Neno kuu la leo: Upendo haugawanyiki kamwe wana jf!

KIDUNDULIMA

JF-Expert Member
Aug 18, 2010
966
537
Wana JF nemeona ni vizuri tushilikiane neno kuu la leo ambalo linasema Upendo kati ya wapendanao haugawanyiki kamwe. Hii ni kutokana kwamba wivu ambao mwanaume unao ndio uleule alionao mwanamke. Mfano kama una mke na mke huyo anakwenda kufanya mambo yale ya kiutu uzima nje ya uhusiano wenu, wivu utakaokuwa nao ndio huohuo atakaoupata mwanamke pale mwanaume utakapoamua kuasi na kwenda nje ya ndoa au mahusiano yenu kuanzisha nyumba ndogo,ya kati na kubwa.

Hivyo wana JF tusigawanye upendo maana haugawiki. Mwisho wake utauzidisha kwa mmoja na kuupunguza kwa mwingine na kuleta migongano katika nyumba na kukosa mwelekeo.

Ni hayo tu kwa leo.
 
Wana JF nemeona ni vizuri tushilikiane neno kuu la leo ambalo linasema Upendo kati ya wapendanao haugawanyiki kamwe. Hii ni kutokana kwamba wivu ambao mwanaume unao ndio uleule alionao mwanamke. Mfano kama una mke na mke huyo anakwenda kufanya mambo yale ya kiutu uzima nje ya uhusiano wenu, wivu utakaokuwa nao ndio huohuo atakaoupata mwanamke pale mwanaume utakapoamua kuasi na kwenda nje ya ndoa au mahusiano yenu kuanzisha nyumba ndogo,ya kati na kubwa.

Hivyo wana JF tusigawanye upendo maana haugawiki. Mwisho wake utauzidisha kwa mmoja na kuupunguza kwa mwingine na kuleta migongano katika nyumba na kukosa mwelekeo.

Ni hayo tu kwa leo.

Mie naona kichwa cha habari na paragraph ya pili vinajichanganyana,kitendo cha kukubali kwamba unaweza kuuzidisha au kuupunguza kwa mmoja wao,unathibitisha kwamba upendo unagawanyika.Ebu rudi tena uweke maelezo yako sawa kabla infidelities hawajaamka.
 
Mie naona kichwa cha habari na paragraph ya pili vinajichanganyana,kitendo cha kukubali kwamba unaweza kuuzidisha au kuupunguza kwa mmoja wao,unathibitisha kwamba upendo unagawanyika.Ebu rudi tena uweke maelezo yako sawa kabla infidelities hawajaamka.

Hakuna kujichanganya bali inadhihirisha kuwa huwezi kuwapenda watu wawili sawasawa bali kitakachotokea ni kuuondoa kwa mmoja na kuuhamishia kwa mwingine
 
mi nafikiri unachanganya tamaa na upendo...huko nje wanaongozwa na tamaa na hawaendi kupenda au kugawanya upendo.....ila upendo utabaki kuwa kwa yule mmoja ambaye moyo umeridhia zaidi na si mwili na matamanio yake....:rain:
 
mi nafikiri unachanganya tamaa na upendo...huko nje wanaongozwa na tamaa na hawaendi kupenda au kugawanya upendo.....ila upendo utabaki kuwa kwa yule mmoja ambaye moyo umeridhia zaidi na si mwili na matamanio yake....:rain:

Uko sawa kabisa mpendwa. Ila je wale wanafunga ndoa na wake zaid ya mmoja inakuaje?
 
mi nafikiri unachanganya tamaa na upendo...huko nje wanaongozwa na tamaa na hawaendi kupenda au kugawanya upendo.....ila upendo utabaki kuwa kwa yule mmoja ambaye moyo umeridhia zaidi na si mwili na matamanio yake....:rain:

Kweli kabisa Michelle hapa ndo watu wanapopotoka kwani wanashindwa kutofautisha kati ya tamaa na upendo!!!
 
Uko sawa kabisa mpendwa. Ila je wale wanafunga ndoa na wake zaid ya mmoja inakuaje?

nafikiri ni kukidhi haja za mwili na kutafuta satisfaction ya matamanio ya moyo.....ila nachelea kuamini kuwa kuna upendo unagawanywa....pale inatumika hekima,busara na uwajibikaji tu wa wanandoa wote ila yawezekana anapendwa mmoja .....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom