Hivi maana yake nini, unaishi na mwanaume miaka 5 mmezaa watoto wawili,kiuchumi kidogo mnajiweza, lakini hataki kutangaza ndoa, kwenda kwenu wala kukupeleka kwao. na kila siku yupo busy na bint huwa anadai ni x-girl friend wake, ampigie simu,amtumie ela, amfanyie kazi zake za shule. anadai hawezi kuacha kuwasiliana nae kwa sababu pia wanatoka kijiji kimoja na wanaundungu, kuhusu ndoa unapomkumbusha anakwambia hilo ndo jambo la maana kuongelewa lkn dakika moja amesahau mpaka utakapomkumbusha tena jibu ni lilelile.nipo jia panda maana hata ndugu zangu wanaogopa kunitembelea wakiamini hapa hamna ndoa. Wanangu hawajabatizwa nimeenda kanisani nikaambiwa hamna ndoa hakuna watoto kubatizwa. Nifanyeje maana nimembeleeleza nahisi kukata tamaana niondoke nikaanze maisha yangu na wanangu ili aendelee kutafakari anataka nini.