Ndoto za Kuhamia Ughaibuni....Soma hapa.

Hio story ya huyo nesi mimi pia naona ni kama hadisi tu za Abunwasi au ana matatizo kibao aliyopata hapo mbeleni na sasa inabidi alipe madeni ya kale. Kazi ya Nesi inalipa kishenzi mtu asikwambie aisee! Hao watu wanachukua kuanzia dala 30 hadi arobaini kwa saa. Sasa hebu piga hayo mahesabu kama anafanya 16hrs kwa siku baada ya taxes how much is she bringing home?Mimi nasema hivi maana mke wangu ni nesi na pia anafundisha manesi University na hela yake najua.

Sasa hebu nami nitumbukize hamsini yangu kwa wale wanaokandia maisha ya ughaibuni na kuyalinganisha na ya Bongo. Jamani hii nchi maisha ukiyapatia mambo yako yanakwenda mswano kinoma! Tatizo la wengi wetu ni kua tukitoka nyumbani tuna hadisi kibao za kudanganya watu what we are going to do in the States thereby setting our expectations to be way too high. Kisha mtu akifika huku na akipigwa na hali halisi anachanganyikiwa na kukosa mwelekeo. Mie najua watu wengi sana niliokuja nao mwaka wa 1999 ambao walikua wakiwaambia washkaji kijiweni eti wanakuja kusomea mara sijui urubani, mara udaktari mara sijui u-lawyer. Mwenzenu mimi nikawa nasema nitaangalia kama digrii yangu ya ualimu itafua dafu na sikua na mengi ya kujisifia. Kama kutakua kubaya nitarudi home maana sijaua mtu wala sikufukuzwa.

Basi nilipojimiksi huku jambo la kwanza nikachangamkia shule na kupata the basics (ID na SSN) baadae nikawatumia jamaa wa EEC digrii yangu waifanyie evaluation kisha waniambie nikowapi kulingana na standards zao. Majibu yaliporudi wakaniambia kila kitu safi naeza kuapply leseni ya kufundisha. Kipindi hicho mwenzenu nafanya kazi za kuuza dukani usiku bila noma maana I had set my goals.Kuna vijana wakibongo walikua wanakuja pale wakitoka klabu huku wamebwia na zereu zao....eti wanashangaa nafanya kazi na kuajiriwa nami nikawa siwajibu kitu maana I knew what I was doing to secure my future in this country. Basi nikafanya mitihani ya kupata leseni na mambo yakatiki na mwenzenu nikaaply katika shule kadhaa. Nilipopata majibu na kuenda interview mambo tena yakakubali na nikapata kazi katika shule za serikali na nikapata sehemu napiga tuition na Sylvan Education Systems ambao ni kama private flani hivi na malipo yao poa kinoma . Hela yangu ikawa safi, bills zote nalipa, medical insurance ninayo na familia iko poa(nina mke na watoto wawili wa kike). Juzi likizo ya krismasi nimetinga vekeshen ya nguvu na kulala hotelini siku sita na tripu ya mbungani nikapiga. Hivi sasa nimerudi back to base na niko poa kishenzi.

Kwa hivyo hawa wanaosema wanarudi Africa kwa kua maisha ughaibuni hayafai au hayawezekani wana lao jambo. Mtu anaeza kusema anakampuni yake lakini ukienda kumtembelea unakuta ishu zote anafanyia chumbani kwake na amerejista jina la kampuni yake ili kujaribu kusifia watu nyumbani kua ana kampuni. Hii ni kutafuta sifa za kimpumbavu na kuwaonyesha washkaji kijiweni kua ni mkulu flani. Kumbuka alipotoka home alikua keshasema anaenda Marekani kufanya vitu vya nguvu. Anapoingia kiwanja anakuta mambo tofauti na inabidi 'akili mukichwa'. Nishaona wengi wameingia na kujifanya wao ni watoto wa wakulu bongo na kwa hivyo hawataki kazi za kuajiriwa...yaani waleta dharau wakikuona mchizi unahangaika na dei waka yako au night shift mahala flani. Anatesa miaka miwili afu hela zinapogoma kutoka home inabidi atafute usawa mwengine. At that time kumbuka mtu hakuenda shule kutimiza ahadi ya viza yake, ashachelewa kutafuta SSN na ID na pia visa ime-expire na sasa ashapoteza status. Sasa vijana wetu kama hawa ndo wanalia njaa na kufanya kazi zisizoeleweka...hata pia kuanza kuuza madawa. Hapo ndo mwisho wa barabara yake....:rip:

