dm2000inter
Member
- Oct 27, 2010
- 29
- 10
Hili tukio halina tofauti na lile la mwaka 2000 ambapo Mfanyabiashara Jaffar Abubakar amabaye alikuwa ni swahiba wa RPC Kilimanjaro wakati ule Mohamed Chicco na IGP Omar Mahita, alimuua bwana mmoja kwa kumfunga kamba mikononi, kumwagia mafuta ya taa kisha kumchoma moto. Yule bwana aliungua kwa asilimia 75 baadae akafa. Polisi wakatoa Press Release kuwa ameuawa na wananchi wenye hasira kali. Tunalishukuru Gazeti la Mwananchi lililia na kashfa hii hadi DCI wakati ule Adad Rajabu akaagiza kufanyika kwa uchunguzi upya bila kuwashirikisha Polisi Kilimanjaro na ushahidi mzito ukapatikana lkn bahati mbaya mtuhumiwa alikuwa ametorokea nje ya nchi na hadi leo anaswakwa na Interpol. Case ile haina tofauti na hii. Ushahidi ulivurugwa kwa makusudi. Leo polisi wanashikwa na kigugumizi kuwakamata watuhumiwa lkn najiuliza hivi hao ndugu wakafikia kikomo cha uvumilivu wakaamua kujichukulia sheriw mkononi mtawalaumu? IGP Mangu, hebu onyesha watanzania kuwa hili lililofanywa na ofisi ya RCO Kilimanjaro ni uhuni,hukubaliani nao na wachukulie hatua walioshirili ufisadi huu ili kurejesha heshima ya jeshi la polisi.