Ndalichako mbuzi wa kafara?

Ndalichako mbuzi wa kafara?

Mwanamume

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2013
Posts
269
Reaction score
216
Tangu kutolewa kwa matokeo ya wahitimu wa kidato cha nne 2012 kumekuwa na maoni mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumtaka Katibu Mkuu Mtendaji wa NECTA, Ndalichako, ajiuzuru. Leo naomba wanaJF tulidadavue hili kwa kina. Kwani nionavyo mm huyu mama hana kosa lolote, wala hakuchangia hata chembe ktk kufeli kwa wanafunzi hao. Huyu ni muonjaji tu wa pishi lililoandaliwa na Kawambwa kupitia wizara anayoiongoza. Alipoonja katoa majibu kuwa pishi halijaiva. Ni jukumu letu watz kuwahoji wapishi kupitia mpishi mkuu Kawambwa kuwa kwanin kaipua pishi lisiloiva vema?

Ningelikuwa mm ndiyo Kawambwa siku nyingi sana ningekuwa nimeachia ngazi. Pengine Kawambwa anashindwa kufanya hivyo kwa sababu zifuatazo.

a) Atakuwa amemsaliti aliyemteua ( rais wa nchi) ambaye ametamka wazi kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa 2 kuwa hajui sababu za kufeli F4. Sasa kama mkuu wa nchi hajui Kawambwa naye hawezi kujiuzulu kwa kuwa bila shaka naye atajifanya hajui?

b) Atakuwa amekisaliti chama chake. Ikumbukwe kuwa hizi social clubs ambazo zilibatizwa jina la sekondari za kata ilikuwa ni karata ya kisiasa ya CCM, ili kuonyesha kuwa wanakuza elimu nchini wakati wanajua kuwa shule hizo hazina KILA KITU cha kuzifanya ziitwe shule.

Hivyo Kawambwa kujiuzuru ktk mazingira kama hayo unahitajika moyo wa kishujaa kama wangu.

Hata hivyo, wazazi na jamii ya watz kwa ujumla hatukwepi lawama hizi hata kidogo. Tukubali kabisa kwamba kabla hatujamnyooshea Kawambwa ama mtu mwaingine tujinyooshee sisi wenyewe kwanza. Kwanini?

1.Mafataki ndiyo sisi wenyewe tunaowapotosha watoto wetu kingono. Unamlaumu Ndalichako?

2.Kwanin hatukuhoji na kuandamana wakati ule serikali inatuhimiza tupeleke watoto wetu, tena wasiojua kusoma na kuandika ktk majengo yaliyobatizwa majina ya sekondari? Tulitegemea matokeo yapi hapo? Unamlaumu Ndalichako?

Mtoto wako ana simu nzuri kama vile anafanya kazi ikulu. Humuulizi katoa wapi? Mwanao anarudi nyubani saa 4 usiku kila siku eti katoka tuisheni. Husituki tu? Mwanao anasuka nywele kama vile anakwenda kufanyiwa sendoff. Huoni? Kule vijijini mtoto kapanga uswazi, mazingira duni halafu na msosi ni wa kugongea. Atafaulu huyo? Mwano anaongea na simu usiku kucha na mabwana wenye umri mkubwa kuliko babake. Hamuoni? Mnamlaumu Ndalichako? Kuna watoto wanaingia ubia na makonda ili wapate unafuu wa nauli, mwishoe wanakuwa nyumba ndogo au kubwa ya konda. Hamlijui hilo?

Shule za mission hakuna ujinga kama huo. Mwanafunzi wa kike ama wa kiume wote wananyoa nywele, hakuna kumiliki simu shuleni, hairuhusiwi kuwa na nguo za nyumbani shuleni. Halafu wote boarding.

Tunatafuta mchawi ktk hilo? Tunaunda na tume? Nipeni mimi hiyo hela. Nikisikia Ndalichako anatjwa kuhusika ktk kufeli f4 roho inaniuma, na ninapata hisia kuwa anatolewa kama kafara ili kulinda mapapa walio madarakani. Kawambwa umenisikia?
 
