Neno La Leo: Hakuna Anayekufa Na Sifuri..!

Neno La Leo: Hakuna Anayekufa Na Sifuri..!

maggid

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2006
Posts
1,084
Reaction score
1,250
Ndugu zangu,

Nimesoma juu ya Mabadiliko Makubwa kuhusiana na Mitihani ya Sekondari hapa nchini.

Kwamba mfumo umebadilishwa. Na kuwa kuanzia sasa hakutakuwa na division ziro. Naam, hakuna sifuri.

Habari hiyo imenikumbusha dada huyo pichani, anaitwa Mariam, ni muhudumu kwenye moja ya ofisi za mjini Dar es Salaam. Si kawaida kuwakuta Watanzania wakisoma vitabu. Na nilipomwona akiwa ameshika kitabu cha mwandishi Edwin Semzaba kiitwacho ' Marimba ya Majaliwa' ilibidi niongee nae kuhusiana na maudhui ya kitabu hicho ambacho mimi pia nimeshakisoma.

Kwa maneno yake mwenyewe, na si ya kuyasoma kitabuni, aliweza kutumia dakika kumi nzima kunisimulia yaliyo kitabuni. Mariam amemaliza Kidato Cha Nne na sikumwuliza alipata daraja gani. Yawezekana naye alitoka na sifuri.

Lakini, tukubali, mwanadamu hawezi kumaliza miaka minne shuleni halafu atoke na sifuri. Na kama ni hivyo, basi, ama alikuwa akiudhuria darasa lisilo na mwalimu au mwalimu wake alikuwa ni punguani.

Mimi kama Mwalimu pia, na kwa kumsikiliza Mariam akinisimulia yaliyomo kwenye kitabu alichosoma, na ningekuwa ni mwalimu wake wa fasihi, basi, isingewezekana kabisa Mariam atoke na sifuri shuleni.

Na akina Mariam wako wengi. Mifumo yetu ya elimu inawakatisha tamaa. Na laiti wangepimwa uwezo wao kwa namna nyingine, basi, wangefika mbali pia kielimu.

Nachukua fursa hii kuipongeza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kuchukua hatua hii ya kubadilisha mfumo wa mitihani.

Ingawa changamoto inabaki kama ilivyoelezwa na Dk. Joyce Ndalichako, kuwa tuna ukosefu wa uadilifu miongoni mwa walimu. Kwamba wanadanganya pale wanapotoa ripoti za maendeleo ya mwanafunzi. Na kama asilimia 40 ya ufaulu itatokana na Continious Assesment ( CA) kwa maana ya maendeleo ya mwanafunzi. Basi, mkazo utiliwe kwenye uadilifu wa walimu.

Vinginevyo, kila mwanadamu ana uzoefu na maarifa anayoyakusanya tangu kuzaliwa. Kuna anayoyapata shuleni ( Episteme) na kuna yale ya maishani ( Fronesis).

Hivyo, hakuna anayekufa na sifuri.

Ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa.
Iringa.
 
wapimwe uwezo kwa namna nyingine?

kukariri bongofleva na bongo movies?

waletewe maswali ya

1.mtindo wa ngololo ulianzishwa na nani?

Wema sepetu amecheza filamu ngapi?

naona hapo 'tutashangaa uwezo wa wanafunzi wetu'
 
Division 5 ni jina tu kama ilivyokuwa Division Zero...sioni la kupongeza zaidi ni mbinu tu iliyotumik kutoa faraja...
 
Huu ni aina ya ukwepaji wa uboreshaji wa mashule ya serikali na ya kata!
Aibu sana kwa master-mind wa ujinga huo!
 
maggid hata mtu akipata moja, we shud apriciate, hiyo siyo sifuri.
 
Last edited by a moderator:
maggid hata mtu akipata moja, we shud apriciate, hiyo siyo sifuri.

Tu' appriciate nini katika 0? Kwamba anajua kusoma na kuandika?

Tatizo langu ni kwamba tunajua wanafunzi wengi walivyo siku hizi, hata hizo maksi wanazopata sio ukomo wa uwezo wao!!

Tunaelewa kuna mapungufu mengi sana katika mfumo mzima na mazingira ya elimu kwa ujumla ila wanafunzi hao pia wanaweza zaid ila kwa kiasi kikubwa hawakujitahidi kias cha kutosha!?

Unataka wapongezwe kwa lipi wanapopata division 0?!

Ninaye ndugu yangu ambaye pia alipata 0 mwaka jana, na nikiangalia na kuongea nae ni kweli matokeo yake yanamstahili, ningeshangaa sana kama walau angepata div 3; uzuri nae wakati akinieleza nia yake ya kutaka kurudia madarasa alikiri kuwa ni kweli hakujitahidi kias cha kutosha, kwa maneno yake anasema alikua na kampan ambayo kiukweli hawakua wakisoma kabisa!