Kwa hivyo its upon the individual and what his/her goals are. Ukija ughaibuni kwa vile unataka 'uwakomesha' washkaji mtaani basi utaambulia patupu. Ukija na set plans na unapiga mambo yako kimpango, I can say here confidently you will definitely be better off. Mimi nimeishi uswahilini, nimepanda dalala nikienda kazini, nimekula chipsi vumbi ili mradi nistiri njaa...nimepiga kazi ya serikali ambapo mshahara ulikua wakipuzi huku ukizangatia kua viongozi ni mafisadi na hawajali maslahi ya watu wanaofanya kazi serikalini. Nikilinganisha these two situations, I can say I'm better off a thousand times where I'm at. Sio kujisifu lakini ni kwa sababu nilifanya mambo yangu kwa mpango na sasa navuna. Nikija Africa, natesa kiheshima na narudi bila hata kuenda ubalozini kuomba viza. Msiba ukitokea natoe hela ya kugharimia wageni watakaofika home na pia nasafiri kuonyesha solidarity. Vijana wetu wengi wako out of status na wanajua wazi wakirudi home, Marekani hawatoiona tena. Wako wengi tu hapa wamepoteza wazazi na wanashindwa kuenda kuzika!!!...Yaani ni huzuni mtupu. Kazi wanazofanya hazieleweki, medical insurance hawana na ole wao wapate matatizo ambayo itabidi watinge hospitalini...hio bili itabidi walipe for the rest of their lives!

My advice to people ni kwamba ukija huku, don't put your expectations too high and be real. Fanya yaliokuleta huku kulingana na viza yako for at least 2yrs huku ukiangalia maswala ya papers.

Senti yangu hamsini hio.

Mungu ibariki Africa
I know what you are talking about Brother, I relate your story to my story, and I'm living the American dream. Niceeeee!.
 
mitsnzania ina matatizo sana arifu....imagine mods wana wivu balaa...mashori kunifagilia basi wakafuta avatar yangu....na mie nunda idon give a damn..

BTW karibu konyagi na sprite
Mimi nagoma , yaaani ile avator yako wameitoa ya nini?nilikuwa napata raha sana nikioana humu JF / kuna wanafiki walikuchongea nini? hii inabidi waitolee maelezo mkuu.
 
African migrants abandon the American dream


The American dream is not all it is cut out to be and some Africans
are turning their backs on life in the US
.

_51775774_sammymainapacking.jpg

Sammy Maina says the ten years he spent in the US would have been
more profitable at home in Africa

By Leslie Goffe
Focus on Africa Magazine
bbc.co.uk/news/world-africa-12810828

6 April 2011 Last updated at 00:19 GMT


Frustrated by tough economic times in the United States, Sammy Maina is packed, ready and waiting to return to Kenya.

"I'm fed up and finished with the US," declares Mr Maina, 33, owner of a prepaid calling card firm, Myaatel, and a money transfer company, Doubles Xpress, that caters for African immigrants.

But with money scarce because of the recession, fewer and fewer immigrants can afford to purchase his international phone cards or pay to use his money transfer services.

"People here don't have money any more," complains Mr Maina, who says the "American Dream" of a big house, flashy car and piles of money was unrealistic.
Instead he found long hours, little pay and limited joy.

Life in America is so demanding, says Mr Maina, that it has cost several of his African friends their marriages and even led some to commit suicide. "It is very difficult right now and so many people are packing and going back to Kenya in big, big numbers."

'Little Senegal'
There are an estimated one million Africans in the US.

According to the homeland security department, 130,000 Africans migrate legally to the US each year.

It is impossible to say how many returnees there are, as the evidence is anecdotal but representatives of African community associations in New York, Atlanta and Boston all say they know of large numbers of expatriates making plans to leave the US.

The reason: they cannot find jobs and have become desperate about their future here.

New York's Association of Senegalese in America has been inundated with requests from expatriates who have lost their jobs, are facing homelessness, and who want financial help to return home.

Dame Sy, a volunteer with the association, says members donate money to buy aeroplane tickets to send home Senegalese who are down on their luck in New York.
"We just sent one home in January and before that we sent between 12 and 15 last year," explains Mr Sy. "Everyday, people are talking about it."

At the association's offices in the "Little Senegal" section of Harlem, in New York, I was introduced to a 41-year-old illegal immigrant called Ndoum.

She has been having a very difficult time in the US, she says, and would happily go home to Dakar if she could find the money for a plane ticket.

Before the recession it was possible for an undocumented immigrant like her to find a menial job in a factory. Unable now to find work, and in constant fear of being seized by immigration police, Ndoum does not know what to do.

"I tell people: 'Don't come to the US now'," she says tearfully.

'Sweet Liberia'
Kenyan Irene Onyango is a 37-year-old nurse living in Delaware, near Washington DC. Her income sometimes barely covers her bills. She is also concerned that working a 16-hour day is damaging her health.

When she goes to Kenya on holiday, her friends refuse to let her pay for anything because they say she has to slave to earn her money in the US.
Now that the Kenyan constitution has been amended to allow dual citizenship, Ms Onyango says she can go home and not worry that should she need to return to the US one day, she will be stopped.

"Believe me," she says, "the next plane that goes to Jomo Kenyatta airport will have me on it."

But migration expert Kathleen Newland, a director of the Migration Policy Institute in Washington DC, says what Ms Onyango and other Africans resident in the US are doing when they return to Africa, is not reverse migration.
_51775365_pastorshadrachdeline,creditreggieerawoc%282%29.jpg

"Africans in the US will leave in record
numbers." predicts pastor Shadrach Deline


Ms Newland says this is better described as "the formation of transnational populations" - people who keep a foot on two continents.

"I think you are very unlikely to find Africans who have settled in the US giving up the insurance policy of a green card or US citizenship to completely transfer their lives back to Africa," Ms Newland says.

What transnational people like Ms Onyango will do, she adds, is divide their lives between two places. "What it does tell us about Africa is there is a lot more hope and optimism about the economic prospects," she says.

Liberian singer and pastor Shadrach Deline is one of several African expatriates in the US to recently release a song expressing a longing for Africa.

In Tomorrow I Am Going Home, Deline, a pastor of the Nation of Christ Believers' Fellowship Center in Atlanta, Georgia, sings he has "sweated hard" in the US. Now it is time for him to "sell his house, sell his car, sell his boat" and go home to "sweet, sweet Liberia".

In the video, Deline removes his Western-style three-piece suit and puts on an African robed garment.

Deline says the song's message resonates with African expatriates because no matter how comfortable an exile they enjoy, an African will always yearn for home.

"There will come a time," he says "when Africans will not even bother coming to the US because life will be so beautiful back in Africa. There will be no need to ever leave."
 
