Ndio mapenzi ya kisasa au ananipotezea muda?

Ndio mapenzi ya kisasa au ananipotezea muda?

Habari ya kweli; Jirani yangu mmoja alikuwa na familia nzuri tu, mke na mtoto mmoja, tukakaa nao karibu tu kwa muda halafu mama akawa mja mzito. Jamaa alikuwa na gari muda mrefu tu, wana kazi wote wawili, mke alipokaribia kujifungua akamwomba mke wangu amfichie kahela kake. Akamwomba kuwa hata akija ana shida gani asimpe mpaka siku ya kwenda kujifungua.
Alipomwuliza kwa nini shoga? Akamjibu kuwa hiyo ni hela ya kukodisha gari la mumewe siku atakaposhikwa uchungu. Ikaja siku ghafula akaona ka ndio uchungu, kumbe haukuwa wa kweli, lakini alipelekwa hospitali na ilikuwa usiku, asubuhi akaja omba ile hela shs Elfu hamsini. Aliichukua analia kabisa. Mke wangu alipo muuliza kwa nini akasema ameambiwa alipe kwa kukodisha gari hilo .
Wiki iliofuata ukawa uchungu wa kweli, na ile hela imeshatumika, ikawa kilio, gari haitoki mpaka atoe nauli, mbona ilibidi nitoe gari yangu kumpeleka hospitali mama wa watu. Alipojifungua ikabidi tuwakalishe kikao kwa nguvu na matishio kuwa bwana asipokuja tunamhamisha mtaa.
Ilikuwa aibu ya mwaka mama alivyoeleza jinsi anavyo nyanyaswa na hilo lidubwana. Hata kwenda kazini lazima alipe nauli ya mwezi kabla. Ofisi zipo karibu lakini hata lunch hampi. Matumizi ya home wachangie sawa kwa sawa.
Dada, angalia, huyu wako asijekuwa ni wa dizaini hii. Kaa chonjo, usikimbilie harusi ujekuta ni dubwana badala ya bwana.
 
Huna chako hapo bi dada....jipange upya...ana gari hata kukurudisha kwako anashindwa???wengine wana miguu tu na wanasindikiza wapenzi wao!!
 
Pole sana mkuu KATOTY kwa yote yaliyokufika. Kwanza kabisa unapaswa kumshukuru Mungu kwa kukujalia uwezo wa kugundua mapungufu ya mpenzi wako maana si wote ambao wana uwezo wa kung'amua mapungufu ya wapenzi wao.

Kutokana na maelezo yako hapo juu binafsi mimi nakushauri kwanza ujaribu kukaa chini na mpenzi wako mpate kuzungumza na umweleze namna ambavyo hupendezwi na tabia yake na namna ambavyo unatamani awe au akutendee. Kama anakupenda kweli nina imani atakusikiliza na atajirekebisha.
 
Last edited by a moderator:
usiite stori bali ni riport ya ukwelii. And tell yu what, bado wanakaa pamoja hata leo lakini sijasikia tena yanayoendelea humo ndani kwao kwani wameamua kujitenga nasi

ni bora bidada ajihadhali kabla ya hatari
 
Na umejitahd kuvumilia my dia!khaa hlo ni zaid ya bahili,atakupa tabu mbelen
 
sasa kama mwanaume hakusaidii kwa lolote na wewe unahitaji msaada hata hela ya tax hakupi kwake unafuata nini?

Hiyo trela sinema yenyewe bado. kachunguze S4 yake ina password. Kuna mipicha kapiga na wenzako. na mtu wa aina yake anakutumia tu kwa faida yake. imagine anaongiza midola kibao na hakusaidii unasubiri nini. chapa lapaaaaaa

Hili ndilo la maana. Maadili hayazuii kutoa hela kwa mtarajiwa wako. GUMEGUME hilo chapa lapa halina maana hilo.
 
Its funny how you actually mean something to someone and they just turn around and prove you wrong......he is not that into you girl.....he doesnt knw ur worth (on to the next one).
 
Back
Top Bottom