MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
Napongeza jitihada za Chadema, kwenye kampeni zao za uchanguzi, Watanzania tumekuwa tukifuatilia maoni na mapendekezo ya Watanzania wanaopenda mabadiliko ya uongozi wa taifa letu.
Hali kwa sasa siyo shwari hata kidogo ndani ya ccm, kwa sasa zaidi ya magari 200 ya serikali yamebadilishwa namba na kuwekwa namba za kiraia na yapo kwenye kampaini za ccm, malipo yote ya pesa serikalini yamesimamishwa, pesa zinapelekwa kwenye uchaguzi.
RUSHWA na USHIRIKINA ni sehemu ya kampeni za CCM.
Watanzania wenye hofu ya Mwenyenzi MUNGU, naomba tufanye kitu kimoja, na hakika kwa umoja wetu tutafanikiwa, na itakuwa ni hatua yetu muhimu ya kusonga mbele kwa kishindo tukielekea siku ya uchanguzi siku 42 zijazo kuanzia leo.
1) Tumuwezeshe Dr. Slaa, wabunge, madiwani wahitimishe mikutano yao ya ushawishi wa kuchanguliwa kwa kishindo.
2) Taratibu za kuwapata mawakala waaminifu zianze sasa kwenye kila kijiji, tarafa, wilaya, mkoa na taifa.
Kila jambo jema lina gharama zake, tusibweteke kwa juhudi za mtu mmoja, kila mtu kuanzia sasa ajihesabu kuwa sehemu ya mafanikio ya kuleta matumaini mapya kwa jamii ya Watanzania.
Kama upo tayari kuwa sehemu ya ushindi fanya jambo moja sasa kati ya haya:-
1) Changia CHADEMA kwa kianzio cha shilingi zisizopungua 10,000/=
2) Shawishi watu 10 kwa kuwatembelea, kuwapia simu au watumie SMS nao wachangie kwa kiwango cha 10,000/= au zaidi.
Account za Benki
CHADEMA-M4C CRDB 0J080100600
CHADEMA NMB 2266600140
Weka kwenye tawi lolote la benki hizi nchini
Changia kwa simu (SMS)
Tuma neno:
"SLAA" kwenda namba 15710
"CHADEMA" kwenda namba 15710
"NAJIUNGA" kwenda namba 15710
Namba hizi ni kwa mitandao ya ZAIN, TIGO na VODA.
Kuchangia kwa njia ya M-PESA
0758 223344
0764 776673
ZAP 0789 555333
Unaweza kuhakiki uhalali wa namba zao hapa:
Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Tunategemea JF pekee watashawishi watu 1,000,000 katika siku hizi 42 zilizobaki zitakazompa Dr Slaa mtaji wa zaidi ya shilingi bilioni 10 pamoja na kumpa kura ya ushindi ya NDIYO.