Yes! Am working as a registered nurse 40hrs a week na if I nachukua more hrs if I want at anytime. Unaweza kufanya double shifts or full time in 2 facilities bila shaka. I am making $70k + a yr napiga MBA healthcare management hybrid course na pia I am looking to invest in Tz na patner in manufacturing industry from this year. Na tyr tumeshaset mambo yote ya kimsingi by nxt month tunaanza construction tazama www.scheerfoundation.org Nina Mke na wtt hapa hatujapata tatizo lolote la kutushinda

Na haya yote nimefanya wkt nimekuja hapa 2009 July. Nakubaliana kwa 1000000% na mchangiaji hapo juu kuwa its abt goal setting na kuwa na nia ya kumeet your strategies. But huwezi kulinganisha US na Nyumbani kule Singida matongo nilipotoka. Nilishfanya kazi km afsa wa jw hd kuwa luteni for 7 yrs bt did nothing zaidi ya kutumikia mafisadi na kunywa pombe za nusu bei

Mmmhh...sounds too good to be true to me. Kama ulikuja 2009, hiyo degree ya Registered Nurse ulimaliza kwa muda gani?
 
Pengine sii nurse as in RN bali ni care partner-CNA, OR even LVN. Nurses make decent money, no matter how much debt you have ..With an RN salary one can pay off their debts really quickly.

My undesratnding is that these jobs in the healthcare sector like RN, LVN and CNA work on 12 hour shifts. I think huyo lazima atakuwa na 2nd job. Yeah that nurse story does not add up at all!!!
 
Kuna vijana wakibongo walikua wanakuja pale wakitoka klabu huku wamebwia na zereu zao....eti wanashangaa nafanya kazi na kuajiriwa nami nikawa siwajibu kitu maana I knew what I was doing to secure my future in this country.
Watanzania walikuwa "wanashangaa nafanya kazi na kuajiriwa," Watanzania gani hao, watoto wa Rostam Aziz? Hivi Marekani kuna anaemshangaa mwenzie kwa kufanya kazi ya kuajiriwa? Kumbe ufanye nini, kazi ya utumwa? Ab-Tichaz acha story za kutunga, mtu anaweza kuwa anaheshimika sana mpaka akifungua mdogo wake kutema cheche za personals zake za kuchemka ndio unamwoan huyu nae kumbe ni wale wale.

Unasifia Marekani weee halafu ukiwa Africa unalala hotel, umekuwa mtalii nyumbani? Mtanzania hajivunii kulala mahotelini, hata nyumba ya kupanga Mtanzania anaishi kwa sintokubali moyoni mwake, hatumsifu mlala mahoteli, huyo kwa mila za Kitanzania hana kwake, hana kwao, hana pa kulala. Sasa mafanikio gani unayojisifia sana kama ukija Afrika huna pa kulala?

Na hao unao wa slam kwa kutokuwa na makaratasi, unawashauri nini, waondoke au wakahonge Uhamiaji au wakafunge ndoa na crack heads wa Kimarekani? Maana unapasifia sana US halafu unasema wengi hawawezi hata kurudi wakati wa misiba, ni kwamba hapafai maana karatasi hazitoki kirahisi au kosa ni lao, wafanyeje?
 
Nilikuja na DV na tayari nilifanya Diploma na BSc Nursing Tz nilipokuja ilikuwa ni kufanya evaluation tu kupitia CGFNS (Tazama CGFNS International - global credibility in credentials evaluation) nikatambuliwa equivalency na nikafanya NCLEX (Tazama https://www.ncsbn.org/nclex.htm) ambayo ni mtihani wa nursing. Unapofaulu huu mtihani then unapata unrestricted license ya RN yaani unaweza kufanya kazi state yoyote unachotakiwa ni kufanya endorsement state unayotaka kuhamia.

Nikitangaza nataka kazi sasa hivi hapa, baada ya masaa matano nitafunga simu kwani hata chaji itaisha kila recruiter anapiga anataka kuongea aconvince kuajiriwa kupitia kampuni yake. Ukitaka kazi kama RN sasa hivi anayekuajiri kwanza anakupa bonus ya kukubali kuingia mkataba naye, kati ya $5000 hadi $20,000(e.g. ukitaka Alaska) ya kuappreciate commitment na relocation money ukaanzie maisha na kujicommit 2 years bila kukatisha mkataba.

Kuna global acute shortage ya nurses na nchi zote zinatafuta trained and experienced nurses, ukiwa US ukitaka kazi ambayo hutakaa bila kazi kbs fanya nursing then kama huipendi shift unapotaka. But it pays!!

