Ndugu zangu sio kila kinachonga'aa ni dhahabu majuu sio mchezo

Le mutuz kwa umbo na umri wewe ni mkubwa na ni mtu mzima haswa! Lakini kwa akili wewe ni mtoto mdogo na hata darasa tano hujafika..una akili za kitoto sana haiyumkini hata hao watoto wadogo unaopoga nao picha wanakung'ong'a!you are too shallow...inasikitisha sana tavitafuta hivyo vyuo vilikupa hizo degree ninue credibility zake..aibu!

Kwani huyu unayemreply ni le mutuz.??
 
hivi huyu le manyonyoz na mbuta nanga wana tofauti kweli???wote wanamiliki blog pia, labda tofauti ni mbuta nanga ni mtoto wa kichaga wa milimani na le manyonyoz mtoto wa mchepuko wa ex prime minister...but all in all wamefanania sana na ndo maana walitongozana wakapishana maneno...big up le manyonyoz na mbuta nanga!!!mko juu.
 
- Nilitumia muda mwingi kwenda Shule so between Shule na kazini I had no time ya kutaabika kwa sababu I was always busy with purpose unajua madhara ni kuwa busy with no purpose au kutokuwa busy maana sio oazi zote zinaruhusu overtime kwa hiyo kama huna kazi ya overtime utaishia kukaa home kuangalia TV asubuhi mpaka jioni weekend nzima!!, it never happen to me kwa sababu I was laways busy!!

Le Mutuz

10568995_10152611400578620_6265867876734145634_n.jpg
 
Hata iweje,majuu bado ni bora kuliko bongo,kodi wanayolipa inaonekana kwenye maendeleo na nyingine wanasaidia wajinga wa africa,hapa bongo hata ulipeje kodi bado nchi imechoka tu,so majuu ni bora sana,hapa ma expat wanafanyakazi hata kodi hawalipi,kazi ya magamba ni kuonea machinga tu,hapa dhahabu na wanyama pori wanatoroshwa kwenda nje nasi kubaki maskini,kwa point zote,majuu patabaki kuwa ni bora tu,hapa bongo hata kazi ya kuchimba choo ni ngumu kuipata,bongo ni kuzimu,kuna dhiki za kijinga sana hapa,so usijaribu kuifagilia bongo na kuponda majuu.
 
Mara Nyingi nikiona Le Mutuz big Show nafurahi kwakuwa Huyu jamaa mzima mkononi na mdomoni pia #Le Mu2 safiiiii
acha wajigonge
 
Uko sawa kabisa kiongozi.. Bora nirudi nifagie barabara za home watanienzi hata kwa jina la'Baba Mafagio' kuliko kuendelea kuwa mwehu kwa wazungu.. Nyumbani ni nyumbani tu bandugu, kwa wazungu sahau. Watakutumia at the end of the day watakutupa jalalani, hakuna future kabisa mimi ni muathirika mmojawao... Kwani nini bana, mbona Le Mutuz ameweza home after 30 yrs ya msoto! NARUDI HOME

Rudi aisee.
 
Hahaha,mkuu Le mutuz umenifurahisha sana,et mtu anakuja mtandaoni na kuanza kutukana serikali,duh
 
PUMBAF ZENU HAMNA PASSPORT, MTAZIPATA WAPI?

KIINGE CHA MALKIA HAMJUI, UTHUBUTU HAMNA, WAOGA TU NYIE. NYAMBAF KUFENI HUKOHUKO MSIJE KUJAZA NZI HUKU. SISI NDO ZETU KUJIRUSHA KWA KUBAGULIWA TUNAYAWEZA.

NIKIJA HUKO NAKUJA NIMEVAA KANDA MBILI, NA BUKTA CHAFUUUU, MKATE TAMAA UZURI, ILI MNIBAGUE VIZURI, HALAFU NITUMIE KWA NAFASI DOLA ZANGU.
 
