denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,511
- 68,141
Salaam,
Nimeona video muda mfupi uliopita ambapo Mh. Spika Job Ndugai jana aliamua bila aibu yoyote kusimamia udhalilishwaji kwa Mbunge wa Viti Maalum Chadema Mh. Yosepher Komba aliofanyiwa na Mbunge Viti Maalum CCM, Jackline Msongozi.
Huyu Mbunge wa CCM ki umri ni sawa na mzazi kwa Mbunge wa Chadema, lakini kuamua kuzungumza aliyozungumza kuhusu tuhuma za ngono kwamba Mbunge wa Chadema nae alimlalamikia kufanyiwa, na Spika kwa nafasi yake kuacha hilo jambo litokee bungeni ni udhalilishaji mkubwa waliomfanyia Mbunge wa Chadema, iwe ni kweli wabunge hao wawili waliongea pembeni au sio kweli.
Ieleweke wazi, hili suala bado linafanyiwa uchunguzi kwenye vyombo vya usalama, sasa kwanini Mh. Spika kwa nafasi yake aache lijadiliwe bungeni? haoni huku ni kuingilia mamlaka za kiuchunguzi zinazoendelea juu ya jambo hilo?
Binafsi nashindwa kuelewa, kwanini Spika wa Bunge letu kaamua kusimamia bunge kwa kuonesha ushabiki wa kiwango cha juu namna hiyo? kufanya bunge letu la JMT kugeuka kijiwe cha umbeya na mipasho, huku akimzuia Mbunge mwanaume wa CDM alietaka kuingilia kati suala hilo kwa kumwambia mambo ya wanawake asiingilie, yaani hapa Ndugai anaona raha kusimamia mipasho inayoendelea bungeni chini ya uongozi wake kwasababu tu inazungumzwa na Mbunge wa chama chake?
Kwanini ameamua bila aibu kulinajisi bunge letu kwa kiwango hiki? Spika amefikia kiwango cha kusimamia udhalilisha wa utu ili tu kukilinda chama chake? Spika anasimamia uonevu ili tu kujifurahisha yeye binafsi na baadhi ya wabunge wa chama chake wanaopenda kuona mambo ya kijinga kama yale!
Baada ya kumfanyia uonevu huo, anawaita askari wamtoe Mbunge wa CDM nje kwa kisingizio alileta vurugu wakati akijaribu kujitetea, halafu askari wanafika na kumtoa nje tena kwa kumsukuma!.
Aibu hii kama taifa hakika itatuaibisha kwa kipindi chote ambacho Spika Ndugai ataendelea kuwa Spika wa bunge letu.
Nimeona video muda mfupi uliopita ambapo Mh. Spika Job Ndugai jana aliamua bila aibu yoyote kusimamia udhalilishwaji kwa Mbunge wa Viti Maalum Chadema Mh. Yosepher Komba aliofanyiwa na Mbunge Viti Maalum CCM, Jackline Msongozi.
Huyu Mbunge wa CCM ki umri ni sawa na mzazi kwa Mbunge wa Chadema, lakini kuamua kuzungumza aliyozungumza kuhusu tuhuma za ngono kwamba Mbunge wa Chadema nae alimlalamikia kufanyiwa, na Spika kwa nafasi yake kuacha hilo jambo litokee bungeni ni udhalilishaji mkubwa waliomfanyia Mbunge wa Chadema, iwe ni kweli wabunge hao wawili waliongea pembeni au sio kweli.
Ieleweke wazi, hili suala bado linafanyiwa uchunguzi kwenye vyombo vya usalama, sasa kwanini Mh. Spika kwa nafasi yake aache lijadiliwe bungeni? haoni huku ni kuingilia mamlaka za kiuchunguzi zinazoendelea juu ya jambo hilo?
Binafsi nashindwa kuelewa, kwanini Spika wa Bunge letu kaamua kusimamia bunge kwa kuonesha ushabiki wa kiwango cha juu namna hiyo? kufanya bunge letu la JMT kugeuka kijiwe cha umbeya na mipasho, huku akimzuia Mbunge mwanaume wa CDM alietaka kuingilia kati suala hilo kwa kumwambia mambo ya wanawake asiingilie, yaani hapa Ndugai anaona raha kusimamia mipasho inayoendelea bungeni chini ya uongozi wake kwasababu tu inazungumzwa na Mbunge wa chama chake?
Kwanini ameamua bila aibu kulinajisi bunge letu kwa kiwango hiki? Spika amefikia kiwango cha kusimamia udhalilisha wa utu ili tu kukilinda chama chake? Spika anasimamia uonevu ili tu kujifurahisha yeye binafsi na baadhi ya wabunge wa chama chake wanaopenda kuona mambo ya kijinga kama yale!
Baada ya kumfanyia uonevu huo, anawaita askari wamtoe Mbunge wa CDM nje kwa kisingizio alileta vurugu wakati akijaribu kujitetea, halafu askari wanafika na kumtoa nje tena kwa kumsukuma!.
Aibu hii kama taifa hakika itatuaibisha kwa kipindi chote ambacho Spika Ndugai ataendelea kuwa Spika wa bunge letu.