Ukienda Quick Search unaweza kuona prospects za RN na demand, job descriptions, wages e.t.c. Kazi yangu ilikuwa kufanya graduate studies tu from there. Nikimaliza if I opt to stay I can then be a Director of Nursing popote US, Australia or UK na I can surely make a handsome amount of money to live with my family.

Thanks

Una swali jingine?

Mwanaume mzima utoke Tanzania na Diploma plus Degree in Nursing? Unataka kusema ulijiandaa kwa kusoma taaluma yenye demand ya Nursing kabla ya kuja USA ukijua ungeshinda DV lottery huku kazi za Nursing ni bwerere, siyo? My hunch is your story is still not credible.
 
Mimi nagoma , yaaani ile avator yako wameitoa ya nini?nilikuwa napata raha sana nikioana humu JF / kuna wanafiki walikuchongea nini? hii inabidi waitolee maelezo mkuu.
Mkuu kuna miwatu humu ina roho mbaya kama wakaanga sumu uknw mashori walikuwa wanaizimia pm kibao nilikuwa napata wakitaka niwe penpal wao....BTW hukupata XXXXL scand lingekupa papers
 
Watanzania walikuwa "wanashangaa nafanya kazi na kuajiriwa," Watanzania gani hao, watoto wa Rostam Aziz? Hivi Marekani kuna anaemshangaa mwenzie kwa kufanya kazi ya kuajiriwa? Kumbe ufanye nini, kazi ya utumwa? Ab-Tichaz acha story za kutunga, mtu anaweza kuwa anaheshimika sana mpaka akifungua mdogo wake kutema cheche za personals zake za kuchemka ndio unamwoan huyu nae kumbe ni wale wale.

Unasifia Marekani weee halafu ukiwa Africa unalala hotel, umekuwa mtalii nyumbani? Mtanzania hajivunii kulala mahotelini, hata nyumba ya kupanga Mtanzania anaishi kwa sintokubali moyoni mwake, hatumsifu mlala mahoteli, huyo kwa mila za Kitanzania hana kwake, hana kwao, hana pa kulala. Sasa mafanikio gani unayojisifia sana kama ukija Afrika huna pa kulala?

Na hao unao wa slam kwa kutokuwa na makaratasi, unawashauri nini, waondoke au wakahonge Uhamiaji au wakafunge ndoa na crack heads wa Kimarekani? Maana unapasifia sana US halafu unasema wengi hawawezi hata kurudi wakati wa misiba, ni kwamba hapafai maana karatasi hazitoki kirahisi au kosa ni lao, wafanyeje?

Taso,

Heshima kwako natanguliza ndugu yangu.

I believe hujanielewa katika hio posting yangu hapo juu nilikua na lengo gani.Kwanza kabisa nilichosema si hadithi ya kutunga mzee mwenzangu. These are true stories in the neighborhood I used to live. My target in posting ni kusema kwamba kuna categories mbili za watu wanaokuja ughaibuni.Kuna wale wenye malengo na target za maana wale wasiokua na malengo bali wamekuja kutamba tu. Hio story niliosema hapo juu ni kitu kilichofanyika almost 10yrs ago na kwa vile sitaki kumdhalilisha mtu, Im not at liberty to mention names.

Kuna vijana wengi pia waki-Tanzania ambao tulisota nao katika hali niliokutajia hapo juu na sasa wako poa kimaisha. Kuna room mate ambaye tulipiga makazi na kuchangamka pamoja na baada ya m'da alipomaliza degree yake akaingia Army Reserve ya Michigan na watu wakawa wanamuambia atapelekwa Iraq akafie huko. I encouraged him to follow his dream na kwa kua ana-degree sio lazima atapelekwa frontline maana hata wamarekani wenyewe amewazidi kete. He moved on into the the US Army proper na saa hizi yuko posted Ujerumani na hajakanyaga Iraq mpaka leo. Huku Marekani ukija na cheti cha form 6 na uwe ngangari wakutafuta kisomo, utawazidi hata hawa wazawa.If you keep the right company then you move forward, lakini ukijimiksi na mediocre company, basi utaishia in a mediocre state. The choice is on the individual.