Yaani hata hiyo elimu uliyopata nahisi haijakusaidia lolote katika maisha yako. kwa maana ipi , moja huwezi kukaa eneo moja kisha , ukatoa taarifa kwa ujumla I mean we umeka NY then unatoa taarifa ya nchi nzima.
pili ,unaposema ulaya unamaanisha nchi nyingi(bara) na kila nchi ina sheria zake.
Yaani naona umeshindwa kujua tatizo ni nini kisha ukakurupukia solution yake.
kwa nchi kama marekani ,nahisi sheria zao unazijua na tartibu za kwenda pale ,so sifikirii kuwa mtu anaweza kwenda ishi pale bili kuwa na acc inayoeleweka.

Kupunguza maneno we sema ulikuwa mpenda mademu na casino, ndicho kikubwa ulichojifunza pale, na hadi leo hii ndio tabia zako, ulichokisoma hata application yake sijawahi kuiona. zaidi zaidi umekuja kuongeza matatizo tu bongo.

namalizia kwa kusema to travel is to learn.
jitahidi kuishughulisha akili yako kufikiri.
Nyanyado ntakupenda maisha yangu yote baby. umeolewa?
 
- ha! ha! ha! maneno mengi hewa tupu kaka nimekusoma ulichofanya kuongea uswahili uswahili na kutumia sana jina langu lakini nothing serious, zaidi tu ya maneno mengi yasiyokuwa na hoja kaka ukitaka kucheza na mimi on a serious note ongea hoja.

1. On me nimekaa Majuu 30 years, Nimejisomesha Degree 3, nimejenga nyumba kwenye shamba langu la eka 5 Kinyerezi, nimeondoka huko nikiwa eligible for Pesheni soon nitaanza kuipokea mpaka ninakufa, nimelifanyia kazi shirika moja tu miaka yote 25 niliyokaaa US kwa hiyo U know my pesheni itakuwa Super at least usd $2,000 kila mwezi ambazo zitaingia kwenye account yangu kila mwezi kama sheria ya US inavyosema, nimerudi sasa nimeanzisha blog ambayo sasa ni Kampuni kubwa ina ofisi zake na wafanyakazi 3, na nimeashachana nayo nipo Mbagala kwenye ICD na pia soon ninaelekea kufungua Radio na TV, sasa kweli mkuu unaweza kuniambia with your right mind kwamba nisingeenda Majuu ningekuwa na akili hizi zote, au unataka kuniambia Tanzania kuna wabongo wengi wenye mafanikio ya maisha kama yangu baada ya kwenda majuu miaka 30?

2. Umeongelea utafiiti sijui ni utafiiti gani unaousema ambao umekosekana kwenye my post, nimeongelea ukweli wa wale wote wanaokwenda US kama wakimbizi wa uchumi sijawazungumzia waliokwenda kusomeshwa na Serikali, sijazungumzia waliokwenda kikazi, lakini hata wewe unajua hao ni wachache sana huko, inapofanyika sherehe mji kama New York ya wabongo, niambie kuna madakitari wangapi wanakuwepo kama sio mmoja tu au wawili? I mean wewe umeandika kunishambulia mimi binafsi bila facts zaidi ya kuokota kuokota ujinga ujinga humu kwenye mitandao, zile picha ninazopiga ambazo wewe huzipendi na unaziiita utoto ndio zinafanya blog yangu kuwa namba one na kuingiza pesa nyingi ambazo zinaishia kuwaajiri vijana nilionao, vipi wewe kutokupiga picha na mebebz kunakuingizia pesa? ha! ha! ha!

- Kaka ukweli ni kwamba huna hoja, wewe unaongelea proffesionals wanaokwenda US kwa mpangilio wa kiserikali mimi nimeongeleea wale kama mimi tuliokwenda kwa njia zetu wenyewe na wanaotaka kwenda kwa njia zao wenyewe, pole sana kaka I am fine na maisha yangu na sikushindwa huko maana mpaka leo wazungu niliowafanyia kazi wanabembeleza nirudi nimekataa kata kata jinsi ninavyipenda bongo, majuzi nilienda West Africa ilikuwa niake Wiki 2 baada ya siku 4 tu niawaomba wenyeji wangu kuwa nataka kurudi bongo maana pamoja na kuniweka the best hotel in Lagos na Accra NILIKUWA ninakumbuka misha yangu super hapa bongo, maisha ni popote ila ni muhimu kusema tuliyoyaona mimi nimeandika niliyoyaona wewe umeandika mipasho tena bila FACTS cause hunijui maana ungekuwa unaijua ungejua kwamba New York nzima hakukuwa na mbongo aliyekuwa akifanya kazi kama mimi,

