Ndugu zangu Wahayanhii bado ipo??

client3

JF-Expert Member
Aug 6, 2007
2,332
3,152
Nilibahatika kuishi mkoani Kagera miaka ya themanini,kwa wahaya kuna ndoa zile za lazima yaani kijana anamwinda dada mahali halafu anamkamata akiwa na vijana wenzie, kisha anampeleka kwake,yule dada akishalala kwa usiku mmoja tu nyumbani kwa kijana kwa jadi ya kihaya huyu tayari ni mkewe. sasa kwa vile nilikuwa mtoto sikuwahi kuuliza haya maswali yangu,naomba wahaya mnisaidie
1. je na mdada alikuwa akijua kuwa anakaribia kubebwa?
2. nini maana yake maana wengi wao walikuwa ndani ya maandalizi ya kuwaoa haohao lakini ghafla anakatisha anambeba mdada hii sikuwa naelewa kabisa maana yake.
3. je ndoa hizi zilikuwa zinadumu?
4. je hii jadi ipo mpaka leo na nini maana yake?
 
ngoja nitarudi baadae kidogo naenda kumuita Bishanga kwanza tukufanyie kidogo kakikao
 
Muda wote huo takriban miaka zaidi ya 30 ulikuwa unasubiri nini hadi leo hii, umeamua kuuliza swali hili?
Demu wako alibebwa au...? Umemkumbuka?
 
Hizo hata usukumani zipo. It is a calculated movie. Wanajuana sana. Usidhani ni kamata kamata tu. Na hii inafanyika sana kama wazazi wanaleta kauzibe
 
Ndo mama zetu na ndo wake zetu leo hii na bado maisha ya ndoa mwendo nchibuyu tofauti na hizi za .com za kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa

Karibu Kagera,onyegele nakanyeto.
 
Tamaduni nyingine zitakuwa zipo ila nyingine zitakuwa zimebadilika kuendana na utandaopen wa sasa.
 
Ndo mama zetu na ndo wake zetu leo hii na bado maisha ya ndoa mwendo nchibuyu tofauti na hizi za .com za kupakana mafuta kwa mgongo wa chupa

Karibu Kagera,onyegele nakanyeto.

leka aije. nijakumchwekeza. mia
 
Back
Top Bottom