Ndoa ndoano

Chamachama

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2014
Posts
200
Reaction score
129
Jamani ipo hivi, Jamaa yangu ni Mwalimu ,ana mahusiano na mwalimu mwenzie ,na wana miezi michache tu,lakini ikumbukwe huyu dada tayari alikuwa na mchumba kabla ya kukutana na huyu mwalimu mwenzie bila kujua.

Lakini mwalimu alijua uwepo wa huyu jamaa,tatizo liko hapa ,jamaa yangu tayari amekwisha funga Ndoa (Harusi) tena kanisani na huyu mwalimu,

Nzuri zaidi mwanamke alitokea kwa mwalimu siku anaenda Dar es salaam kufunga harusi na huyo teacher alimsindikiza mpaka stendi,baada ya harusi kwisha wameenda honeymoon jamani ndoa ina siku tatu binti kamtamkia mumewe hamtaki na hampendi.

Bali mapenzi yapo kwa yulemwalimu,binti ashaondoka na hayupo kwake yupo kwa mwalimu hapa ,jamani hebu tumshauri huyu jamaa ,na tuangalie kiundani huyu dada alikuwa na lengo gani.
 
Haina shida hayo ndio maisha aliyochagua kuishi. Acha awe uwanja wa mazoezi
 
Wanawake wengine ni kama wana mapepo tu,
Kuwatia watoto wetu nuksi.

Wakati mwingine wanalazimisha watu kutumia kitu chenye ncha kali.
 
Hiki kipengele nimesoma mara mbili sijakielewa.........naweza kuwa kichwa nazi.......?
Yaani kidumu kilimsindikiza binti ili aende kuolewa Dar. Baada ya siku tatu tu binti kadivorce na kurudi kwa kidumu ambacho ni mwalimu mwenzie mikoani
 
Wanawake wengine ni kama wana mapepo tu,
Kuwatia watoto wetu nuksi.

Wakati mwingine wanalazimisha watu kutumia kitu chenye ncha kali.
Mama si mabinti ila ni pressure za wazazi ati mbona hujaolewa, olewa sasa. Ni bora ikafika wakati watoto wenu msiwa-pressurize ati waolewe. Hii ni mbaya sana kulazimisha binti aolewe. Mwache akimuona anayemfaa ataolewa tu kama hakuna achana naye ni maisha yake
 
Asante kwa kunielewesha.......kumbe ndio ilikuwa hivyo........huyo mwanamke ni mchafu sana........hafai.......
Tumeaambiwa tusihukumu tusije hukumiwa. Ila kubali usikubali ni kosa la la Wazazi na jamii kwa huyo binti. Uliza wengi wenu mnavyopata stress ukitimiza miaka 25 bila kuchumbiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…