Tangu kutolewa kwa matokeo ya wahitimu wa kidato cha nne 2012 kumekuwa na maoni mbalimbali ikiwa ni pamoja na kumtaka Katibu Mkuu Mtendaji wa NECTA, Ndalichako, ajiuzuru. Leo naomba wanaJF tulidadavue hili kwa kina. Kwani nionavyo mm huyu mama hana kosa lolote, wala hakuchangia hata chembe ktk kufeli kwa wanafunzi hao. Huyu ni muonjaji tu wa pishi lililoandaliwa na Kawambwa kupitia wizara anayoiongoza. Alipoonja katoa majibu kuwa pishi halijaiva. Ni jukumu letu watz kuwahoji wapishi kupitia mpishi mkuu Kawambwa kuwa kwanin kaipua pishi lisiloiva vema?
Ningelikuwa mm ndiyo Kawambwa siku nyingi sana ningekuwa nimeachia ngazi. Pengine Kawambwa anashindwa kufanya hivyo kwa sababu zifuatazo.
a) Atakuwa amemsaliti aliyemteua ( rais wa nchi) ambaye ametamka wazi kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa 2 kuwa hajui sababu za kufeli F4. Sasa kama mkuu wa nchi hajui Kawambwa naye hawezi kujiuzulu kwa kuwa bila shaka naye atajifanya hajui?
b) Atakuwa amekisaliti chama chake. Ikumbukwe kuwa hizi social clubs ambazo zilibatizwa jina la sekondari za kata ilikuwa ni karata ya kisiasa ya CCM, ili kuonyesha kuwa wanakuza elimu nchini wakati wanajua kuwa shule hizo hazina KILA KITU cha kuzifanya ziitwe shule.
Hivyo Kawambwa kujiuzuru ktk mazingira kama hayo unahitajika moyo wa kishujaa kama wangu.
Hata hivyo, wazazi na jamii ya watz kwa ujumla hatukwepi lawama hizi hata kidogo. Tukubali kabisa kwamba kabla hatujamnyooshea Kawambwa ama mtu mwaingine tujinyooshee sisi wenyewe kwanza. Kwanini?
1.Mafataki ndiyo sisi wenyewe tunaowapotosha watoto wetu kingono. Unamlaumu Ndalichako?
2.Kwanin hatukuhoji na kuandamana wakati ule serikali inatuhimiza tupeleke watoto wetu, tena wasiojua kusoma na kuandika ktk majengo yaliyobatizwa majina ya sekondari? Tulitegemea matokeo yapi hapo? Unamlaumu Ndalichako?
Mtoto wako ana simu nzuri kama vile anafanya kazi ikulu. Humuulizi katoa wapi? Mwanao anarudi nyubani saa 4 usiku kila siku eti katoka tuisheni. Husituki tu? Mwanao anasuka nywele kama vile anakwenda kufanyiwa sendoff. Huoni? Kule vijijini mtoto kapanga uswazi, mazingira duni halafu na msosi ni wa kugongea. Atafaulu huyo? Mwano anaongea na simu usiku kucha na mabwana wenye umri mkubwa kuliko babake. Hamuoni? Mnamlaumu Ndalichako? Kuna watoto wanaingia ubia na makonda ili wapate unafuu wa nauli, mwishoe wanakuwa nyumba ndogo au kubwa ya konda. Hamlijui hilo?
Shule za mission hakuna ujinga kama huo. Mwanafunzi wa kike ama wa kiume wote wananyoa nywele, hakuna kumiliki simu shuleni, hairuhusiwi kuwa na nguo za nyumbani shuleni. Halafu wote boarding. Tunatafuta mchawi ktk hilo? Tunaunda na tume? Nipeni mimi hiyo hela. Nikisikia Ndalichako anatjwa kuhusika ktk kufeli f4 roho inaniuma, na ninapata hisia kuwa anatolewa kama kafara ili kulinda mapapa walio madarakani. Kawambwa umenisikia?

Acha porojo wewe,kama kweli tunaka wototo wetu wapte elimu bora ni lazima baraza la mitihani lote livunjwe na kuundwa tena katika mfumo ulio bora,pia wizara ya elimu ifumuliwe yote kuanzia waziri mpaka mfagizi,tutengeneze wizara ya elimu mpya, hii ni kwa dharura tu,suluhisho la kudumu ni kuvunja mfumo mzima wa serikali ya tanzania kuanzia raisi mpaka mfagizi,tujipange upya ili tijenge nchi yenye kueleweka
maana hivi sasa nchi hii inaongozwa na wanasiasa walioshindwa katika maisha ambao tunaweza kuwagawanya katika makundi makubwa matatu:

