuki ya kwenye makaratasi isiyotekelezeka - hatutaki wote tunaonekane wazezeta.
 
''am very secured so don't expect me to leave this position''
 
Ngeleja,
Hakuna cha kusubiri, uongozi ni ridhaa. Ili uongoze inatakiwa unaowaongoza waridhie na uongozi wako.


Mkuu,Ngeleja anaongoza wafanyakazi wa wizara yake sasa unaposema anawaowaongoza hawajaridhia basi lazima uje na ushahidi wa akina nani hawajaridika ana utendaji wake .


Kwa sasa hakuna mtanzania anaefurahishwa na mwenendo wa wizara unayoiongoza. Hakuna zuri la kufurahisha kwenye wizara yako, hakuja hata kimoja kwako cha kujivunia, hakuna jipya. Umepwaya, umeshindwa, umeanguka. Umemsononesha hata yule aliyekuteua kukupa majukumu hayo!


watu hawaridhiki na mwenendo wa miradi ya umeme na siyo wizara hivyo jitahidi kujenga hoja na siyo kukurupuka tu.Yapo mazuri kama wizara ambayo yamefanyika na yanahitaji kupewa sifa.suala la Umeme ni tatizo ambalo hata mimi mwenyewe linanikera ila sidhani kama waziri ndiyo anasababisha kuwapo huu mgao

Nishati ya umeme ni nguzo kuu ya maendeleo ya taifa. Hukufaham umuhim wake, ukafuruhia kupata nafasi hiyo, ukajisahau, sasa umetusababishia janga la kitaifa, huna majibu sahihi ya hatma ya janga hili, huna cha kusubiri, ondoka.




JK ametembea dunia nzima kutafuta wawekezaji, kusini, kaskazini, mashariki na magharibi, imekuwa bure, hasara kwa taifa na upotevu wa bure wa kodi zetu, kwani hakuna uwekezaji kwenye kiza, hakuna uwekezaji kwenye umeme unaotegemea hatma ya mungu kuleta mvua.
Ondoka, umeleta siasa kwenye umeme, huku ukifahamu siasa haziwashi umeme.
Hapa JK ameingiaje?uwekezaji wa symbion unadhani umekuja hivi hivi?ule wa Kiwira je?Miradi mingine mipya imekuja hivi hivi tu...come on


Ondoka. Umesababisha mauaji kwa kukata umeme na kusababisha joto kali kwenye maghala ya kuhifadhia mabomu gongo la mboto na kuua halaiki ya watu, kusababisha mayatima, vilema na homeless innocent civilians.
ona unaleta viroja,Mauaji gani ambayo yamefanyika na yamefanywa na waziri?kweli mabomu yalilipuka kutokana na joto?kuna AC pale..au unaongea kama kijana wa kijiweni tu...ha ha ha


Huna haja ya kuendelea kuwepo. Hila zako zote zimegonga mwamba. Wewe na company yako. Kila uongo umebainika, kuanzia mikataba ya uongo, wamiliki wa kufoji wa dowans, hadi hila dhaifu za kupitisha bajeti yako kwa hongo.


Mikataba ipi ni ya uongo?wamiliki wa kufoji ni wakinani hao?


Huna mvuto kwa watanzania kama waziri. Una force tu kuendelea na wizara hiyo. Hakuna kinachoendelea kukuweka hapo, zaidi ya ubinafsi, ung'ang'anizi na ukibaraka.

Sikuwahi kujua kama mvuto ni sifa ya mtu kuwa waziri...


You know JF ni sehemu ya kukata issue na kumkoma nyani giladi..issue hizi za kimajungu majungu hazina nafasi na hapa si maali pake..

wabunge wana nafasi kubwa ya kuamua kuhusu suala la umeme..Yes na mawazo yote yapo hapa


https://www.jamiiforums.com/hoja-nz...a-the-use-of-emergency-powers-act-1986-a.html


na kama kweli wabunge wanataka wanachokitaka waidhinishe fedha za kutosha ili mradi wa Stielger's Gorge uanze
 
JK ametembea dunia nzima kutafuta wawekezaji, kusini, kaskazini, mashariki na magharibi, imekuwa bure, hasara kwa taifa na upotevu wa bure wa kodi zetu, kwani hakuna uwekezaji kwenye kiza, hakuna uwekezaji kwenye umeme unaotegemea hatma ya mungu kuleta mvua.
Ondoka, umeleta siasa kwenye umeme, huku ukifahamu siasa haziwashi umeme.

Hapo kwenye redi ndo pameniacha hoi, hakika mimi nakwambia mpaka siku ambayo JK atatembelea Nyamongo na Ryorya ndo Umeme utawaka. Ngereja hawezi kujiuzuru hadi CCM ishinde Igunga.
 
