Ndani ya BBC: Kitila Mkumbo atetea 'Ushoga'

Ndani ya BBC: Kitila Mkumbo atetea 'Ushoga'

Nelson Kileo

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2011
Posts
3,054
Reaction score
3,263
Akiwa anaongea kwenye mahojiano moja kwa moja na mtangazajiwa BBC SAHILI Charles Hillary ...

Dk Mkumbo ameonekana akiutetea ushoga na kusema Museven kajivika ubabe aisiokua na uwezo nao .. Ni baada ya kuulizwa anaonaje issue juu ya Uganda na misaada iliyozuiwa na world bank baada yakupitishia sheria kali ya kuzuia ushoga ..

Kitila mkumbo kwa jinsi aliivyoongea ananyesha kabisa kwamba ni lazima nchi za Africa kuukubali ushoga .



============================
Ufafanuzi toka kwa Dr. Kitila Mkumbo
============================

Tusipotoshe. Katika mazungumzo yangu sikutetea wala kupinga ushoga kwa sababu hiyo haikuwa mada. Nilichosema:

i) Misaada kutoka nchi za magharibi huambatana na masharti. Masharti mengi yanalenga katika kuchochea utawala bora hasa ukilenga kukuza demokrasia ya kimagharibi na kulinda haki za binadamu. Moja ya haki ambazo zinalindwa sana na nchi za kimagharibi ni haki za wapenzi wa jinsi moja.

Kwa hiyo ilitarajiwa kwamba nchi hizo zingeikatia misaada nchi ya Uganda pale ambapo Rais Museveni angesaini sheria inayotoa adhabu kali kwa wapenzi wa jinsi moja. Nikasisitiza hakuna njia ya kukwepa masharti haya kama nchi za kiafrika zitaendelea kutegemea misaada kutoka magharibi. Hatuwezi tukala keki na tukawa nayo at the same time.

ii) Viongozi wa kiafrika wanapenda kujivika ujasiri bandia katika mambo yasiyo na tija. Katika bara la Afrika kuna matatizo mengi na makubwa zaidi kuliko ushoga. Lakini wanatumia kadi ya ushoga kwa sababu ni swala gumu katika bara la Afrika ili kujipatia umaarufu hewa. Ushoga haliwezi kuwa tatizo kubwa kuliko rushwa na wizi wa raslimali unaoendelea bara la Afrika.

Rais Museveni ana matatizo makubwa ya kiutawala na hali yake kisiasa si njema kuelekea uchaguzi wa mwaka 2016 na anatumia hili la ushoga ili kujikweza na kujiweka sawa katika kuwasaulisha waganda matatizo ya kisiasa na kiuchumi yaliyosababishwa na utawala wake. Anatumia pia kadi ya ushoga ili aendelee kugombea kiti cha urais wakati alipaswa kuondoka juzi.

Bahati mbaya mawasiliano yalikatika na nikaishia hapo.
 
Nimeangalia huyo mwanazuoni alivyojibu hoja kama ilivyoelekezwa kwake na Bw Charles Hilary kuhusu athari za sheria ya ushoga Uganda.
Nikajiuliza umakini wake una kiwango gani kama hata vitu vidogo kama maoni ya kunyimwa misaada yanawezaje kuathiri Nchi hana majibu sahihi!
 
Unasahau ya kwamba kuwa Prf,sio kuwa na akili nyingi na busara
 
akiojiwa na charles hilary wa bbc, amemponda mseveni kuwa ana mapungufu hivyo kataka apate umaarufu kwa kupinga ushoga. Mimi nimejiuliza maswali mengi, kwa kuwa mseven ni dhaifu kwenye utawala wa kidemokrasia, ni dikteta basi ata ushoga aukubali? Mimi binafsi nimemuona dr kitila hamnazo. Ata kama mseven ana mapungufu, je ili la ushoga kafanya vibaya? Nakumbuka humu jf, watu wengi tumekuwa tunamponda mh rais kwa mambo mengi, lakini alipomshauri kagame aelewane na wapinzani, watz wengi tulimsapoti na ata wanyarwanda walivoanza kumshambuli Rais, wengi tulikuwa nyuma ya rais wetu. Je kitila alitaka M7 aruhusu ushoga? Kwa ili ya ushoga dr kitila huko peke yako labda wale masalia wako.
 
Nimeangalia huyo mwanazuoni alivyojibu hoja kama ilivyoelekezwa kwake na Bw Charles Hilary kuhusu athari za sheria ya ushoga Uganda.
Nikajiuliza umakini wake una kiwango gani kama hata vitu vidogo kama maoni ya kunyimwa misaada yanawezaje kuathiri Nchi hana majibu sahihi!

Ina maana hujui madhara watakayopata Uganda kwa kunyimwa hiyo misaada?You must be one those uninformed Chadema supporters whose decision making is ruled by emotions and not reasoning or rationale.Uganda waliahidiwa kupewa karibu dollar million 90 kwaajili ya mradi wa afya je unadhani Uganda watapata wapi pesa kufidia kiasi hicho cha pesa walichoahidiwa na World Bank (USA Agency) ili kuendelea na miradi ya afya waliyokwishaipanga?However i still support Museven decision to sign a bill that bans a same sex marriage in Uganda.
 
amesema,"viongozi wa africa wanajivika ujasiri wasiouweza" hapa ina maana anashabikia ushoga na hakubaliani na Museveni kusaini, ameiaibisha Tanzania na taaluma yake na chuo chake.
 