A.Kundi la wanasiasa walioshindwa katika elimu,kundi hili linaongozwa na wafuatao;
1.Freeman Mbowe
2.John Mnyika
3.Maji maarefu/Ngonyani
4.Suleimani Bungara(mbunge kilwa kusin-CUF)
5.Joseph Mbilinyi/sugu

B.Kundi la wasomi walioshindwa katika fani walizosomea.Kundi hili linaongozwa na wafuatao;
1.Prof.Lipumba
2.Padri Slaa
3.Prof.Muhongo
4.Dr.Kafumu
5.Prof.Magembe


C.Kundi la wafanyabiashara walioshindwa kuwanyonya zaidi watanzania wakiwa nje ya siasa.Kundi hili linaongozwa na wafuatao;
1.Rostam Azizi
2.Ndesamburo
3.Lowasa
4.Abood wa morogoro
5.Mohammed Dewji
6.Kinana katibu mkuu wa CCM

Kumbuka hao ni mifano tu,lakini kuna wengine wengi tu ambao unaweza kuwaongoza katika kila kundi.

Watu hawa ukiwaona na kuwasikiliza wanavyoongea na kutokwa na mapovu Bungeni na kwenye majukwaa ya siasa utazani wanitakia mema nchi hii kumbe wapo katika haraki za kutafuata neema za matumbo yao na familia zao baada ya kushindwa ndot zao katika maisha.

Sasa kama taifa linaongozwa na watu kama hawa tunategemea nini kama sio matokea mabaya kama haya,umasikini wa kutupwa,na kila njanga katika taifa hili
 
Acha porojo wewe,kama kweli tunaka wototo wetu wapte elimu bora ni lazima baraza la mitihani lote livunjwe na kuundwa tena katika mfumo ulio bora,pia wizara ya elimu ifumuliwe yote kuanzia waziri mpaka mfagizi,tutengeneze wizara ya elimu mpya, hii ni kwa dharura tu,suluhisho la kudumu ni kuvunja mfumo mzima wa serikali ya tanzania kuanzia raisi mpaka mfagizi,tujipange upya ili tijenge nchi yenye kueleweka
maana hivi sasa nchi hii inaongozwa na wanasiasa walioshindwa katika maisha ambao tunaweza kuwagawanya katika makundi makubwa matatu:

A.Kundi la wanasiasa walioshindwa katika elimu,kundi hili linaongozwa na wafuatao;
1.Freeman Mbowe
2.John Mnyika
3.Maji maarefu/Ngonyani
4.Suleimani Bungara(mbunge kilwa kusin-CUF)
5.Joseph Mbilinyi/sugu

B.Kundi la wasomi walioshindwa katika fani walizosomea.Kundi hili linaongozwa na wafuatao;
1.Prof.Lipumba
2.Padri Slaa
3.Prof.Muhongo
4.Dr.Kafumu
5.Prof.Magembe


C.Kundi la wafanyabiashara walioshindwa kuwanyonya zaidi watanzania wakiwa nje ya siasa.Kundi hili linaongozwa na wafuatao;
1.Rostam Azizi
2.Ndesamburo
3.Lowasa
4.Abood wa morogoro
5.Mohammed Dewji
6.Kinana katibu mkuu wa CCM

Kumbuka hao ni mifano tu,lakini kuna wengine wengi tu ambao unaweza kuwaongoza katika kila kundi.

Watu hawa ukiwaona na kuwasikiliza wanavyoongea na kutokwa na mapovu Bungeni na kwenye majukwaa ya siasa utazani wanitakia mema nchi hii kumbe wapo katika haraki za kutafuata neema za matumbo yao na familia zao baada ya kushindwa ndot zao katika maisha.

