PreGE2025 Ndolezi Petro wa ACT Wazalendo asema kuwa kuwakataza wananchi wasijiandikishe ni kampeni ya hovyo ya CDM kuwahi kutokea

PreGE2025 Ndolezi Petro wa ACT Wazalendo asema kuwa kuwakataza wananchi wasijiandikishe ni kampeni ya hovyo ya CDM kuwahi kutokea

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Waziri kivuli wa ofisi ya waziri mkuu- bunge, Sera, vijana, kazi na ajira, Kutokea ACT Wazalendo, Ndolezi Petro kupitia ukurasa wake wa X ameandika kuwa uamuzi uliotolewa na Mwenyekiti wa Chadema Ubungo wa kuwazuia wananchi kujiandikikisha kwenye daftari la uchaguzi kuwa ni kampeni ya hovyo ya CDM kuwahi kutokea.
1742194476160.png


===
Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa kichama Ubungo

“Nape yalimtoka yaliyokuwa moyoni akizungumza kwamba kushinda inategemea nani anayetangaza yule ni kijana wa kwenye chama kile kwa muda mwingi sana kwa hiyo kwa vyovyote ni vyema tukamsikiliza. Ikiwa hivyo kwamba mapenzi ya yule anayetanganza ndiyo uamuzi, wananchi wana haja gani ya kuja kujiandikisha na sasa tunawaambia kwamba zoezi la kujiandikisha kupiga kura kwa mkoa wa Dar Es Salaam wanatakiwa waanze kesho ili iweje wajiandikishe waende kwenye zoezi ambalo kwa hakika kura zao hazitaheshimiwa. Na ndiyo maana katika vikao vyetu tulivyofanya kwa siku za karibuni tumedhamiria dhahiri kwamba hatutatoa ushirikiano kwenye suala hili la uandikishaji wa wapiga kura, wanachama wetu na ndugu zetu hatuna sababu ya kupoteza muda kwenda kwenye daftari ambalo hilo daftari lenyewe tunataka hilo daftari lenyewe lifanyiwe mabadiliko.

“Tunaposema Reforms ni pamoja na hilo daftari uchaguzi liweze kufumuliwa liweze kuandikishwa upya. Msimamo wa chama chetu ni kuhakikisha kwamba lile daftari la wapiga kura watu sahihi waliopo kule ndani waandikishwe lakini pili tuwe na uwezo wa kulifikia daftari hilo bila mizengwe.” Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, Mkoa wa Kichama wa Ubungo Amos Maziku.

Source: Jambo TV

Soma pia: Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
 
Waziri kivuli wa ofisi ya waziri mkuu- bunge, Sera, vijana, kazi na ajira, Kutokea ACT Wazalendo, Ndolezi Petro kupitia ukurasa wake wa X ameandika kuwa uamuzi uliotolewa na Mwenyekiti wa Chadema Ubungo wa kuwazuia wananchi kujiandikikisha kwenye daftari la uchaguzi kuwa ni kampeni ya hovyo ya CDM kuwahi kutokea.
View attachment 3273669

===
Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa kichama Ubungo

“Nape yalimtoka yaliyokuwa moyoni akizungumza kwamba kushinda inategemea nani anayetangaza yule ni kijana wa kwenye chama kile kwa muda mwingi sana kwa hiyo kwa vyovyote ni vyema tukamsikiliza. Ikiwa hivyo kwamba mapenzi ya yule anayetanganza ndiyo uamuzi, wananchi wana haja gani ya kuja kujiandikisha na sasa tunawaambia kwamba zoezi la kujiandikisha kupiga kura kwa mkoa wa Dar Es Salaam wanatakiwa waanze kesho ili iweje wajiandikishe waende kwenye zoezi ambalo kwa hakika kura zao hazitaheshimiwa. Na ndiyo maana katika vikao vyetu tulivyofanya kwa siku za karibuni tumedhamiria dhahiri kwamba hatutatoa ushirikiano kwenye suala hili la uandikishaji wa wapiga kura, wanachama wetu na ndugu zetu hatuna sababu ya kupoteza muda kwenda kwenye daftari ambalo hilo daftari lenyewe tunataka hilo daftari lenyewe lifanyiwe mabadiliko.

