Ngara: Polisi wavamia kijiji usiku wa manane na kuondoka na mmoja

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Polisi wilayani Ngara wamevamia kijiji cha Mgoma, kata ya Mgoma na mkamata ndugu Peter Safari wa Kijiji cha Mgoma, kata ya Mgoma saa 8 za usiku wa kuamkia leo na kuondoka naye kusikojulikana. Wakati huo huo, walifika nyumbani kwa William Marco, ambaye walikuta hayupo nyumbani kwake usiku huo hivyo wamechukua pikipiki yake. Mpaka sasa Polisi wilayani Ngara haijatoa taarifa yoyote.

Tangu lini polisi wanakamata raia katika makazi yao saa 8 za usiku? Vibali walivipata wapi vya kukamata raia saa 8 za usiku? Huo ndio ulinzi wa amani au uhalifu wa amani? Taarifa hizi zinasikitisha. Ni dalili kuwa serikali kupitia kwa polisi inawanyanyasa raia jambo ambalo linaweza kuleta mchafuko. Ikumbukwe kuwa katika wiki mbili zilizopita, raia mmoja na Polisi wawili waliuawa katika kata ya mgoma na kituo cha polisi kuchomwa moto.

Tukipata taarifa zaidi, nitawaletea.

Source: Mimi mwenyewe nikiwa Ngara
 
Polisi wilayani Ngara wamevamia kijiji cha Mgoma, kata ya Mgoma na mkamata ndugu Peter Safari wa Kijiji cha Mgoma, kata ya Mgoma saa 8 za usiku wa kuamkia leo na kuondoka naye kusikojulikana. Wakati huo huo, walifika nyumbani kwa William Marco, ambaye walikuta hayupo nyumbani kwake usiku huo hivyo wamechukua pikipiki yake. Mpaka sasa Polisi wilayani Ngara haijatoa taarifa yoyote.

Tangu lini polisi wanakamata raia katika makazi yao saa 8 za usiku? Vibali walivipata wapi vya kukamata raia saa 8 za usiku? Huo ndio ulinzi wa amani au uhalifu wa amani? Taarifa hizi zinasikitisha. Ni dalili kuwa serikali kupitia kwa polisi inawanyanyasa raia jambo ambalo linaweza kuleta mchafuko. Ikumbukwe kuwa katika wiki mbili zilizopita, raia mmoja na Polisi wawili waliuawa katika kata ya mgoma na kituo cha polisi kuchomwa moto.

Tukipata taarifa zaidi, nitawaletea.

Source: Mimi mwenyewe nikiwa Ngara

Kama huyo mtu amefanya kosa polisi wanayo haki ya kisheria kumtafuta popote alipo na muda wowote iwe usiku au mchana na saa yoyote
 
Uelewa wako ni mdogo

hua ina walazimu polisi kumkamata m2 hata kama iwe saa nane usiku...
 
Mleta mada kama vile si mtanzania. Kwa hiyo mke wake akibakwa saa nane za usiku, polisi watasubili papambazuke ndo mbakaji akamatwe! Kigezo kwamba raia mmoja na polisi walikufa si kigezzo cha kuzuia polisi kufanya kazi zao. Labda kama kuna haki zimekiukwa katika utekelezwaji wa majukumu hayo ya polisi, hiyo ndo hoja ya kujadili.
 
Mi sikuelewa huyo mmojani kuku,mbuzi,ng'ombe,na kama ni binadamu je ni ngariba,jambazi,mchuna ngozi ama nini..
 
Polisi wilayani Ngara
wamevamia kijiji cha Mgoma, kata ya Mgoma na mkamata ndugu Peter
Safari
wa Kijiji cha Mgoma, kata ya Mgoma saa 8 za usiku wa kuamkia
leo na kuondoka naye kusikojulikana. Wakati huo huo, walifika nyumbani
kwa William Marco, ambaye walikuta hayupo nyumbani kwake usiku
huo hivyo wamechukua pikipiki yake. Mpaka sasa Polisi wilayani Ngara
haijatoa taarifa yoyote.

Tangu lini polisi wanakamata raia katika makazi yao saa 8 za usiku?
Vibali walivipata wapi vya kukamata raia saa 8 za usiku? Huo ndio ulinzi
wa amani au uhalifu wa amani? Taarifa hizi zinasikitisha. Ni dalili
kuwa serikali kupitia kwa polisi inawanyanyasa raia jambo ambalo
linaweza kuleta mchafuko. Ikumbukwe kuwa katika wiki mbili zilizopita,
raia mmoja na Polisi wawili waliuawa katika kata ya mgoma na kituo cha
polisi kuchomwa moto.

Tukipata taarifa zaidi, nitawaletea.

Source: Mimi mwenyewe nikiwa Ngara

We mwizi wewe! unaogopa polisi! au ni mmoja wa watenda maovu!
 
Back
Top Bottom