Ndoa hii itakalika kabisa

Ndoa hii itakalika kabisa

iphone 18 promax

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2012
Posts
2,921
Reaction score
2,161
kuna mtoto wa baba yangu mdogo anataka kuoa mwanamke aliye na elimu ya degree na yeye ni kidato cha NNE japo hela zipo hii ndoa itakalika kweli Mimi naona kama hawaendani hebu tusaidizane wewe umewahi kuona
 
Yasiyokuhusu yasikusumbue,wao wameamua kuoana wakiyajua yote hayo.
 
Hiyo ndoa baada ya miaka miwili inahatihati ya kuwa migogoro isiyoisha kwasababu yawezekana mwanamke yuko desperate kuolewa tu ila elimu inamata sana. Na hawa viumbe kama ujuavyo, wanasumbua sana wakishajua wako juu kwa kitu flani.

Mwambie ajipange na kuwa makini, akimpa kinafasi tu, mwanamke atakuwa baba halafu mwanaume atakuwa mama.
 
Hiyo ndoa baada ya miaka miwili inahatihati ya kuwa migogoro isiyoisha kwasababu yawezekana mwanamke yuko desperate kuolewa tu ila elimu inamyata sana. Na hawa viumbe kama ujuavyo, wanasumbua sana wakishajua wako juu kwa kitu flani.

Mwambie ajipange na kuwa makini, akimpa kinafasi tu, mwanamke atakuwa baba halafu mwanaume atakuwa mama.

Natamani ifungwe hii ndoa Ili tushuhudie huyo mwanaume atakayekuwa mama atakavyobeba Tumbo na kuingia leba.
Wanaume wengi hawajiamini sijui kwa nini.
Hebu tambueni elimu ya mke,financial stability yake na chochote kingine alichokuzidi havishushi uanaume wako!!!
 
Natamani ifungwe hii ndoa Ili tushuhudie huyo mwanaume atakayekuwa mama atakavyobeba Tumbo na kuingia leba.
Wanaume wengi hawajiamini sijui kwa nini.
Hebu tambueni elimu ya mke,financial stability yake na chochote kingine alichokuzidi havishushi uanaume wako!!!

Mkuu sijamaanisha mwanaume atabeba mimba, lakini kuna level ambayo mwanamke akishakuwa na sauti ndani ya nyumba tayari sifa zote za mwanaume ashazibeba.

Hata hivyo wanawake ndio hawajiamini ndio maana akishapata nafasi kama hiyo anaitumia kugeuza ukweli ktk familia.

Familia nyingi zenye wake wenye either kipato kikubwa au elimu kubwa wanakuwa hawashikiki. Akili ya mke siku zote inajua mwanaume anatakiwa anizidi na kunihudumia kwa kila kitu, ikiwa kinyume mwanaume hesabu maumivu in a long run.

Hiyo ndoa itadumu tu endapo mke sio mhaya, wanahofu ya Mungu au mwanaume hatoyumba kiuchumi.
 
Natamani ifungwe hii ndoa Ili tushuhudie huyo mwanaume atakayekuwa mama atakavyobeba Tumbo na kuingia leba.
Wanaume wengi hawajiamini sijui kwa nini.
Hebu tambueni elimu ya mke,financial stability yake na chochote kingine alichokuzidi havishushi uanaume wako!!!

Madam Ennie (sorry kama si ke maana jf nayo ina yake kwenye hizi IDs) sentensi yako ya mwisho imekaa kinadharia zaidi. Imejikita zaidi kwenye vile mambo yalipaswa kuwa si vile mambo yalivyo.
 
Madam Ennie (sorry kama si ke maana jf nayo ina yake kwenye hizi IDs) sentensi yako ya mwisho imekaa kinadharia zaidi. Imejikita zaidi kwenye vile mambo yalipaswa kuwa si vile mambo yalivyo.
Uko sahihi mie ni ke.
Sidhani kama ni kinadharia,ndivyo mambo yalivyopaswa kuwa na ndivyo yalivyo.
Wanaume wajiamini tu na hata ku support wake zao ikibidi maana hizo gains mwisho wa siku ni za familia.
 
kuna mtoto wa baba yangu mdogo anataka kuoa mwanamke aliye na elimu ya degree na yeye ni kidato cha NNE japo hela zipo hii ndoa itakalika kweli Mimi naona kama hawaendani hebu tusaidizane wewe umewahi kuona

Acha wivu,afadhali huyo ana hela na form four yake kuna jamaa yangu std 7 ana mke ana master na wako happy now ndoa yao ina ten years na watoto watatu,hiyo imagination yako au kawivu fulani kanakusumbua achana nayo ndoa ni taasisi ya kipekee duniani.
 
Madam Ennie (sorry kama si
ke maana jf nayo ina yake kwenye hizi IDs) sentensi yako ya mwisho
imekaa kinadharia zaidi. Imejikita zaidi kwenye vile mambo yalipaswa
kuwa si vile mambo yalivyo.

Hahaha! Dah!
 
Hakuna mahali ndoa inahusisha elimu ya mtu au watu...

Ndoa ni darasa la upendo...acheni wenye kutaka kupendana zaidi waoane!!!
 
hapa haijalishi chuo darasa la 7 au mtoto wa bakhresa ukishindwa kutambua mipaka yako kama mke ni kibuti tu hela za kwangu hazikuhusu ww na elimu ya kwanfu haikuhusu ww
 
Ukiona mtu anahusisha elimu na ndoa ujue huyo hajajua maana ya ndoa ni nini... Ndoa inatakiwa ibaki kama ndoa na elimu ibaki kama elimu. ili mradi tu mmekubaliana wote wawili mkaridhiana kuwa mwili mmoja
 
Kitu anachohitaji mwanaume ni kujiamini. Kuna wanaume wana digrii moja na wanawalipia wake zao kusoma phd. Na wanawapa support hata wakati wa kukusanya data.

Wewe haujiamini, nduguyo anajiamini. Stay on your lane!
 
Acha wivu,afadhali huyo ana hela na form four yake kuna jamaa yangu std 7 ana mke ana master na wako happy now ndoa yao ina ten years na watoto watatu,hiyo imagination yako au kawivu fulani kanakusumbua achana nayo ndoa ni taasisi ya kipekee duniani.

nimeiona couple moja hiyo nikaona kweli hii kitu ipo.
Jamaa darasa la saba, mke alikuwa form four wakati anaolewa.
Amesomeshwa na mumeww hadi sasa hivi ana masters na wako very happy, hii si maigizo ni maisha yao halisi.
Sikujuaga elimu ya jamaa hadi juzi tu hapa ndio nikaambiwa.
Hii kitu inawezekana sana tu kama kweli wataona sababu wanapendana
 
Kitu anachohitaji mwanaume ni kujiamini. Kuna wanaume wana digrii moja na wanawalipia wake zao kusoma phd. Na wanawapa support hata wakati wa kukusanya data.

Wewe haujiamini, nduguyo anajiamini. Stay on your lane!

Exactly umesema!
 
Nackitika sana kuona wanaume wenzangu wale wenye vichwa viwili vinavyofanya kazi ipasavyo kushindwa kujiamini eti! kisa mwanamke amesoma wakati ukiangalia hata kwenye holy bible tumeshapewa mamlaka ya kuwatawala. Wanaume amkeni
 
Kwani digrii kitu gani kwenye mahusiano? huo ni uoga wako mpaka wameanza mahusiano na kufikia hatua hiyo maana yake wameridhiana, ndo nyie mnafurahi watu wanapopata shida na ndoa zao ili mpate sababu ya kuendelea kuzini
 
Back
Top Bottom