NEC: Kauli kinzani za NEC zinaonesha taasisi hiyo kuchanganyikiwa kabla ya uchaguzi

Kamundu mngoko

JF-Expert Member
Jun 10, 2015
231
23
Katika hali isiyo ya kawaida NEC imetoa taarifa zinazokinzana kuhusu mita 200 ndani ya siku mbili mfululizo yani jana na leo.

Katika taarifa ya habari ya ITV ya saa mbili usiku jana tarehe 18, Oktoba Jaji Damiani Lubuva alitoa ufafanuzi kuwa wakati wa muda wa upigaji kura kumalizika wananchi wataweza kusubiri matokeo yao umbali wa mita 200, lakini hawataruhusiwa kusubiri matokeo hayo kabla ya muda wa wa upigaji kura kumalizika.

Leo tarehe19, Oktoba kwenye taarifa ya habari ya ITV ya saa mbili usiku kamishna wa NEC akiongea kutoka Mtwara amesema baada ya kupiga Kura watu waende kwao, je tuamini kauli ya nani katika tume, kama tume imeshachanganyikiwa hata kabla ya uchaguzi, tunaiomba mahakama itoe tafsiri ya sheria husika, kwa sababu jambo hili lisiposhugulikiwa lina kila dalili ya kuleta machafuko ikiwa polisi watakubali kutumika ovyo na Serikali.
 
ninavyojua hili jambo la mita 200 litapatiwa ufumbuzi!shida yangu ni kujiuma uma kwa n.e.c!why?
 
Lubuva si tatizo ndani ya NEC tatizo ni mkurugenzi wa NEC na kamishna wake.
 
Nikiangalli hali inavyo kwenda ndani ya NEC namkumbuka Marehemu Kivaitu aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya Kenya. Kwenye kitabu kinacho itwa IT IS OUR TURN TO EAT NOW, Kivaitu anasema alipoteza kabisa mamlaka ya kuiongoza Tume mara baada ya Mwai Kibaki kuteuwa makamishna mapya wa Tume. Hawa Makamishna waliletwa kwenye Tume kwa Kazi maalum. Alipokuwa akiitisha vikao mara zote walimwambia ...WE KNOW WHAT WE ARE DOING ans WE ARE HERE FOR PURPOSE. Hii hali ali ripoti kwa balozi wa Marekani akitegemea kupata msaada kwani uchaguzi huo uligharamikiwa kwa sehemu kubwa sana na Marekani but it was in Vain.

Hivyo hao makamishna wa tume yetu ambao wengine wameteuliwa hivi karibuni...THEY KNOW WHAT THEY ARE DOING aand THEY ARE THEIR FOR PURPOSE
 
Back
Top Bottom