Kwa swala la mabagara na gombss,,,,nadhan MWINY NDO WA KUONDOKA,HATA KAMA HAKUKUWA NA UMEME WANGEWEZA KUZUIA,,,KWAN YALIPOLIPUKA MBAGARA KULIKUA NA MGAO????,,,,,
Ngeleja,Hakuna cha kusubiri, uongozi ni ridhaa. Ili uongoze inatakiwa unaowaongoza waridhie na uongozi wako.Kwa sasa hakuna mtanzania anaefurahishwa na mwenendo wa wizara unayoiongoza. Hakuna zuri la kufurahisha kwenye wizara yako, hakuja hata kimoja kwako cha kujivunia, hakuna jipya. Umepwaya, umeshindwa, umeanguka. Umemsononesha hata yule aliyekuteua kukupa majukumu hayo!Nishati ya umeme ni nguzo kuu ya maendeleo ya taifa. Hukufaham umuhim wake, ukafuruhia kupata nafasi hiyo, ukajisahau, sasa umetusababishia janga la kitaifa, huna majibu sahihi ya hatma ya janga hili, huna cha kusubiri, ondoka.JK ametembea dunia nzima kutafuta wawekezaji, kusini, kaskazini, mashariki na magharibi, imekuwa bure, hasara kwa taifa na upotevu wa bure wa kodi zetu, kwani hakuna uwekezaji kwenye kiza, hakuna uwekezaji kwenye umeme unaotegemea hatma ya mungu kuleta mvua.Ondoka, umeleta siasa kwenye umeme, huku ukifahamu siasa haziwashi umeme. Ondoka. Umesababisha mauaji kwa kukata umeme na kusababisha joto kali kwenye maghala ya kuhifadhia mabomu gongo la mboto na kuua halaiki ya watu, kusababisha mayatima, vilema na homeless innocent civilians.Huna haja ya kuendelea kuwepo. Hila zako zote zimegonga mwamba. Wewe na company yako. Kila uongo umebainika, kuanzia mikataba ya uongo, wamiliki wa kufoji wa dowans, hadi hila dhaifu za kupitisha bajeti yako kwa hongo.Huna mvuto kwa watanzania kama waziri. Una force tu kuendelea na wizara hiyo. Hakuna kinachoendelea kukuweka hapo, zaidi ya ubinafsi, ung'ang'anizi na ukibaraka.
 
mkuu,ngeleja anaongoza wafanyakazi wa wizara yake sasa unaposema anawaowaongoza hawajaridhia basi lazima uje na ushahidi wa akina nani hawajaridika ana utendaji wake .





Watu hawaridhiki na mwenendo wa miradi ya umeme na siyo wizara hivyo jitahidi kujenga hoja na siyo kukurupuka tu.yapo mazuri kama wizara ambayo yamefanyika na yanahitaji kupewa sifa.suala la umeme ni tatizo ambalo hata mimi mwenyewe linanikera ila sidhani kama waziri ndiyo anasababisha kuwapo huu mgao

nishati ya umeme ni nguzo kuu ya maendeleo ya taifa. Hukufaham umuhim wake, ukafuruhia kupata nafasi hiyo, ukajisahau, sasa umetusababishia janga la kitaifa, huna majibu sahihi ya hatma ya janga hili, huna cha kusubiri, ondoka.





Hapa jk ameingiaje?uwekezaji wa symbion unadhani umekuja hivi hivi?ule wa kiwira je?miradi mingine mipya imekuja hivi hivi tu...come on



ona unaleta viroja,mauaji gani ambayo yamefanyika na yamefanywa na waziri?kweli mabomu yalilipuka kutokana na joto?kuna ac pale..au unaongea kama kijana wa kijiweni tu...ha ha ha





mikataba ipi ni ya uongo?wamiliki wa kufoji ni wakinani hao?




Sikuwahi kujua kama mvuto ni sifa ya mtu kuwa waziri...


You know jf ni sehemu ya kukata issue na kumkoma nyani giladi..issue hizi za kimajungu majungu hazina nafasi na hapa si maali pake..

Wabunge wana nafasi kubwa ya kuamua kuhusu suala la umeme..yes na mawazo yote yapo hapa


https://www.jamiiforums.com/hoja-nz...a-the-use-of-emergency-powers-act-1986-a.html


na kama kweli wabunge wanataka wanachokitaka waidhinishe fedha za kutosha ili mradi wa stielger’s gorge uanze

upuuuzi mtupu!!! Unataka ushahid gani kuonyesha watz walimchoka ngeleja na baadhi ya mawaziri wengine wa jk??
Unataka ushahid gani kujua mikataba mobovu iliyoingiwa ktk sekta ya umeme??
Unata ushajid gani kuona kuhusika kwa jk ktk hii hali tuliyonayo??
Unataka ushahid gani kuona safari za jk zinavyozid kutuumiza kama taifa??
Kama hujauona ushahid mpakasasa hautaweza kuuoona milele!!
Maana akili zako zipo tumboni na machoyako yapo mfuko. ...nyie ndio vibaraka mnaouza nchi kwa mlo wa siku moja, watu kama nyinyi uarabuni ni kitanz tu.
 
Back
Top Bottom