Ndani pachungu

Ndani pachungu

Majibu ya mitihani yao yakishatoka hautawaona tena hapo, maana wataona aibu kuja na zero zao.
 
Naishi na mume na mtoto wa wifi angu ana 26 miaka kaja kurudia mtihan
Kweli ananinyima usingizi bint hataki umwambie chochote akikosea ukimrekebisha ananuna anisemesh

1) ana group la wanafunzi wenzie wakija kusoma mpaka unaona aibu mavazi waliyovaa yaajabu ..maongez yao niyawanaume tu nikampiga marufuku mbele ya mjomba wake hawa mabint Kama hawana nguo nzuri za kuvaa nisiwaonde ndan kwangu...
alinuna wiki nzima, mama mkwe alipokuja kutusalimia ambae Ni bibi yake kamlea akaanza kuwaleta tena nilivyomkataza alizila kula wiki siku 2 mama mkwe akanichukia

2) anakibur yan usimwambie hata fanya usafi anataka yeye ndie apange kila kitu ndan akikosea usimwambie kitu
Mbaya zaidi mme wangu yaan nimpole kupita maelezo ambae hawez kuongea wala kukemea kitu yan hata kwangu nimtu asieweza kabisa
Bint anaweza rudi ata usiku mjomba wake anaishia kuguna tu
Nimejaribu kumweleza tabia ya mwanae lkn ananyamaza tu
Sijui nifanyeje jmn
Dada mbona unajipa presha kwa mambo ambayo haykuhusu, achana nae , wahusika wake wakuu wameachana nae we unataka kujipa presha , maisha yenyewe mafupi haya mpuuzie tu
 
There is this Poem which mirrors exactly the societal differences we are undergoing, "A Freedom Song'" by Marjorie Oludhe Macgoye...............
"Since she’s my sister’s child
Atieno needs no pay
While she works my wife can sit,

Atieno’s sly and jealous
Bad example to the kids,

That girl stays too long at market
Who will teach her what is right?,

Atieno’s soon replaced
Meat and sugar more than all
She ate in such a narrow life
Were lavished in her funeral
Atieno’s gone to glory
Atieno yo."
A perfect reflection of the societal differences in our communities. Man thanks for this~Dem old days Atieno yo
 
Sijui nifanyeje jmn
Dada hapa umetaja watu watatu waliozidi umri wa 18 years. Na wote kwa mtazamo wako kwenye hili swala hawako sawa. Mume ulimchagua mwenyewe kwa mema uliyoona mbele zake. Kama basi nasaba ya kwao yote imeenda against wewe kwenye swala hilo tatizo obvious ni wewe. Labda kwa namna unayomwambia si sawa. Labda kuna unayoficha kuhusu scenario nzima. Labda ulionesha wazi kutokupenda yeye kuishi hapo. Huyo si mwanao. Jaribu kumuelewesha kistaarabu. Kama hajajisikia kufanya kazi na kwao wanaona sawa basi jitahidi umvumilie maana ndo tabia za kwao tena na wewe ushaolewa huko. Mara nyingi sana wanawake wanaosema waume zao ni wapole mno ndo wale ambao hawasikilizi chamume na wanacotrol balaaa!
 
Miaka 26, umri wa mke wa mtu kabisa huo.... No wonder anakiburi. Weka camera kisirisiri maeneo ya nyumbani kwako hata mmeo asijue, utaujua ukweli tuu.

Matata K.
 
Hii hali ilimkuta rafiki yangu, mtoto wa wifi alikuwa ameota mapembe nyumbani kwake. Tukimaliza kazi hataki kurudi nyumbani. Nilikuwa ninampa moyo arudi kwani nyumba ni yake na ana watoto wadogo.

Anaweza kufika nyumbani binti hajapikaw chochote, watoto wamelishwa cornflakes. Anaanza kutoa nyama saa mbili ili mume wake na watoto wapate a proper meal.

Yule binti aliolewa, huko kwa mume nae anaipata fresh.
 
Yeye ndio kawa Kama mwenye nyumba yan Mimi nifate anavyotaka akifanya kitu usiniulize ...ukimwachia hela ya matumiz usimuulize chenji ananuna hajibu nami nashinda kazin
Simple tu, ukitoka job pita sokoni kununua vya km ni mboga ya kesho. Asb pakikucha hakuna kuacha ht senti.
 
Yeye ndio kawa Kama mwenye nyumba yan Mimi nifate anavyotaka akifanya kitu usiniulize ...ukimwachia hela ya matumiz usimuulize chenji ananuna hajibu nami nashinda kazin
Piga kimya, Kama Ni pesa ya matumizi ya nyumbani usimpe, hakikisha kila kitu kipo ndani.
 
Kwa mara ya kwanza naona watu wamekuja kutoa ushauri bila kejeli na masimango.
Hongereni sana
Ni kwa sababu kwenye hiyo ndoa anateseka mwanamke kwahiyo inaonekana kawaida ila angekuwa anateseka mwanaume ungeshasikia kauli kama "wanawake ni mashetani" mara "wanawake wa siku hizi hawafai kwa kuoa ni wa kupiga na kusepa tu" na mambo kama hayo
 
Cha kufanya acha roho mbaya.

Tafuta kazi ya kufanya uwe busy sana.

Acha mdomo..

Acha kushindana na watoto wadogo...

Acha kumfunda sio mtoto huyo ni mtu mzima mwenzako.

Mpunguzie mumewe drama ametoka kazini kachoka hataki kusikia upuuzi wa kike kike..

Ukiweza kufanya hayo basi amani itarudi kwa kasi na mtaishi km mtu na mdogo wake.....
 
Back
Top Bottom