Injinia
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 849
- 26
Nimekuta hii habari kwenye gazeti la Mwananchi. Habari yenyewe ni ndefu kidogo hivyo nimefupisha na kusisitiza mambo muhimu.
Hivi kwa nini NEC/ CCM wanatabia ya kupuuza maoni yoyote ambayo yanaitakia mema nchi? Huyu mzee ni wa kusikilizwa kwani na yeye aliwahi kuwa sehemu ya serikali na ana uzoefu wa muda mrefu.
Angeongeza pia na sababu ya kutokuongeza majimbo kuwa hii: hakuna pesa za kulipa mishahara ya mamilioni ya hao wabunge wa ziada!
UGAWAJI WA MAJIMBO NI SUALA LA KIKATIBA
James Magai na Hussein Kauli
TUME ya Taifa ya Uchaguzi imesisitiza kuwa itaendelea kuongeza idadi ya majimbo ya uchaguzi kwa kuwa hilo ni suala la kikatiba.
Kauli hiyo ya NEC inapinga maoani ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mstaafu, Jaji Mark Bomani aliyoitoa katika waraka wake kwenda kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake akielezea udhaifu katika nfumo wa sasa wa uchaguzi kwamba unachagia kuwepo kwa vitendo vya rushwa.
Ndani ya waraka huo, pamoja na kuelezea faida na athari za mfumo wa uchaguzi ambao ni mfumo wa majimbo pia alipinga hatua ya serikali ya kuongeza idadi ya majimbo kwa kutumia kigezo cha idadi ya watu katika majimbo husika.
Akizungumza na Mwananchi jijini jana baada ya mkutano kati yake na viongozi wa vyama vya siasa ngazi ya mkoa jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Nec, Jaji Omar Makungu alisisitiza Katiba inatutaka kila baada ya miaka 10 kuangalia mipaka ya majimbo na kuona kama kuna mahitaji ya kuongeza idadi ya majimbo au la. Tunavyo vigezo 13 ambavyo tunaviangalia kabla ya kuongeza majimbo, kama majimbo yatakizi vigezo hivyo, basi tutaongeza kulingana na maombi yaliyowasilishwa kwetu.
Alisema moja ya vigezo hivyo, ni ukumbi wa Bunge kuweza kuhimili idadi husika ya wabunge.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Uratibu wa Bunge), Philip Marmo aliwahi kutoa tahadhari kuhusu shinikizo la kuongezwa majimbo kwa madai kwamba nafasi katika ukumbi wa bunge mjini Dodoma zimejaa.
Jaji Bomani alisisitiza hakuna ulazima wowote wa kuongeza idadi ya majimbo ya uchaguzi kila kukicha kwa kisingizio cha kuongezeka kwa idadi ya watu na kueleza kuwa miaka ya nyuma wilaya nzima ilikuwa na jimbo moja tu la uchaguzi na uwakilishi ulikuwa wa kuridhisha.
"Marekani yenye wakazi 300 milioni ina wabunge (House of Representatives) 435, na wastani wa wakazi ni zaidi ya 700,000 kila mbunge. Uwakilishi mzuri si wingi wa wawakilishi.
Kuhusu mfumo mzima wa uchaguzi wa sasa ambao ni wa majimbo alisema una faida kwa wapiga kura kwa kuwa wanapata nafasi ya kumchagua kiongozi wanayemtaka, lakini pia akasema mfumo huo hutumia gharama kubwa na kuchochea rushwa na ufisadi kwa jumla.
Hivi kwa nini NEC/ CCM wanatabia ya kupuuza maoni yoyote ambayo yanaitakia mema nchi? Huyu mzee ni wa kusikilizwa kwani na yeye aliwahi kuwa sehemu ya serikali na ana uzoefu wa muda mrefu.
Angeongeza pia na sababu ya kutokuongeza majimbo kuwa hii: hakuna pesa za kulipa mishahara ya mamilioni ya hao wabunge wa ziada!
UGAWAJI WA MAJIMBO NI SUALA LA KIKATIBA
James Magai na Hussein Kauli
TUME ya Taifa ya Uchaguzi imesisitiza kuwa itaendelea kuongeza idadi ya majimbo ya uchaguzi kwa kuwa hilo ni suala la kikatiba.
Kauli hiyo ya NEC inapinga maoani ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mstaafu, Jaji Mark Bomani aliyoitoa katika waraka wake kwenda kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake akielezea udhaifu katika nfumo wa sasa wa uchaguzi kwamba unachagia kuwepo kwa vitendo vya rushwa.
Ndani ya waraka huo, pamoja na kuelezea faida na athari za mfumo wa uchaguzi ambao ni mfumo wa majimbo pia alipinga hatua ya serikali ya kuongeza idadi ya majimbo kwa kutumia kigezo cha idadi ya watu katika majimbo husika.
Akizungumza na Mwananchi jijini jana baada ya mkutano kati yake na viongozi wa vyama vya siasa ngazi ya mkoa jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Nec, Jaji Omar Makungu alisisitiza Katiba inatutaka kila baada ya miaka 10 kuangalia mipaka ya majimbo na kuona kama kuna mahitaji ya kuongeza idadi ya majimbo au la. Tunavyo vigezo 13 ambavyo tunaviangalia kabla ya kuongeza majimbo, kama majimbo yatakizi vigezo hivyo, basi tutaongeza kulingana na maombi yaliyowasilishwa kwetu.
Alisema moja ya vigezo hivyo, ni ukumbi wa Bunge kuweza kuhimili idadi husika ya wabunge.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Uratibu wa Bunge), Philip Marmo aliwahi kutoa tahadhari kuhusu shinikizo la kuongezwa majimbo kwa madai kwamba nafasi katika ukumbi wa bunge mjini Dodoma zimejaa.
Jaji Bomani alisisitiza hakuna ulazima wowote wa kuongeza idadi ya majimbo ya uchaguzi kila kukicha kwa kisingizio cha kuongezeka kwa idadi ya watu na kueleza kuwa miaka ya nyuma wilaya nzima ilikuwa na jimbo moja tu la uchaguzi na uwakilishi ulikuwa wa kuridhisha.
"Marekani yenye wakazi 300 milioni ina wabunge (House of Representatives) 435, na wastani wa wakazi ni zaidi ya 700,000 kila mbunge. Uwakilishi mzuri si wingi wa wawakilishi.
Kuhusu mfumo mzima wa uchaguzi wa sasa ambao ni wa majimbo alisema una faida kwa wapiga kura kwa kuwa wanapata nafasi ya kumchagua kiongozi wanayemtaka, lakini pia akasema mfumo huo hutumia gharama kubwa na kuchochea rushwa na ufisadi kwa jumla.