Pili si eti nilikua najisifu kwa kusema niliosema na kama ungelikua unanifahamu kwa undani zaidi Im a very humble individual. Sikulelewa katika familia za hela na kwa neema zake mwenyezi nimefikia nilipofikia. Unaniuliza swali la kwa nini nilale hoteli?...Kama kweli unataka jibu basi ni kwa sababu nilikua na mgeni(my wife wangu) na alikua anataka ajionee mwenyewe sehemu zilivyo. Nyumba ninayo lakini inampangaji na kwa sababu za mkataba si kutaka a-relocate during my stay there. Nakushangaa ukisema eti mtu akiwa mtalii kwao ni makosa. Nyumba ipo Dar es Salaam na nyengine ipo Arusha...Sakina Triple A to be exact.

Kulingana na wasia ninaotoa kwa wale waliopoteza mwelekeo, ni bora warudi nyumbani waanze upya maana nd'o washachelewa kwa sababu ya tamaa zao na anasa. I will not advocate for anybody to marry a crackhead for papers sake maana hizo dili zishashtukiwa na wakati wa interview utapigwa chini tu. Tushawaambia mara kibao warudi home lakini bado wamegoma na wakipatwa na matatizo basi watu huzima simu na hawataki kusikia kilio cha kujitakia. There are many success stories and also failures na mimi napinga hoja ya watu kutoa blanket condemnation kua wabongo walio ughaibuni wanasota kila siku. Hapa nilipo kuna Accountant wa kibongo tuliokua tunapiga kazi za kuuza dukani kitambo hicho, kuna dada mmoja ni Instructor/Lecturer University, kuna Wanabiashara wawili watu wa nguvu, kuna wale wanaopiga kazi hospitali,kuna waalimu kama mimi na wengine wengi. Kwa ubavu wa pili kuna wale ambao maisha yao yamejikita katika kuvuta bangi na kubwiya unga huku wakiwa na vicheche visivyoeleweka. Grupu hii ndo inapatia watu sifa mbaya.

Kwa hivyo naomba unielewe ninachosema mwenzangu. Story za maisha ya watu huku ughaibuni zipo kibao hata tunaeza andika novel ya komedy flani. Kuna wengine wanatafutwa na mwera maana walikumbwa na kesi na wakaingia mitini. Kuna wale ambao washatumika kifungo jela baada ya police chase ya magari mpaka unashangaa.Hii ilimkuta kijana mmoja wakichaga aliyedhani yuko Arusha na anakunywa tembo kisha anataka kuendesha gari hovyo. Mwera zilipompiga mataa, mchizi akakataa kusimama na ikabidi police chase ya magari kibao ungedhani ni wale wa-Mexico wa L.A.. Jamaa aligonganga gari la bwana mwengine ndipo akasimama. Aliposhuka na ulevi kichwani alikumbuka kulia "Yesu mwana wa Maria" mpaka zile mwera zikacheka. Jamaa alikosea kidogo tu kupigwa tembe.Mwishowe ikabidi mshkaji akope hela za kulipa mahakama baada ya kesi na mambo ya probation. Yaani ni vituko mtindo mmoja.

Kwa hayo machache, I was just making a point and not boasting.

Good day to you.
 
Hata kama yote ingekuwa kweli, hiyo Nursing ni kazi ngumu relatively speaking, na tukirudia chanzo cha malumbano, siyo ajabu wengi kwenye career choice hiyo wanaelemewa na stressful working conditions. Siyo kila mtu anathamini pesa zaidi na material comforts/assets duniani. That being said, kama kuingia US Army nayo ishakuwa dili, basi that kinda sums it all up.
 
Pengine sii nurse as in RN bali ni care partner-CNA, OR even LVN. Nurses make decent money, no matter how much debt you have ..With an RN salary one can pay off their debts really quickly.

