Neno 'mtukufu' badala ya mheshimiwa

Neno 'mtukufu' badala ya mheshimiwa

Mtoa mada usiwe ******
Anzeni kukataa bunge lisiitwe "bunge tukufu"
Waambie wazee wa ukuta watoe hoja hayo maneno yasiwe yanatamkwa bungeni
Kwani sehemu tukufu ni nyumba za ibada.
Bunge kama mkusanyiko wa wananchi kuamua mambo mema juu yao ni halali kuitwa bunge tukufu, ila mtu kuitwa mtukufu ni sifa ambayo si ya kuendekeza.
 
Mungu tu hatakiwi kujaribiwa lakini kwa binadamu kujaribiwa ni kawaida,kwahiyo
binadamu asichukie kujaribiwa
Kazi ya kuleta majiribu kwa watu ni ya shetani, huyo binadamu anayetaka kumjaribu binadamu mwenzake tumfikiriieje?
 
Kamwe huwezi kuwa MTUKUFU ukiwa na roho mbaya, roho iliyojaa visasi kama huyu Mungu wa Ikulu.

Mara ya kwanza nilipomsikia Lissu akilitumia kumtaja Mh. Rais, nilijua ni panic za kutoka mahabusu. Ila sasa haka kamchezo kanaendelea.

My concerns ni kuwa Tanzania hutajawahi kupata Rais aliyejiita mtukufu. Tulizoea kusikia hilo neno kwa jirani zetu wakenya enzi za Daniel na tuliona siyo sawa.

Kujiita mtukufu ni kujikweza kwa hali ya juu. Hili neno likiachwa lishamiri huko mbeleni litageuzwa kuleta picha mbaya kwa Mh Rais.

Wito wangu mamlaka husika zisiache hili jambo likue.

Nawasilisha!
 
Mi nafikiri kumuita mtukufu inaweza kuwa sawa..maana alisema mwenyewe kuwa hajaribiwi na wala hatajaribiwa....na Mungu tuna muita Mtukufu kwa kuwa hajaribiwi na hakuna wa kumjaribu vinginevyo adhabu I juu yake.
Kazi ya kumjaribu mtu ni kazi ya ibilisi. Nashangaa binadamu nao wanaililia ili wamjaribu rais, kama siyo ushetwani ni nin?
 
Hapana. Wa kwanza kulikataa alikuwa ni Mzee Ruksa na alichagizwa na Masheikh kuwa "anakubali kwa dhati yake kuwa, yeye ni mtukufu?" Swali likawa gumu kwake!
Neno mtukufu liliisha utawala wa Mkapa. Yeye ndio alikataa kuitwa mtukufu. Nyerere na Mwinyi wote walikuwa watukufu. Mleta mada achakukimbilia kuandika vitu usivyovijua.
 
nimekuwa nikifikilia sana bila majibu..

kwanini Raisi wa Jamhuri wa Muungano, alifikia hatua na kusema "Wewe DK Shein, wakitoka Malaika unafuata wewe"
kauli hizi zimeendelea kwendana sanjari na kauli za raisi kuitwa Mtukufu (Mtakatifu) na kukiri yye mwenyewe kuwa hajaribiwi na mtu asidhubutu kumjaribu, atakiona cha moto...

tukirudi nyuma rais Benjamin Mkapa, alikataa kuitwa mtukufu na hata Yesu mwenyewe alikataa kuitwa Mtukufu/mtakatifu hapa dunian, (MARK 10:17..) na Yesu ndiye kiumbe chenye ubinadamu kilichoweza kushinda majrbu yote na wala sio mwingne

Ujasili wa Mganga mkuu kujiita yy mtukufu asiyejaribiwa anautoa wap?
 
Hapana. Wa kwanza kulikataa alikuwa ni Mzee Ruksa na alichagizwa na Masheikh kuwa "anakubali kwa dhati yake kuwa, yeye ni mtukufu?" Swali likawa gumu kwake!
Duh, hilo swali lilikuwa gumu!
 
Mara ya kwanza nilipomsikia Lissu akilitumia kumtaja Mh. Rais, nilijua ni panic za kutoka mahabusu. Ila sasa haka kamchezo kanaendelea.

My concerns ni kuwa Tanzania hutajawahi kupata Rais aliyejiita mtukufu. Tulizoea kusikia hilo neno kwa jirani zetu wakenya enzi za Daniel na tuliona siyo sawa.

Kujiita mtukufu ni kujikweza kwa hali ya juu. Hili neno likiachwa lishamiri huko mbeleni litageuzwa kuleta picha mbaya kwa Mh Rais.

Wito wangu mamlaka husika zisiache hili jambo likue.

Nawasilisha!
Acha tumwite MTUKUFU MUHESHIMIWA RAIS JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI maana anastahili. ...amen. ..
 
Back
Top Bottom