Sasa kama taifa linaongozwa na watu kama hawa tunategemea nini kama sio matokea mabaya kama haya,umasikini wa kutupwa,na kila njanga katika taifa hili

Unauhakika umeelewa hoja ya mtoa uzi au umekurupuka tu? Umewahi kusikia wapi ufumuzi kama unaoungelea wewe umetokea ndani ya chama tawala au unalopoka tu? Mtoa uzi ametoa point vizuri sana ila wewe unaonekana umeotoka kupata kidogo ndoo maana husomeki kabisa
 
Unauhakika umeelewa hoja ya mtoa uzi au umekurupuka tu? Umewahi kusikia wapi ufumuzi kama unaoungelea wewe umetokea ndani ya chama tawala au unalopoka tu? Mtoa uzi ametoa point vizuri sana ila wewe unaonekana umeotoka kupata kidogo ndoo maana husomeki kabisa

Fikra ngumu vilaza uwa hawazielewi
 
Pengine hujanielewa Ndg Nguvukazi mikono, naomba maelezo ya kina. Ndalichako na NECTA yake wamehusika vipi katika kufeli F4 wa 2012? Hao wadau wengine unaowaita serikali kupitia wizara ya elimu ndicho nilichoandika na nikaenda mbali zaidi kwa kuwaangushia lawama pia wazazi na watz wote. Soma tena uzi wangu. Nguvukazi mikono?
 
Wizara ya elimu yte kwa ujumla wake imepoteana mabadiliko yanahitajika lkn kwa upande fulan serikar inastahili lawama
 
Kama kweli tunamlaumu huyu mama kuwa naye anastahili kujiuzulu basi Watanzania uwezo wetu wa kufikiri una walakini. Baraza la Mitihani halina uhusiano na matokeo haya ya kidato cha nne. Wao hutunga na kusahihisha mitihani kadri walivyoelekezwa na wizara ya elimu (mhitasari wa ngazi husika). Kama mitihani ingevuja, basi lawama zingemwendea huyu mama. Fikiria kama ungekuwa wewe umeambiwa kuwa huu ndo mhitasari wa kidato cha nne na ukaombwa kutunga na kusahihisha mitihani hiyo kwa kufuata mwongozo huo (mhitasari) watoto wakafeli, je utalaumiwa hapa kwa lipi? wakati wanafundishwa hukuwepo, wakati wanaandaa mihitasari hiyo hukuwepo, hapo lawama inakuwa yakwako ki vipi?
 
Tunatafuta mchawi ktk hilo? Tunaunda na tume? Nipeni mimi hiyo hela. Nikisikia Ndalichako anatjwa kuhusika ktk kufeli f4 roho inaniuma, na ninapata hisia kuwa anatolewa kama kafara ili kulinda mapapa walio madarakani.

Nimesoma TOR za 'tume ya Pinda'. Ukiziangalia kwa makini zimejengwa kumng'oa Joyce Ndalichako kwa kigezo cha mapungufu ktk utungaji wa mitihani. Kawambwa atalindwa ( .. ni rafiki wa karibu wa JK), Ndalichako kafara.
 
Unauhakika umeelewa hoja ya mtoa uzi au umekurupuka tu? Umewahi kusikia wapi ufumuzi kama unaoungelea wewe umetokea ndani ya chama tawala au unalopoka tu? Mtoa uzi ametoa point vizuri sana ila wewe unaonekana umeotoka kupata kidogo ndoo maana husomeki kabisa
wewe ulishaona wapi elimu inashuka kwa ghafla hivo ndani ya mwaka mmoja.hiyo ni hujuma amefanya huyo mama,amefelisha watu kwa makusudi,na jibu litapatikana tu.subiri matokeo ya form six
 
ila unachotakiwa kufaham ni kwamba hao madogo waliofeli(KAFALA) ni muhimu kwa maisha yako ya kila siku kwani hao ndio wazoaj taka wetu mitaani,wabeba michanga,tofali,wauza maji mabarabarani,mabaamed wa leo,wafumua vyoo.IN SHORT SI LAZIMA WOTE TUSOME
 
CCM walijikaanga kwa mafuta yao wenyewe walipo ifanyia zengwe hoja ya Mbatia bungeni, laiti bibi kiroboto na Ndugai wangetumia busara ndogo tu leo hii wangekuwa na chakujitetea kwamba jambo hili linafanyiwa utafiti na kamati ya bunge!
 
