Umezaa watoto wako wawili ukiamini wanatosha kwa maisha ya sasa. Mmeo kwa sasa ndio mkubwa kwao na pia wanakaka yao ambaye alikuwa ni mkubwa kwake akafariki na kuacha mototo mmoja wa kuime jina MZEE, mama MZEE aliondoka na mwanae baada ya mmewake kufariki. Mama MZEE baada ya kufiwa na mme alienda akaolewa tena na mme mwingine, na huyu mme mwigine hakumpenda MZEE. Hivyo MZEE alikuwa katika maisha ya shida na manyanyaso na haswa akoishia kuwa mtukutu, shuleni hafiki na pia anaudokozi wa hela na vitu. Basi yule Mama Mzee akaona huyo MZEE amemshinda na pia anamgombanisha sana kwenye ndoa yake mpya, akamleta kwetu sisi ambako ndio kwa baba yake mdogo.Sasa mtihani unakuja baba mdogo yeye anafakazi mkoani familia inakaa Dar, MZEE ameachwa familia Dar, anamiaka 11 umri moja na mwanao mkubwa, lkn mtukutu, mdokozi, hajui kusoma na mmemuandikisha shule za kanumba amegoma hafiki shule anataka aende English media kama watoto wako wengine, mmemuandikisha tuition pia hafiki mda wa tuition anaenda kucheza mbali na nyumbani, Majirani washaanza kulalamika michezo yake na watoto wa kike sio mizuri.Mmeo kila ukijaribu kumeleza matatizo ya mototo anagoma anakwambia nyie wanawake mna maneno sana. Sie kwetu hakuna watoto watukutu kwa hiyo hayo maneno unamsingizia mtoto. Mtoto weekend ambayo baba yake yupo ni mstaarabu ajabu, kila saa ameshika kalamu na karatasi anajifunza aeiou.Yamemkuta rafiki yangu mmoja