- Kaka usiwadanganye wananchi waambie ukweli wa nini cha kutegemea wakija huko, ninamshukuru sana Mungu kwa kunipa nafasi ya kuja huko maana nisingekuwa akili kama niliyonayo sasa yaani ya kufikiria kwamba ninaweza kupiga picha na mabebz hizo hizo zikaniingizia Millions mfukoni, nisingekuja huko sijuii kama ningejua hata kutumia mitandao, kaka karibu sana Tanznia ukihitaji ajira niambie maana sasa ninaanza kuaajiri watu kwa ajili ya RAdio na TV tunayofungua na patner wangu nisingekuja huko haya yote nisingeweza kuyafanya ila haibadili ukweli kwamba kama nilivyosema kama upo sawa hapa bongo sio lazima kuja huko, pole sana najua una stress ya madeni kazana ndio maisha hata mimi nimepitia lakini sasa nimeamua kurudi, halafu pia inaelekea ulikuwa hujui kwamba nilishaenda Ulaya nikakaa halafu nikaurid bongo na kujenga nyumba halafu nikaondoka tena so mimi ni mzoefu wa huko ksana mkuu, pole sana lakini ninaamini nimekusaidia kama bado nitarudi tena sema sema wasap!! ha1 ha! ha1

Le Mutuz
HUNA maana unapiga politics km za babako
 
Hahaha
Mbwembwe nyingi sana lakini hakuna kitu.

Ndio maana hata vibanda hapa bongo hawana.

Mm demu wangu alinishawishi sana nimfuate huko Kwa Obama nikagoma.

Hapa bongo Nina chance ya kuwa president, lakini huko hata Mkiti wa mtaa siwezi Pata.
 
Nimeelewa kwanini dada wa taifa yule kimbaumbau wa majuu yupo bize kutukana serikali na watu wenye uwezo kifedha. Kumbe mitandaoni ndio kwa kutolea uchungu wao wanashinda kutukana watu.
 
- Leo naomba mnipe nafasi nijaribu kuwasaidia baadhi ya ndugu zangu Wabongo ambao hawajafika Majuu na wanaota kufika huko, kwenda kutafuta maisha maana wanaamini kule ni Paradise.

Binafsi nilikuwa na hiyo ndoto nikaitimiza na kujionea mwenyewe na nikajifunza kwamba sio kila kinachong'aa ni dhahabu. I was once a believer of that theory kwamba Majuu ndio kila kitu mpaka nilipofika huko na kujionea mwenyewe kwa macho yangu baada ya kuishi huko miaka 30.

- Kwanza ukifika tu kama nilivyokwenda New York City/USA wabongo wenzako hata unaowajua wanakukimbia maana hawawezi kukusaidia, tatizo la kwanza makaratasi ya kukuwezesha kufanya kazi tena kazi ambazo kwenye maisha yako hapa bongo hukutegemea kuzifanya infact ni kwa mara ya kwanza nikaona Singa singa anafanya kazi kituo cha mafuta sikutegmea kuona hayo hata siku moja.

Huna makaratasi na huna pa kukaa kama umeenda kama nilivyokwenda mwenyewe kivyako vyako, itakuchukua miezi kama 6 ya kusota sana ndio uweze kupata ID na Card ili uweze kupata kazi angalau ya kulea wazee au matahira.

- So kwa mara ya kwanza katika maisha yako unakutana na kitu kinaitwa Kodi, au taxes maana hapa bongo tunacheza cheza tu na kodi kule ni serious ishu, panga pangua huwezi kupata mshahara unaozidi Dola 500 za kimarekani kwa wiki kati ya hizo watakukata angalau 100 za kodi so utabaki na 400 tu chumba 150 kwa wiki, nauli ka kwenda na kurudi kazini, halafu unagundua ili upate hgela extra ni lazima ufanye kazi masaaa mengi, so kwa mara ya kwanza unajifunza kuishi kazini maisha yako yanakuwa ni kazini tu,

