hapo sasakwa nini aliliambia hilo njemba la nje kuwa ana mimba yake wakati ana mume? angeongea kwanza na mume, akimtimua ndo aliambie hilo njemba.
habar za masiku wanajamvi la mmu. Me bado hali yangu ni tete na hiki kitambi. Leo nikiwa clinic nimepata kisa cha kusikitisha, kuna dada mjazito alikuwa analia. Katika maongezi akaniambia ana mimba sio ya mume wake ila kamweleza ukweli mumewe kasema atamtunza tu huyo mtoto ila aandikishwe clinic kwa jina la mumewe. Mwenye mzigo nae kasema aandikishwe clinic kwa jina lake . Mumewe kamsamehe kwa sababu alikuwa anamtesa mkewe na kulala nje. Sasa amejirudi. Na mume hataki huyo mtoto akizaliwa aitwe kwa jina la baba mwingne. Leo ameshindwa kuanza clinic. Tumsaidie kwa mawazo.