My undesratnding is that these jobs in the healthcare sector like RN, LVN and CNA work on 12 hour shifts. I think huyo lazima atakuwa na 2nd job. Yeah that nurse story does not add up at all!!!
Lazima huyo dada atakuwa STNA,Hao wanaitwa nurses lakini ni wasaidizi tu wa hao nurses,yani nurse aides.Sidhani kama huyo dada ni a registered nurse ie LNP. or RN
 
Mbele ni mbele tu...huku afrika(tanzania) hakufai mafisadi,ukimwi kila kona. No rule of law.
 
Anyway tatizo au swali lilikuwa nini? Nilijibu kwamba nurse anaweza kufanya kazi masaa 16 lililoulizwa but mafanikio yapo mahali popote yote uyajuayo yawe materially au vingine unavyosema na yote hayaji kwa uzembe na uvivu, Kama nursing ngumu ni km kazi zingine au ipi rahisi uijuayo wewe? Kila kazi ni stressful but tunafanya tu. Maisha popote but all in all...

Ukubali kwamba siyo kila mtu anajali amount of dollars tu anazolipwa kila saa au kila mwaka kama kipimo cha kuridhika kimaisha. Wewe sema usharubuniwa na false lure of materialism in America: lakini at end of the day, wewe ni mtumwa tu na bila shaka, una madeni kibao hapo ulipo: so much so that, you have to go out and do long hours, at any day and at any time, just so you could barely service your monthly bills aka maintain your so-called "piece of the America Dream".

By the way, kama sikosei, umetoka Bongo ukaenda moja kwa moja USA: sasa unajuaje kama opportunities America ni mara "millioni" ukilinganisha na nchi nyingine? You're sold bro!
 
Ok! mtumwa wa familia yangu but not wa mafisadi!? anyway ni mtazamo wako mkuu nauheshimu! sina deni, napiga kazi, nasoma, nainvest a multimillion dollar project in Tz. Na next week ntakuwa Dar naevaluate project niendelee next stage baada ya kuwekeza $100,000 miezi 8 iliyopita! So my bro keep ya Tz dream Am keeping my Monthly bills aka American dream, tchao

www.scheerfoundation.org

Mos def & more power to you bro! I understand, given your knack for foretelling the future and whatnot, the only thing that can come in between your "multimillion dollar project in Tz" and tenure at your local nursing home, is your foreseen appointment as next Surgeon General of US by Obama in 2013. By the way, what exactly do you mean by "Tz dream"?
 
ab tichaz kaongea akili''unajua watu badala ya kuwaambia ukweli vijana wao wanafanya kuwatisha hyo haisaiidii mwingine sasa anakimbia kunywa maji mkachafu kila cku huyo utamwabia nn?waambie vijana wanenda kufanya nn wajue wanachofuata cyo kuwatisha eti cjui maisha ya ughaibuni hayana dili au vipi maisha popote umejipangaje dunia inafanana sasa hvi''tuwaambie vijana wetu jinsi ya kujipanga kwenda kuchukua dola za wazungu kuzileta nyumbani cyo kazi ya kuwatisha tu'sasa hvi watu wanakwenda vacation florida mtu napiga dili bongo tunawaona wakina shy rose bhanji wanakwenda kutembea marekani likizo''sasa tuwajenge vijan kihivyo cyo kuwapagawisha bna maneno ya kukata tamaa cjui nn'aaaaaaaaaah me wabongo wananikera sana ongea akili kama za jamaa hapo tukuelewe.
 