Akiwa anaongea kwenye mahojiano moja kwa moja na mtangazajiwa BBC SAHILI Charles Hillary ...
Dk Mkumbo ameonekana akiutetea ushoga na kusema Museven kajivika ubabe aisiokua na uwezo nao ..
Ni baada ya kuulizwa anaonaje issue juu ya Uganda na misaada iliyozuiwa na world bank baada yakupitishia sheria kali ya kuzuia ushoga ..

Kitila mkumbo kwa jinsi aliivyoongea ananyesha kabisa kwamba ni lazima nchi za Africa kuukubali ushoga .
kanjanja@work.com
 
nimemsikia mwanzo mpaka mwisho mawasiliano yakakatika,Sijasikia Dr.kitila eti anatetea ushoga.amesema viongozi wa Afrika wanajivika ubabe kwa vitu ambavyo hawaviwezi.m7 amesaini sheria utadhani kweli Uganda haihitaji misaada ya wazungu,tayari analalamika kua jumuia ya kimataifa imesaliti uganda.Alijipangaje kuishi bila misaada?hii ndio ilikua hoja ya Dr. kitila sema mawasiliano na BBC yakakatika.Acheni chuki wadau,jamaa kaongea vizuri na hajatetea mashoga.
 
Nadhani nyote nyie, kwa vile mnaongozwa na hisia, mkiona au kusikia mtu anasema kwamba watu wasipangiwe maisha yao mnamuona mtu huyo kana kwamba anatetea ushoga wakati ukweli wa mambo ni kwamba anatetea uhuru wa watu binafsi kujiamulia namna ya kuishi maisha yao.
 
Akiwa anaongea kwenye mahojiano moja kwa moja na mtangazajiwa BBC SAHILI Charles Hillary ...
Dk Mkumbo ameonekana akiutetea ushoga na kusema Museven kajivika ubabe aisiokua na uwezo nao ..
Ni baada ya kuulizwa anaonaje issue juu ya Uganda na misaada iliyozuiwa na world bank baada yakupitishia sheria kali ya kuzuia ushoga ..

Kitila mkumbo kwa jinsi aliivyoongea ananyesha kabisa kwamba ni lazima nchi za Africa kuukubali ushoga .

Wacha kupotosha wewe,wakati anaongea tupo na kaeleweka kama unataka kuwavuta wasomaji ili nawe uonekane umeandika sawa lkn Dk hakutetea ushoga kabisa,kazungumzia suala zima la misaada tunayopewa AFRIKA na viongozi wengi wanavyoogopa kutoa maamuzi kwa kuogopa kunyimwa misaada,na zaidi kaongea kuwa yaonekana museven kasain kwa vile amebakisha mwaka na nusu kuondoka madarakani na sio huo upotoshaji wako,kwanza kichwa cha habari na ulichoandika ni tafauti.
 
Nimeangalia huyo mwanazuoni alivyojibu hoja kama ilivyoelekezwa kwake na Bw Charles Hilary kuhusu athari za sheria ya ushoga Uganda.
Nikajiuliza umakini wake una kiwango gani kama hata vitu vidogo kama maoni ya kunyimwa misaada yanawezaje kuathiri Nchi hana majibu sahihi!

Hv kumbe swali lilikuwa hivyo!
Nimefungulia TV yangu nikasikia tu anajibu sikuelewa ameulizwa nini. Kama ni hivyo hakujibu hilo swali aliloulizwa kabisa.
 
akiojiwa na charles hilary wa bbc, amemponda mseveni kuwa ana mapungufu hivyo kataka apate umaarufu kwa kupinga ushoga. Mimi nimejiuliza maswali mengi, kwa kuwa mseven ni dhaifu kwenye utawala wa kidemokrasia, ni dikteta basi ata ushoga aukubali? Mimi binafsi nimemuona dr kitila hamnazo. Ata kama mseven ana mapungufu, je ili la ushoga kafanya vibaya? Nakumbuka humu jf, watu wengi tumekuwa tunamponda mh rais kwa mambo mengi, lakini alipomshauri kagame aelewane na wapinzani, watz wengi tulimsapoti na ata wanyarwanda walivoanza kumshambuli Rais, wengi tulikuwa nyuma ya rais wetu. Je kitila alitaka M7 aruhusu ushoga? Kwa ili ya ushoga dr kitila huko peke yako labda wale masalia wako.

Kama ndivyo hivyo naona Dr. Kitila sasa hatumii akili ameamua kutumia kitu kingine kabisa. aliandaa waraka wa siri ndani ya chama chake akajitetea kuwa siyo kitu kibaya tukamwacha. sasa anataka kutuambia kuwa ushoga ni poa, hakika sasa tumetambua kuwa Dr. Kitila hamnazo kabisa
 
Hata ukisaini Ant gay..... haisaidii kitu endapo tu mashoga wapo.
Tanzania gays wapo. Uganda wapo. Aamue(m7) kuanzia leo shoga apigwe risasi na sio kumwaga wino
 
Msiige nchi za magharibu yaani kitila na udokta wako unadiriki kutetea ushoga?kweli umekosa busara.nilitegemea ungelaani kitendo hicho kumbe wewe ni wale wale mliokunywa uji wa mgonjwa?
 
Back
Top Bottom