Need ushauri

Need ushauri

wapendwa nepatashefa kutoka nchi za jirani ana malove makubwa na anataka tuwepamoja ilaana watoto ambao amezaa na wanawake tofauti na wa mwisho wame devorce though huwa anawapeleka watu kwa huyo mke ambaye ana mtoto naye w miaka 3. anataka nikaishi naye na kufunga ndoanchoni kwao sasa nishaidieni mawauo hapo
Mdada sikukatishi tamaa ila unayo nafasi ya kujiuliza kama ameweza kuzaa na wanawake kadhaa na hata kuoa halafu akaachika, sasa wewe utakuwa na kitu gani kipya ambacho utakuwa umekwenda nacho zaidi ya hao waliotangulia? La zaidi ni kwanini baada ya kufanya vurugu huko atokako aamue kuja huku ambapo ni mbali na kwao? Na mwisho, ni kitu gani kimekuvutia wewe hadi umuone ni Golden boy, au kwa kuwa na cv ya kuwa anatoka nje ya mipaka ya tz?! tafakali.
 
Muulize Kongosho zombie lake ilimfanyaje??
Nahisi huu ni MSIMU wa mizombie kuchangamka..mwisho wa mwaka kaka!!

katika jambo ambalo limenifurahisha mwishoni mwa mwaka huu JF ni hili isee !chezeya zombie la konnie wewe!na walahi lazima limuweke ndani!mi nimeomba udada wa hiari kwa hili kubwa la maadui!ili nilipeleke tu kwa maama Kongosho lol!
 
Last edited by a moderator:
Basi ngoja mie nilale pacha naona watoto wa siku ..yaani mapaka ISIDINGO iishe..ni leo???
ah we lala tu mi nabaki humu mpka usiku mpaka Boflo aniambie nikalale!na sijui yu wapi simuoni ati!
 
Last edited by a moderator:
huyo mtasha wako anajua kama huwezi kuandika vizuri,au umeshampa ile kitu ya 0713 kwa?
 
Mzungu! na lugha yenyewe matata si itakuwa ishtighala.
ni mtu wa west africa not mkongo.
 
Aksante sana miwatamu
shauri hizo ndio nazitaka ili na mm nitafakari

Huyu mtu anakaa huko huko kwao na tumekutana kikazi .
 
mhhhhhhhhhhh...........west africa ni nchi mama leta utaifa au hata kabila lake tujue!!!!
 
Dada shumbe mtu akiyakwepesha maji kwenye mkondo wake ni kwa muda tu, yatatafuta ile njia yake then utaambiwa uyapishe maji kwenye sehemu yake hata kama yalikwepeshwa kwa miaka mingi, usipoyapisha yatajietengezea njia yake yenyewe hapo hapo,

Huyu bwana yaelekea ndio zake, maana umesema amezaa na wanawake tofautitofauti, then wa mwisho kampa talaka, so kukupenda isiwe kigezo cha kwanza wewe kukiangalia, maana hao aliowapa talaka aliwapenda sana hadi kufikia kufunga nao ndoa. Yafaa ujitahidi sana kumchunguza na ujue kwa nini hao alitengana nao na wewe hutakuwa na sababu kama za hao walioachwa????

Jifunze pia kama yeye ndio havumiliki au hao ndio hawakuvumilika? Je utaweza kuvaa viatu vilivyoachwa kwa ufanisi ili kudumisha hio ndoa kama kweli itakuwepo? na mengine mengi kadri wakuu hapa watakavyozidi kukushauri, Kila la heri
 
Thank you sana @ Tized yaani unazidi kunifumbua macho mdau.
Nifaamuvyo mm ni kwamba alikuwa na mwanamke huko kwao na kuzaa naye and then akshama nchi kutafuta maisha. katika hiyo nchi aliyokuwapo akapata mwanamke na kuzaa naye lkn onavyoonekana huyo dada ni kijana na ametanguliza sana starehe ns matumizi ya pesa yasiyokuwa na tija.
yeye anavyosema ni kwamba aliwahi sana mambo ya familia wakati hakuwa tayari so ameshindwa kuwa mume na baba mzuri kwenye familia .
ana miaka 44 . na mtoto wake wa kwanza ana miaka 16 yupo naye anasoma boarding, wa pili anakaa kwa msms yake na kusoma huko huwa anaenda wakati wa likizo and wa tatu ni kisichana kidogo tu kinamiaka 3 na kinakaa na msms yake .
 
ha ha ha, tangia siku ile nimelichunia
ila ngoja nilitumia sms ya kwenda kanisani maana lenyewe huwa halisahau.

Muulize Kongosho zombie lake ilimfanyaje??
Nahisi huu ni MSIMU wa mizombie kuchangamka..mwisho wa mwaka kaka!!
 
Last edited by a moderator:
he he he, na kuhangaika kote huku
unadhani kuna ndoa kwa Mghana ama Mnaija?

Umeliwa parefu, ni waongo wa mapenzi hao na wanapenda K kama hewa.

Mzungu! na lugha yenyewe matata si itakuwa ishtighala.
ni mtu wa west africa not mkongo.
 
Karibu sana, Japo sina hakina sana na sababu zake eti aliwahi sana familia, wakati akipata mtoto wa kwanza alikua na 28 years (44 -16) na wa tatu akiwa na 41 years ambapo ni juzi juzi tu apo. Bado alikua amewahi? Labda kuna mengine, sijui! Tuyaache hayo.

Dada Shumbe tafuta muda wako mzuri wa kujitafakari mwenyewe, uangalie nini malengo yako, kwa nini unataka uolewe, kama uko tayari kuwalea watoto ambao sio wako ie watoto wa kambo (maana ukiwatesa watoto wa kambo, wa kwako mwenyewe huwa hawabaki salama hata kidogo), Japo sijui umri wako, lakini mnajiona mkizeeka pamoja na huyu? (Hahaaa, Usije ukawa mjane ukiwa bado kijana mbichi japo hatuombei hayo) wazazi wazazi wako wanalipokeaje n.k n.k.

Kuolewa kwa maana ya bahati hutokea kwa aina ya mume/mke uliempata kwamba mme -match sana karibia mambo yote. Ila kuolewa kwa maana ya kupata mke au mume sio bahati maana ndoa ni mpango wa Mungu watu waoane, kwa hiyo fikiria kwa makini sana juu ya uamuzi utakao uchukua. ''kupanga ni kuchagua'' Asante.
 
@ kongosho huyo si Mghana wala Mnija ni Mzim.
 
kwa kweli nashukuru sana @ Tized unanipa maneno ya heka na faraja sana.
kiukweli hata mm nimempenda pamoj na hayo .
mm ninakaribia miaka 38 na wanaume wa kibongo wamenilaghai sana . yaani sitaki kuwasikia. yule mtu sio mzuri ila ana charisma, mchapa kazi na ana akili sana what is matters to me
 
si unajua elimu yetu ya kanumba ndugu yangu. hatujasoma international skul

hakyaMUNGU wewe ni tatizo sasa hapo ni kanumba au kayumba? na uolewe ili ukaojiongezee matatizo zaid.....
 
Back
Top Bottom