“Tunaposema Reforms ni pamoja na hilo daftari uchaguzi liweze kufumuliwa liweze kuandikishwa upya. Msimamo wa chama chetu ni kuhakikisha kwamba lile daftari la wapiga kura watu sahihi waliopo kule ndani waandikishwe lakini pili tuwe na uwezo wa kulifikia daftari hilo bila mizengwe.” Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, Mkoa wa Kichama wa Ubungo Amos Maziku.

Source: Jambo TV

Soma pia: Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
maelezo na heading yanavurugana kidogo na maudhui ya ndani, nadhani inafaa kuedit maelezo kidogo gentleman na itapendeza zaidi 🐒
 
Waziri kivuli wa ofisi ya waziri mkuu- bunge, Sera, vijana, kazi na ajira, Kutokea ACT Wazalendo, Ndolezi Petro kupitia ukurasa wake wa X ameandika kuwa uamuzi uliotolewa na Mwenyekiti wa Chadema Ubungo wa kuwazuia wananchi kujiandikikisha kwenye daftari la uchaguzi kuwa ni kampeni ya hovyo ya CDM kuwahi kutokea.
View attachment 3273669

===
Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa kichama Ubungo

“Nape yalimtoka yaliyokuwa moyoni akizungumza kwamba kushinda inategemea nani anayetangaza yule ni kijana wa kwenye chama kile kwa muda mwingi sana kwa hiyo kwa vyovyote ni vyema tukamsikiliza. Ikiwa hivyo kwamba mapenzi ya yule anayetanganza ndiyo uamuzi, wananchi wana haja gani ya kuja kujiandikisha na sasa tunawaambia kwamba zoezi la kujiandikisha kupiga kura kwa mkoa wa Dar Es Salaam wanatakiwa waanze kesho ili iweje wajiandikishe waende kwenye zoezi ambalo kwa hakika kura zao hazitaheshimiwa. Na ndiyo maana katika vikao vyetu tulivyofanya kwa siku za karibuni tumedhamiria dhahiri kwamba hatutatoa ushirikiano kwenye suala hili la uandikishaji wa wapiga kura, wanachama wetu na ndugu zetu hatuna sababu ya kupoteza muda kwenda kwenye daftari ambalo hilo daftari lenyewe tunataka hilo daftari lenyewe lifanyiwe mabadiliko.

“Tunaposema Reforms ni pamoja na hilo daftari uchaguzi liweze kufumuliwa liweze kuandikishwa upya. Msimamo wa chama chetu ni kuhakikisha kwamba lile daftari la wapiga kura watu sahihi waliopo kule ndani waandikishwe lakini pili tuwe na uwezo wa kulifikia daftari hilo bila mizengwe.” Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, Mkoa wa Kichama wa Ubungo Amos Maziku.

Source: Jambo TV

Soma pia: Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze
Kwa uchaguzi gani sasa?
 
Kwa aina ya uchaguzi nilioushuhudia 2020, yaani hata sitapiga kura tena nchi hii bila reforms alizosema Lissu.

ACT ni chama kisichojitambua kwasababu kimeundwa bila kuwa na falsafa iliyonyooka.

Ndo maana mara nyingi huwa ni chama kisicho na misimamo
 
Kwa aina ya uchaguzi nilioushuhudia 2020, yaani hata sitapiga kura tena nchi hii bila reforms alizosema Lissu.

ACT ni chama kisichojitambua kwasababu kimeundwa bila kuwa na falsafa iliyonyooka.

Ndo maana mara nyingi huwa ni chama kisicho na misimamo
Katika maamuzi ambayo hayajawahi kuwa na matokeo ni ya kususa kupiga kura.

Tukiweka assumption kuwa kuna wizi wa kura, Kadri kura zinavyopigwa kwa mtu "X" ndivyo ugumu wa kuiba kwa ajili ya mtu "Y" unavyoongezeka, ukijumlisha na ukuaji wa tech, ugumu unazidi kuongezeka. Ugumu wa kuiba kura 2020 huwezi linganisha na 1990 na hutaweza ulinganisha na 2030. Miaka inavyosogea ndivyo inavyokuwa ngumu.
 
Back
Top Bottom