NEC: Tuwatumie Viongozi wa Dini katika Uchaguzi

NEC: Tuwatumie Viongozi wa Dini katika Uchaguzi

Mhoja

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2010
Posts
207
Reaction score
24
Napenda kuishauri Time ya Uchaguzi iwatumie Viongozi wa Dini katika kusimamia zoezi la uchaguzi siku ya Jumapili. Kwa haya malumbano yanayoendelea ya kukaa mita 200 kutoka kwenye kituo au kwenda nyumbani baada ya kupiga kura yanaweza yakaisha.

Naamini kila eneo lina Viongozi wa Dini kama vile Shehe, Imam, Ustadhi, Padre, Mchungaji, Katekista, Mwinjilisti, Nabii au Mtume. Uwepo wa Viongozi hawa utawafanya wapiga kura wawe na Imani na usalama wa kura zao.

Si vema tukasubiri mambo yaharibike ndiyo tukawatumia Viongozi wa Dini kupatanisha au kuombea amani irejee tena. Muda bado unatosha kuwaomba Viongozi wa Dini waweze kusaidia, maana wapiga kura wengi naona hawana imani na Mawakala.

Mungu ibariki Tanzania!!!!!
 
Viongozi Gani Gwajima??
Kumbuka Mkuu Hata Hao Viongozi Wa Dini Nao Wanamapenzi Na Mtu Fulani Na Chama Fulani Kama Binadamu Wengine Tu...Tena Hao Kuhusishwa Kwao Ndo Kutakua Kitu Kibaya Zaidi Kuwahi Kutokea,utaongeza Matatizo Zaidi...
 
Napenda kuishauri Time ya Uchaguzi iwatumie Viongozi wa Dini katika kusimamia zoezi la uchaguzi siku ya Jumapili. Kwa haya malumbano yanayoendelea ya kukaa mita 200 kutoka kwenye kituo au kwenda nyumbani baada ya kupiga kura yanaweza yakaisha.
Naamini kila eneo lina Viongozi wa Dini kama vile Shehe, Imam, Ustadhi, Padre, Mchungaji, Katekista, Mwinjilisti, Nabii au Mtume. Uwepo wa Viongozi hawa utawafanya wapiga kura wawe na Imani na usalama wa kura zao. Si vema tukasubiri mambo yaharibike ndiyo tukawatumia Viongozi wa Dini kupatanisha au kuombea amani irejee tena. Muda bado unatosha kuwaomba Viongozi wa Dini waweze kusaidia, maana wapiga kura wengi naona hawana imani na Mawakala.
Mungu ibariki Tanzania!!!!!



Uko sahihi.
Tatizo ni ubabe unaotumiwa na wakirugenzi na wasimamizi wanazuia mtokeo ya maeneo yale ambayo C C m haina chake.
Ni muda mrefu matokeo hayasomwi kwa hiyari mpaka wananchi waandamane kwa fujo.
Wakurugenzi wanakua wakiharibu uchaguzi kwa kushirikiana na wasimamizi lakini hawachukuliwi hatua na serikali badala yake wananchi ndio wanauawa kwa maslahi ya chama kimoja.
Kwa ushauri wangu ukawa itumie mawakala wachamungu ili wakatae hila na kununuliwa na wajanja wa CCM wanaongangania uongozi kwa kutumia hila na vitisho.
 
Back
Top Bottom