Hii nlishakutana nayo nliletewa Mtoto wa ndugu yangu nikae nae wee akapata marafiki konki wale wa kinondoni watoto wadogo wa cheza chura wakapewa jina utumbo ndizi, nliwatimua hao mashoga bint kapiga simu kwa mama yake, naona nkimpigia simu mama yake hapokei, kumbe kamind.
Nikaona isiwe tabu nikaset ground rules zangu, jioni narudi nawakuta wamejazana sebuleni singeri sauti juu nikatimua.
Mtoto akamind namnyanyasa and the like ataondoka, kanunua akatoka imefika saa 2 usiku nafatwa na marafiki zake Mtoto ametekwa na kisu eti niwatume vijana wakamuokoe, vijana waliokuwepo wakataa, ikabidi sasa nisimame kama Shangai niwaamuru waende kumuokoa asije fanyiwa mabaya.
Mambo mengi ila mwisho nlimpaki kwa mama yake mpaka sasa mama yake hatupo karibu tunakutana tu kwenye issues ila hatupigiani simu wala nini.
Ndugu lawama nachokuambia wewe weka sheria zako azifate basi ukimchekea atakuharibia nyumba, nyumba ni ya mwanamke si mwanaume na Mtoto akiharibika lawama ni za mwanamke si mwanaume.