Makoye Matale
JF-Expert Member
- May 2, 2011
- 6,490
- 2,104
Kucheza mpira ni ajira kama ajira nyingine, mchezaji pia anayo haki ya kuonesha mapenzi kwa klabu anayoipenda kama alivyofanya Ngassa. Azam wanashindwa kuelewa uhuru huo, huwezi kumlazimisha mchezaji apende klabu yako wakati yuko hapo kwa ajili ya ajira. Hata Kaseja alipojiunga Yanga hakuna mtu aliyeamini kuwa Kasejea anaipenda Yanga zaidi ya kufuata maslahi, alivyorejea Simba hakuna pia aliyeshangaa. Kaseja akiwa Yanga alicheza kwa nguvu zake zote na kwa uaminifu mkubwa isipokuwa katika mechi ya mwisho ya ligi ambapo mchezo huo uliisha kwa matokeo ya Yanga 2-2 Simba, siku hiyo alifungwa na Simba mabao ya kitoto sana hata kuibua hisia kwamba anawaachia Simba makusudi. Ngassa akiwa Azam kafanya hivyo hivyo.
Ngassa kwenda Simba ni haki yake pia maadam maslahi yapo, hii haiondoi mapenzi yake makubwa kwa klabu yake adhimu Young Africans Sports Club, Simba waelewe kuwa hiyo ni ajira kama Yanga walivyomuelewa Kaseja. Siku Simba akifungwa na Yanga wasianze kulalama kama ilivyokuwa kwa Kelvin Yondan.
Kijana Ngassa nampa pole kwa masahibu yaliyompata huko Azam FC., lakini pia niwapongeze Simba SC kwa kumpa nafasi ya kuboresha kiwango chake cha soka.
Nampa pole pia kijana Sureboy kwa masahibu ya jinsi hiyo. Sioni kama huyu dogo anastahili kuhukumiwa jinsi hii maana hata siku ya mechi ya Yanga aling'ara maridhawa, sasa sielewi kama Azam FC kwa mawazo yao finyu walidhani wataifunga Yanga kila siku kama walivyofanya huko nyuma wakati wa migogoro lukuki ndani ya klabu. Endapo Sureboy ataendelea kunyanyapaliwa ni vyema akajiunga na klabu nyingine na kuachana na hao Azam FC na huu ndiyo utakuwa mwisho wao (The rise and fall of Azam FC), klabu gani inaongozwa kifamilia, hii lazima ife amini usiamini hakuna good governance hapa ni ubabe na majungu tu.
Msomaji sitaki nikuchoshe, naomba niishie hapa kwa sasa.
Ngassa kwenda Simba ni haki yake pia maadam maslahi yapo, hii haiondoi mapenzi yake makubwa kwa klabu yake adhimu Young Africans Sports Club, Simba waelewe kuwa hiyo ni ajira kama Yanga walivyomuelewa Kaseja. Siku Simba akifungwa na Yanga wasianze kulalama kama ilivyokuwa kwa Kelvin Yondan.
Kijana Ngassa nampa pole kwa masahibu yaliyompata huko Azam FC., lakini pia niwapongeze Simba SC kwa kumpa nafasi ya kuboresha kiwango chake cha soka.
Nampa pole pia kijana Sureboy kwa masahibu ya jinsi hiyo. Sioni kama huyu dogo anastahili kuhukumiwa jinsi hii maana hata siku ya mechi ya Yanga aling'ara maridhawa, sasa sielewi kama Azam FC kwa mawazo yao finyu walidhani wataifunga Yanga kila siku kama walivyofanya huko nyuma wakati wa migogoro lukuki ndani ya klabu. Endapo Sureboy ataendelea kunyanyapaliwa ni vyema akajiunga na klabu nyingine na kuachana na hao Azam FC na huu ndiyo utakuwa mwisho wao (The rise and fall of Azam FC), klabu gani inaongozwa kifamilia, hii lazima ife amini usiamini hakuna good governance hapa ni ubabe na majungu tu.
Msomaji sitaki nikuchoshe, naomba niishie hapa kwa sasa.