- Wazungu wana akili sana System yao wameitengeza makusudi kwamba mtu kama wewe mbongo ukienda unaichangia Uchumi wao tu, uwezekano wa wewe kuwa tajiri kwa kufanya biashara kule haupo kabisa unless uuze madawa ya kulevya, ninasema tena uwezekano wa wewe mbongo kutajirika

Majuu ni haupo kabisa labda ujiunge na kuuza madawa ambayo haitachukua muda mrefu watakushika unajua kwa nini watakushika ni kwa sababu Polisi wa majuu wana akili sana wanajua kwamba hawawezi kuzuia kabisa kuuzwa madawa ya kulevya kwa sababu moja kubwa sana nayo ni Law Enforcement ya kuzuia drugs inaajiri karibu wananchi Millioni 2 wa taifa lao.

Sasa ukizuia madawa ina maana hawa hawatakuwa na kazi kwa hiyo wanavyojifanya wanazuia madawa ni waongo sana nalijua hili kutokana na kusoma Criminology nchini kwao, so wanachofanya ni kwamba kwa mfano Mjini New York.

Polisi wameugawa mji mzima kwa vipande vipande na kukata maeneo ya wauza drugs, wanaowajua one on one lakini hawawashiki hata siku kwa sharti moja tu kwamba wasiue au wasuze ile drugs ya kujipiga sindano, kwa hiyo any crime ikitokea kwenye lile eneo polisi wanamfuata muuza drugs mkubwa pale waliomkabidhi eneo ambaye siku zote ana wafanyakazi wengi mtaani kwa hiyo anajua nani amefanya anawaambia.

Polisi mara moja unashikwa, sasa wewe mbongo kwa vile hujui hii system unajiingaiza na kuanza kuuza drugs, mwenye eneo anakujua mara moja na kuwashitua Polisi ndio mwisho wako na Polisi wa Majuu hawana haraka wanaweza kukuwinda hata mwaka mzima nia na madhumuni yao kukamata system yako nzima na watakushika tu.

- Biashara ya halali huwezi kwa sababu kwanza huna capital ya kutosha na besides Wazungu wameshazoeshwa majina makubwa so siku zote wananunua kwenye maduka yenye majina makubwa, pili kodi ni kali sana huwezi kabisa maana kwenye kulipia kodi utashindwa tu so wabongo wengi majuu wanaojifanya kufanya biashara ninasema ni waongo sana always wana biashara nyingine kuliko wanayoionyesha.

- So huna choice ila kufanya kazi tu kama mbwa, ukitoka kazini ni kulala tu na kukaa ndani ya nyumba kuangalia TV hela huna mpaka mwisho wa wiki ukilipwa Wazungu wajanja sana wanakulipa kila mwisho wiki kusudi uweze kuzitumia hela zote by jumatatu ndivyo uchumi wao unavyosimama imara.

Wazungu wanajua kuwa hela wanazokulipa mshahara hazitoshi kwa hiyo wamekutengenezea system ya Credit Card yaani unapewa Card bila masharti magumu ukope, kufumba na kufumbua una madeni kuliko uwezo wako, hatimaye wanakufikisha mahali unakuwa unalipa madeni yako on interest tu bila kugusa deni lenyewe hasa deni linaendelea kuwa kubwa mpaka mwisho maisha yako ni madeni tu,

- Huku home ndugu na jamaa wanakuaminia kwamba sasa upo vizuri kumbe sio kabisa, kutuma hela huwezi wewe mwenyewe huna hela extra maana ile system haikupi hiyo nafasi, so Rafiki yako wa bongo akija unamkimbia maana huna hela extra ya kumsaidia unajificha mpaka usikie amekuwa sawa ndio unajitokeza na kujifanya kumjua sana na kwamba ulikuwa umesafiri, ndugu yako akija unamkimbia maana huwezi kumsaidia hatimaye unakata mawasiliano na home bongo maana huna pesa.

Pole pole unaanza kuwa kama Wazungu ukitembea unaongea mwenyewe kudadeki madeni yamekukaba mpaka shingoni, zamani ilikuwa rahisi ukizidiwa madeni unaenda Mahakamani una-file kufilisika wanakusamehe siku hizi hamna tena hiyo mpaka ulipe tu.