Mimi niko hapa toka 1997 nilikuja nilipomaliza form six ukweli ni huu. Kama kuna mtu anataka kuja USA na kufanikiwa kwa miaka miwili ni bora ubaki nyumbani.
Ni lazima uwe na lengo ukija marekani watu wengi wanasema nataka maisha mazuri lakini ni lazima uweke bayana unaposema maisha mazuri unamaana gani? Mimi kwa mfano lengo langu halikuwa kuwa na maisha mazuri hapa kwani ningeweza kuwa na maisha mazuri bongo lakini lengo langu lilikuwa (a) Nije hapa niweke base ya watoto na nifungue milango kwa familia kwa baadaye (b) Nisome (c) Nijifunze kuwa imara kimaisha (d) Nipate ujuzi na nitafute business ambazo hazipo Tanzania na nikafanye/nikafungue . Imenichukua miaka mingi kufanya vitu vyote hivyo lakini nimefanikiwa vitu vyote shule ya digrii ya kwanza ni ngumu sana hapa imenichukua miaka 6 kumaliza, makaratasi nimepata, ndugu zangu wamekuja wengine wanatangeneza hadi $100,000 kwa mwaka na mambo yao mazuri wote wamesoma, wote tunajenga nyumbani, ninaenda bongo kufungua biashara n.k. Lakini kwenye miaka yote hiyo nimefanya kazi zote nilianza kuwa kibega na kuosha vyoo na sasa ni analyst kwenye kampuni ya 20 kwa ukubwa duniani. Maisha ni uvumilivu na malengo!. Kuna ndugu zangu wanataka kuja hapa wafanikiwe kwa mwaka mmoja. Kimoja cha kusema ukija marekani jihusishe na watu wenye malengo kwani kuna uswahili sana hapa na kama ukijiingiza kwenye mashindano ya kimaisha utaishia kubeba mabox na kushindana kuvaa, idadi ya wanawake na magari!. Unahitaji ku focus sana hapa.
Kama umesoma na una degree usije hapa nenda canada. Canada wana program ya kutoa Green Card kwa wahamiaji wenye elimu hivyo fanya hiyo process inachukua kama mwaka hivi na inahitaji deposit ya $10,000 wakati ukiingia Canada baada ya kukubaliwa. Uzuri wa hii process ukisha ingia Canada chukua Mkopo wa shule na soma masters na itakuwa rahisi kuja hapa kwasababu utakuwa na creen card ya kanada. Ukija hapa process za makaratasi zitakupasua kichwa sisi tuliweza kwasababu tulikuja wadogo 21 years. Kama ni mtu mzima ni bora upitie nyia ya Canada.
Kitu kimoja ambacho watu wengi hatuongelei ni kwamba Watoto huku wanasoma soma shule nzuri sana na ni bure, mabasi ya watoto ni bure, chakula ni bure,. Vilevile kwa watu wenye magojwa au kama wazazi wako wanamagojwa USA ni pazuri kiwango cha matibabu ni cha juu sana India*100

Hivyo hapa ndugu zangu inatokana na mtu mwenyewe umri, elimu na malengo!!! Lakini kuna watu wengi tu wanafanya kazi nzuri na maisha ni poa sana lakini mwanzo ni mgumu sana.
 
Heshima kwenu wakuu.

Nimesoma posts zote nilichogundua ni kwamba lazima uwe na malengo ukitaka kufanikiwa kimaisha ei kufanyakazi kwa bidii,kukwepa makundi yasiyokuwa na malengo na nk.Malengo ni kitu muhimu sana kama utataka kufanikiwa si huko majuu tu hata huku nyumbani ukitaka kufanikiwa lazima uwe na malengo.

Mkuu Ab-Titchaz & Co

Asante kwa maelezo na ushauri mzuri kwa vijana wetu wanaofikiri ughaibuni kila kitu kiko bwerere.Mkuu huku nyumbani zipo fursa kibao leo ukiniambia niende US sina hamu hata kidogo labda kutembea tu.Nakiri maisha ya US na TZ nitofauti sana US imeendelea sana lakini bado hujanishawishi niondoke TZ kwakuwa ni maskini au vyovyote utakavyosema.Yapo makampuni TZ yanalipa fedha nzuri ukijipanga vyema kwa maana ya kuepuka maisha ya kijinga utasonga mbele.
 
Back
Top Bottom