Uyu mama atahusika tuu kama alitunga mtihani nje ya syllabus otherwise yeye kama yeye hausiki na kufeli kwa vijana wetu
 
From what i heard from some sources, Joyce Ndalichako ndiye "chanzo" cha watoto kufeli coz this time hakukuwa na mitihani iliyoleak..Mitihani ya f4 last year haikuleak even a single paper thats why wale waliozoea kununua paper waliambulia kuandika mistari au kukusanya karatasi tupu. Hii ni hatari sana kwa taifa kama miaka yote watu wamekuwa wakienda vyuoni kwa kununua mitihani... Kwa hiyo mama yetu Ndalichako atakuwa tu mbuzi wa shuhuli coz hakuna waziri anayeelekea kujiuzulu.. Shangaa miaka yote mitihani inaleak but wananchi hawalalamiki, mwaka huu wamebana wananchi mnaandamana.. Jiulize kama mitihani ilitungwa out of syllabus why zile shule zinazoongoza kwa kufanya vizuri still zilifanya vizuri?.. Wanakula pesa ya serikali kuunda tume ni kiini macho tu!
 
Kama kweli tunamlaumu huyu mama kuwa naye anastahili kujiuzulu basi Watanzania uwezo wetu wa kufikiri una walakini. Baraza la Mitihani halina uhusiano na matokeo haya ya kidato cha nne. Wao hutunga na kusahihisha mitihani kadri walivyoelekezwa na wizara ya elimu (mhitasari wa ngazi husika). Kama mitihani ingevuja, basi lawama zingemwendea huyu mama. Fikiria kama ungekuwa wewe umeambiwa kuwa huu ndo mhitasari wa kidato cha nne na ukaombwa kutunga na kusahihisha mitihani hiyo kwa kufuata mwongozo huo (mhitasari) watoto wakafeli, je utalaumiwa hapa kwa lipi? wakati wanafundishwa hukuwepo, wakati wanaandaa mihitasari hiyo hukuwepo, hapo lawama inakuwa yakwako ki vipi?
Nakuunga mkono ndugui yangu.. Unajua kinachowaliza wananchi ni watoto kufeli, ila hawaijui sababu.. Haya yote ni matokeo ya kazi nzuri ya Bi Ndalichako kubana mitihani isivuje.. Mbona kila inapovuja hawalalamiki? sasa mmebaniwa mnalialia. Ndo mjue watoto wenu ni mambumbumbu all these years..
 
Pengine hujanielewa Ndg Nguvukazi mikono, naomba maelezo ya kina. Ndalichako na NECTA yake wamehusika vipi katika kufeli F4 wa 2012? Hao wadau wengine unaowaita serikali kupitia wizara ya elimu ndicho nilichoandika na nikaenda mbali zaidi kwa kuwaangushia lawama pia wazazi na watz wote. Soma tena uzi wangu. Nguvukazi mikono?
Namuonea huruma mama wa watu..Asicheze na wanasiasa watamuumiza.. Mungu atamlipa kwa kazi yake nzuri aliofanya this year..
 
Ndalichako anapaswa kujiudhuru.kwa sababu zifuatazo;kwanza kuna wanafunzi wamepata div three wakati hata mtihani hawakufanya,pia wapo waliopewa alama katika masomo ambayo hawakufanya.mfano mwanafunzi mmoja alipewa c ya biology wakati hakufanya kabisa sayansi.pia kumbuka mwaka jana ktk somo la islamic knowledge nchi nzima kulikuwepo na D saba tu.lkn walipoeuatilia kwa ndalichako alionesha msimamo mpaka walipoamua kuomba script za mitihani ndipo akatoa matokeo upya badala ya script.watu wengi walikua wamepata A,B,na c zakutosha.hivyo anapaswa kuwajibika kwa kua utendaji wake unamashaka.
 
ndalichako na kawambwa waige waziri wa uchukuzi wa zanziber ambae alijiudhuru baada ya ajali ya meli ya mv.skagit.haimani kua yule waziri ndie alikua nahodha au ndie alikatisha tiket ila ni uwajibikaji tu.nawashanga wanaomtetea ndalichako.au mna maslahi nae akiwa pale necta?tujifunze nchi za mbele ambapo kiongozi hujiudhuru hata kama tatizo liko beyond the human control.
 
Yule mama anahusika moja kwa moja na kufeli kwa wingi waliomaliza form four, ilitakiwa aondoke tokea wakati ule wa sakata la Islamic Knowledge jibu lake amelitoa kwenye matokeo ya mitihani ya form four mwaka huu.

Inaonyesha kuwa hayuko peke yake, ni mtandao mpana unaochukua maagizo sehemu fulani afuatiliwe na kila kitu kiwekwe hadharani kama kweli kunatakikana suluhisho la kudumu kuhusu hili tatizo.
 
Back
Top Bottom