- Sasa unaanza kukumbuka bongo, hapa ulikuwa na kazi nzuri ulikuwa unaweza kula mara tatu kwa siku unaweza kwenda bar kunywa kidogo, unaweza kwenda uwanja wa Taifa kuona mipira mikubwa.

Majuu forget it it will never happen huwezi so huna pa kwenda matokeo yake mbongo mmoja akifanya party ya birthday hata ya mtoto mchanga wote mnakimbilia huko watuwazima unakuta mmejaa nyumbani kwa mbongo, kijumba kidogo mnabanana humo humo na kuanza kupiga picha za kutuma bongo kuwakoga wajinga kwamba upo majuu.

Pale kwenye party inatakiwa uwe very careful kwenye kupiga picha unatafuta angle ya kuonyesha upo kwenye bonge la nyumba kumbe mazishi matupu, umevaa nguo za kukopa dukani kwa credit card, kesho kazini mapema sana so hata pale kwenye party huna raha ila unajifanya kuwa furaha sana kumbe uongo mtupu madeni yamekukaba mpaka shingoni masikini wa Mungu,

- Matokeo yake unaanza kuja kwenye mitandao na kuanza kutukana Serikali ya Tanzania na Viongozi wake kisa na mkasa yamekushinda huko Majuu, na kurudi huwezi wengi wao wanaanza ku-develop tabia za ajabu na kutisha sana kisa maisha ni magumu na sivyo walivyotegemea lakini hawawezi kukubali na kusema wazi maana ni aibu.

Wazungu wametengeneza system yao ya maisha ili wanasheria na madakitari tu ndio wale bataz so wewe ukienda kule bila kusoma utachekesha tu, na uzuri wa Wazungu ni kwamba no matter what utakula tu maana kwa mfano usiku fast food zote wanatakiwa ikifika saa sita kutupa chakula kama kipo hakiruhusiwi kwenda next day kwa hiyo ukienda pale watakupa bure maana hawaruhusiwi kukitupa mpaka wahakikishe hakuna mtu anayekihitaji kwanza ni sheriaa.

- So unaanza pole pole kukumbuka bongo, furaha yako yote haipo tena Wazungu kama kawaida yao hawapendi weusi popote unapokwenda wewe ni nothing but nigga, huna thamani yoyote ni good for nothing halafu maisha majuu ni sheria asubuhi mpaka saa ya kulala!!!.........

OK GUYS KWA LEO NAOMBA NIISHIE HAPA NEXT NIKIWA NA TIME KAMA YA LEO WILL DO SOME MORE!!

Le Mutuz
Acha kuponda watu wewe mamaee, wewe unamaisha gani mazuri bongo wakati hata wakiita matajili wa mtaa unaoishi haumo kwenye listi? Kazi kupiga mi self kwenye Hotel kubwa kubwa na kujisifu wakati na wewe ni mchumia juani tu.

Njoo na kiki nyingine nikuanike hadharani.
Kama wewe ulishindwa acha wengine wafaiti. Kumbe uzee ulionao ujakusaidia lolote.
 
Miaka 30 marekani huna kitu? ....kila kitu mipango, mi nna mwaka wa kumi hapa uingereza na nipo safi alhamdulilah. ...nna mke wa kibongo na watoto wawili wote tuna vitabu vya kiingereza. ...tumesoma university kwa government loans na sasa tunafanya kazi. ...na bongo nishaomba kibali cha kufungua fm radio station na nnalimisha mchele huko morogoro. .......sio wote wanaokuja ulaya wanakuja kutaabika, wengine unaweza kuona wanataabika lkn maisha waliyokuwa nayo huko bongo ni magumu kuliko wanayoishi huku. ....kama unapata fursa ya kuja ulaya we njoo ....sasa kipi bora, kuendelea kumpiga mizinga babaako au kuja kujaribu maisha huku?.....ila ukija huku kisha karatasi zikakataa ni bora uwahi nyumbani kuliko kupoteza muda
Upo sawa mkuu, uyo alikuja kuuza sura tu huko, mbona hata bongo hapa anachochote zaidi ya kupiga picha serena hotel anakunywa chai na skonzi, hana akili uyo mlipuuze amekalia siasa uchwara tu.
 
Back
Top Bottom