Halafu huyu ndio KATIBU MKUU wa ACT.Msiige nchi za magharibu yaani kitila na udokta wako unadiriki kutetea ushoga?kweli umekosa busara.nilitegemea ungelaani kitendo hicho kumbe wewe ni wale wale mliokunywa uji wa mgonjwa?
akiojiwa na charles hilary wa bbc, amemponda mseveni kuwa ana mapungufu hivyo kataka apate umaarufu kwa kupinga ushoga. Mimi nimejiuliza maswali mengi, kwa kuwa mseven ni dhaifu kwenye utawala wa kidemokrasia, ni dikteta basi ata ushoga aukubali? Mimi binafsi nimemuona dr kitila hamnazo. Ata kama mseven ana mapungufu, je ili la ushoga kafanya vibaya? Nakumbuka humu jf, watu wengi tumekuwa tunamponda mh rais kwa mambo mengi, lakini alipomshauri kagame aelewane na wapinzani, watz wengi tulimsapoti na ata wanyarwanda walivoanza kumshambuli Rais, wengi tulikuwa nyuma ya rais wetu. Je kitila alitaka M7 aruhusu ushoga? Kwa ili ya ushoga dr kitila huko peke yako labda wale masalia wako.
Najua mnamuogopa sana Kitila Mkumbo, kwahiyo mnajitahidi sana kumchafua kwa lolote mnaloweza.
Chadema inapewa msaada na Chama cha Ujerumani kinachoamin ushoga mbona hamtoi tamko kukataa mamilioni hayo.
Wanafiki wakubwa nyie.
utake usitake ushoga ulikuwepo! Upo! Na Utakuwepo! Hata tuweke sheria ima tusiweke! Alichofanya mseve ni kutafuta umaarufu na sifa zisizo na faida kwake wala wananchi wa Uganda! Kwani angefunika kombe yapite kungekuwa faida zaidi!amesema,"viongozi wa africa wanajivika ujasiri wasiouweza" hapa ina maana anashabikia ushoga na hakubaliani na Museveni kusaini, ameiaibisha Tanzania na taaluma yake na chuo chake.
Kwa bahati mbaya, ujumbe mzima (kamili) wa Dr. Kitilla umepotea kwa wengi kutokana na jazba kubwa kuhusu ushoga. Ni kweli kuwa ushoga haueleweki wala kukubalika kwa wengi wetu. Lakini upande muhimu wa ujumbe wa Dr. Kitilla ni jinsi wanasiasa wa ovyo kama Museveni wanavyoweza kuchukua kete hiyo MOJA TU kujipandisha chati ghafla. Kwenye mikakati ya kisiasa, mtu wa aina hiyo tunamuita "a political genius". Mtu ajikombe kwa mataifa makubwa kwa vitu vyote na kukandamiza watu wake kisha akurupuke dakika za majeruhi na kupitisha sheria dhidi ya ushoga na kuishia kuoneka "shujaa wa kipekee" barani Afrika! Kwa hulka hiyo ya mitazamo finyu, tutaendelea kuwakabidhi ikulu zetu "watoto wa mjini" ambao nao hawatakuwa na hiyana kuendelea kutuhenyesha bila simile.
Natumaini mnaomshambulia Dr. Kitilla ikitokea hapa TZ CCM wakiandika rasmi kwenye ilani yao ya uchaguzi mwaka 2015 kuwa wakiingia madarakani jambo la kwanza ni kutunga sheria ya kunyonga mashoga wote nchini basi mtahamishia kura zenu kule kwani kwa tafsiri nyepesi, vyama vingine visivyo na kipengele hicho manake "vinaunga mkono" ushoga! Kama ni hivyo, ni bora tuanze kumuuliza kila mwanasiasa anayetaka madaraka nchini ana msimamo gani kuhusu ushoga ili mambo yawe bayana mapema kabisa.
utake usitake ushoga ulikuwepo! Upo! Na Utakuwepo! Hata tuweke sheria ima tusiweke! Alichofanya mseve ni kutafuta umaarufu na sifa zisizo na faida kwake wala wananchi wa Uganda! Kwani angefunika kombe yapite kungekuwa faida zaidi!
Na pia hayo matatizo mengi hayahalalishi ushoga...tuachane ushabiki wa kisiasa bwana mkumbo hajakosea hata kidogo , suala la ushoga bwana mseveni analitumia km his plolitical will.
.
africa kuna matatizo mengi sana ushoga haundoi matatizo yetu..
Huyu jamaa ( Dr. Kitila Mkumbo ) hafai kabisa ndio maana hata watani zangu chadema wamemfukza. Katika maisha kuna maswala yanayohtaji suluhu ya haraka kulinda heshima ya jamii. Na kuna mipango ya mda mrefu. Sidhan kwamba unaweza kushughulkia matatizo mengine wakati kuna swala linalomomonyoa maadili. Huyu sijamwelewa kabisa
Nimekuelewa saana ulichokisema .. !
kwa vile uliangalia mahojiano hayo ww binafsi , basi ni lazima ukubaliane na mm kua Mtikila alishindwa kuonyesha msimamo wake juu ya swala la ushoga .. !
Huwezi niambia tunamshambulia Mtikila kwa sababu wengi tunauchukia ushoga laa.
Mtukila
Dk. jana sidhni kama aliongea na kuonyesha nn anasema .. !
Na sidhani kama Dk alitakiwa kua neutral kwnye swala hili .. !
Na pia alionyesha kumyooshea kidole Museven na kumlaumu indirect kwa maamuzi aliyoyachukua ..
Najua mnamuogopa sana Kitila Mkumbo, kwahiyo mnajitahidi sana kumchafua kwa lolote mnaloweza.
Chadema inapewa msaada na Chama cha Ujerumani kinachoamin ushoga mbona hamtoi tamko kukataa mamilioni hayo.
Wanafiki wakubwa nyie.
funguka Mkuu tuelimishane isiwe Taboo!Daa!!! hataree.