Sasa huyu nae tu'appreciate aliyofanya?!
Mwakani najua ufaulu utaonesha 'kupanda' maana kama mtu mmoja alivyoandika humu wameloanisha pamba kabla ya kuipima lazima uzito uwe mkubwa!

Bahati mbaya ni kwamba kwa viwango hivyo kubweteka kupo kwingi sana, macho hudanganya akili kuwa inaweza maana vinaonekana viko chin (A hadi 75 na B hadi 50) kuliko wakati mwingine wowote, je matokeo yatakapokua mabaya tena tutaenda wapi? tutamlaumu nani?

Ila nilikwambia awali na ninarudia, ninamuomba Mungu atujalie maisha marefu ili sote tushuhudie hiki kilichotengenezwa!
 
Last edited by a moderator:
Tuseme nini kwa wale:
1. Wanaochora mazombi kwenye booklets

2. Wanaoandika mistari ya bongofleva badala ya kujibubu maswali

3. Wanaoandika matusi je ?

Hao nao wana ufaulu mdogo ??
 
Hata hivyo hakuna division zero! Kuna I, II, III, IV na FAIL. We zero umeitoa wapi? Unataka kusema wanafunzi hawafeli? Kama ndivyo, kwa nini walimu hufundishwa Research Evaluation & Measurement (REM). Na kama hawafeli kwa nini kuna tools kama Standardized tests, teacher-made tests etc

cc: Kitila Mkumbo
 
Last edited by a moderator:
Kaka mjengwa! Matokeo ya necta hakuna div.0, kuna div 1-4 & fail. Refer website yao. Bado div5 itaitwa 0 manake ni mazoe
 
Mkuu Maggid , wazo la serikali ni zuri ila kuna jambo moja linanitatiza kwani sijaweza fahamu ni namna gani serikali itawatumia au ina mpango upi na kundi la wataokuwa wamepata ufaulu wa daraja la 4 na la 5 (ufaulu hafifu) ? au ndo watabaki mtaani/ vijiweni na divisions zao?
Naomba kujuzwa kama serikali ina mpango mkakati juu ya hilo kundi tajwa.
 

Attachments

  • imagesGF.jpg
    imagesGF.jpg
    10.3 KB · Views: 59
  • index.jpg
    index.jpg
    8.6 KB · Views: 50
Jambo muhimu nu kutilia mkazo mafunzo ya vitendo badala ya kuegemea sana kwenye nadharia....

Ni rahisi sana kumfundisha binadamu kwa vitendo kuliko kumlazimisha akariri.

Mafunzo ya vitendo yataongeza ubora wa elimu yetu.


Ningeshauri shule zote za sekondari zifuate mfumo wa VETA.

au tufute shule zote za sekondari tubakishe vyuo vya ufundi tu.

Ukimaliza la saba unaingia VETA miaka mitano kisha Chuoni .
 
Mfumo mpya ni JANGA lingine katika elimu ya Mtanzania kama yale yaliyotangulia katika mfumo wa elimu la kurudia mitihani ya kidato cha nne baada ya mwanafunzi kufeli na mikakati ya kuua juhudi za kufundisha ndani ya kipindi kwa kuanzisha TUITION. Ili tufikirie vizuri juu ya mfumo wa Elimu Tanzania, tuchukue kipindi mpaka mwaka 1988. Mitahala ya wakati huo na uwajibikaji wa wanataaluma wa masuala ya Elimu walikuwa makini sana, mabadiliko yaliyofuata hapo, yalitoa nafasi ya kufeli na kupungua kwa juhudi za walimu madarasani. Nitarudi!
 
Division 5 ni jina tu kama ilivyokuwa Division Zero...sioni la kupongeza zaidi ni mbinu tu iliyotumik kutoa faraja...

Fier
Tofauti ipo tena kubwa sana! Utafiti umeonyesha kuwa kuna uhusiano mkubwa sana baina ya ufaulu na mwanafunzi kuandaliwa kisaikolojia unapoweka division fail ambao mnaiita zero hii haitoi picha halisi ya mazingira ya kitu inaitwa elimu, nikuulize swali hivi inawezekana kabisa mtu akashindwa kujua hata jina lake na namba yake ya mtihani? Maana instruction pia ni sehemu ya mtihani ondoa ukweli ya kwamba hata hio maksi 1 nayo pia si sifuri! Sasa kwa nini tusiliite daraja hili division 5 kwa maana ya " ufaulu hafifu" isitoshe wakati wa mfumo wa mwanzo ukiwa na hio zero maana yake hupewi cheti, hebu tujiulize kwanini asipewe cheti wakati amehitimu masomo ya kidato husika ijapokuwa ni kwa "ufaulu hafifu" au mnafikiri kuhitimu ni kupata A tu!
 
Yaani kali zaidi ni ile ya kumpa alama za maendeleo ya kila siku mtahiniwa wa QT eti unaziweka hizo hizo kwa masomo yote, kazi kweli
 
Back
Top Bottom