Ndoa ya dini 2 ipi ilio sahihi?......

mahirtwahir

JF-Expert Member
Jan 12, 2013
613
311
Salamu ukumbini, nimerudi wamalenga
Nauliza uwanjani, majawabu sitopinga
Yametokea mjini, msiniifanye mjinga
Dini mbili harusini, ndoa gani tutafunga

Moja ya kuumeni, dini njema imefunga
Kijana ana imani, muislamu kajijenga
Lakini mashakani, mchumba alompanga
Nisharti kanisani, ndoa kwenda funga

Mapenzi yalozaini, hatoweza kujikinga
Yamezama akilini, sukari aita mchanga
Tena ameshabaini, kwa dhana alojenga
Bila yeye kanisani, mapadri wataipinga

Mapenzi ya majinuni, ambayo yamejitenga
Yamesibu na kukeni, mahaba yameviringa
Wako tayari jamani, msikitini kwenda funga
Alovinjari shekhani, kafiri anampinga

Nami niko hatarini, tahadharini malenga
Mnijibu kwa makini, hoja zenu kuzipanga
Jukumu langu idhini, ambayo nnaichunga
Itoke kwamisheni, ndoa njema kuifunga

Lapili haki yanani, kwa dini imenifunga
Naye mwanadani, kaja nawake mnyanga
Atakavyo karibuni, ujanani kujitenga
Kaja na hoja nyingi, zimeleta majanga

Asema yumo hakini, kwa hoja alozojenga
Tafauti hajabaini, mapenzi yamemfunga
Nimpe mume yakini, mchumba nisompinga
Jambo la walakini, makanisa anajenga
 
Ndoa ya dini kuwili, serikali kuifunga
Isije pini mahiri, upandemo kujitunga
Si jambo la kukariri, hekima ya kujifunza
Bomani mkanadhiri, ndoa yenu kuikunga

Ukenda msikitini, kanisani hujaenda
Utakosa kwa idhini, wakwezo utawatenga
Vipi kuanza ubini, kwa choyo cha kuwachenga?
Bomani kula yakini, ndoa yenu kuijenga

Baba we wapata mama, na mama apata baba
Ni heri kuunga vyama, kwenye lindi la mahaba
Vipi ulete lawama, kwa kuikana nasaba?
Bomani nenda salama, ndoa ya tunu dawama
 
Ndoa ni maridhiano, kwa mke pia kwa mme,
kwa yakwenu mapatano vipi dini ziwanyime,
uwacheni mvutano, na maneno muyapime
si kanisa si msikiti, ndoa ni watu wawili
 
Kama mume islamu,mke shurti asalimu.
na kama mume wa kanisa,mke budi kunasa.
bila kumung'unya maneno,mke hana kikomo.
watoto kukosa msimamo,kwa mume kukosa ukomo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom