Kiranja wa jamii
JF-Expert Member
- Jan 2, 2023
- 1,137
- 2,702
Baada ya lile jinamizi la Oktoba 29, watu wangi walioto ndoto za kutisha
Kuna waliowaona polisi kadhaa wakifungwa magereza kwa makosa yasiyo ya kwao,
Kuna waliolia kilio na kuomboleza ndotoni huku wakilikumbatia na kulibusu jeneza la kiongozi mmoja mkubwa sana
Kuna walioota wakiona mamlaka za watawala wa nchi wasiyoijua zikiyumba, viongozi wakivurugana, kuzushiana maneno na hata kudhalilishana hadharani
Lakini, katika zote kuna ndoto iliwasumbua sana watawala wa nchi isiyojulikana ya kuwatia hatiani wanaowasumbua na kuhakikisha wanafia magereza na wafuasi wao kusambaratika
Kila walipoota ndoto hii, kwasababu waliiota wote kwa pamoja asubuhi waliweka vikao vya majadiliano na kutafuta suruhisho la ndoto hiyo
Soma Pia: Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia za Uchaguzi mwaka 2025
Hatimaye wamepata wanachokiona ndo suruhisho! Kutengeneza mashitaka mazito mazito dhidi ya kila wanayemuhisi hayuko upande wao
Ndio, ni hakika na kweli kwao hilo ndio suruhisho waliloliona na katika kulitekeleza hawataona taabu kuwatoa kafara baadhi ya waliokuwa miongoni mwao. Ndio, usipotoa kafara utaaminikaje?
Mbuzi wa kafara wajiandae kisaikolojia watasurubiwa pamoja na hao waliolengwa
Ndoto ya muda mrefu ya kulisambaratisha kundi kubwa linaloaminika na kukubaliwa na wengi, wameshaihamishia kwenye mchoro wa makaratasi
Swali la msingi, wamepiga mahesabu yao vizuri? Wame "calculate the risks na wako tayari kuzi handle?
Sasa kumekucha na kumekucha na tume pacha ya ile ya Chande
Kuna waliowaona polisi kadhaa wakifungwa magereza kwa makosa yasiyo ya kwao,
Kuna waliolia kilio na kuomboleza ndotoni huku wakilikumbatia na kulibusu jeneza la kiongozi mmoja mkubwa sana
Kuna walioota wakiona mamlaka za watawala wa nchi wasiyoijua zikiyumba, viongozi wakivurugana, kuzushiana maneno na hata kudhalilishana hadharani
Lakini, katika zote kuna ndoto iliwasumbua sana watawala wa nchi isiyojulikana ya kuwatia hatiani wanaowasumbua na kuhakikisha wanafia magereza na wafuasi wao kusambaratika
Kila walipoota ndoto hii, kwasababu waliiota wote kwa pamoja asubuhi waliweka vikao vya majadiliano na kutafuta suruhisho la ndoto hiyo
Soma Pia: Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa Kijinai wa Matukio ya Ghasia za Uchaguzi mwaka 2025
Hatimaye wamepata wanachokiona ndo suruhisho! Kutengeneza mashitaka mazito mazito dhidi ya kila wanayemuhisi hayuko upande wao
Ndio, ni hakika na kweli kwao hilo ndio suruhisho waliloliona na katika kulitekeleza hawataona taabu kuwatoa kafara baadhi ya waliokuwa miongoni mwao. Ndio, usipotoa kafara utaaminikaje?
Mbuzi wa kafara wajiandae kisaikolojia watasurubiwa pamoja na hao waliolengwa
Ndoto ya muda mrefu ya kulisambaratisha kundi kubwa linaloaminika na kukubaliwa na wengi, wameshaihamishia kwenye mchoro wa makaratasi
Swali la msingi, wamepiga mahesabu yao vizuri? Wame "calculate the risks na wako tayari kuzi handle?
Sasa kumekucha na kumekucha na tume pacha ya ile ya Chande