Nchi zenye Dhahabu nyingi zaidi duniani

Nchi zenye Dhahabu nyingi zaidi duniani

Dhahabu ni sarafu ya yakihistoria ambayo inakubaliwa popote ulimwenguni bila dhamana ya mtu mwingine. Kwa mfano, dola za Marekani lazima zidhaminiwe na serikali ya Marekani kuwa na thamani ya gharama wakati dhahabu ni ya kinadharia daima yenye thamani ya kitu mahali popote, wakati wowote.

Benki kuu katika nchi na mashirika ya kifedha duniani zinashikilia akiba za dhahabu kama sera ya bima dhidi ya mfumuko wa bei au janga zingine kali za kiuchumi. Dhahabu ni bidhaa inayofuatwa zaidi na kuuzwa Duniani, ambayo inafanya kuwako na soko la pesa kavu ikiwa hatua zinahitajika kusaidia sarafu kubwa. Kwa mfano, kama dola ya Marekani ingepungua sana kwa thamani inayohusiana na sarafu zingine, serikali inaweza kuuza dhahabu kununua dola na kusaidia thamani yake.
 
Pamoja na kwamba Afrika ndiyo bara linaloongoza katika uzalishaji wa dhahabu lakini ndiyo nchi zenye reserve ndogo zaidi ya dhahabu, HOPELESS PEOPLE!!...
 
Dhahabu ni sarafu ya yakihistoria ambayo inakubaliwa popote ulimwenguni bila dhamana ya mtu mwingine. Kwa mfano, dola za Marekani lazima zidhaminiwe na serikali ya Marekani kuwa na thamani ya gharama wakati dhahabu ni ya kinadharia daima yenye thamani ya kitu mahali popote, wakati wowote.

Benki kuu katika nchi na mashirika ya kifedha duniani zinashikilia akiba za dhahabu kama sera ya bima dhidi ya mfumuko wa bei au janga zingine kali za kiuchumi. Dhahabu ni bidhaa inayofuatwa zaidi na kuuzwa Duniani, ambayo inafanya kuwako na soko la pesa kavu ikiwa hatua zinahitajika kusaidia sarafu kubwa. Kwa mfano, kama dola ya Marekani ingepungua sana kwa thamani inayohusiana na sarafu zingine, serikali inaweza kuuza dhahabu kununua dola na kusaidia thamani yake.
Sasa Afrika tungekuwa tuna hifadhi dhahabu si ingetusaidia sana hasa ukizingatia currency za Afrika hazipo stable..
 
Dhahabu au almasi zinatumika kama pesa... Mataifa mbalimbali wabahifadhi dhahabu kwenye hazina badala ya pesa..

Na hii ni kwa sbbu madini hayo hayashuki thaman kama vile pesa zinaposhuka..

Note:
Naweza nisiwe sahihi kwa maelezo.. Lakin aidia ni hyo
Hivi, kazi ya dhahabu ni gani
 
Hivi, kazi ya dhahabu ni gani

Umeshawahi jifunza kuhusu REAL MONEY?

Dhahabu ndiyo pesa, tumeaminishwa zaidi pesa ni hizi karatasi, kama dhahabu ingekuwa kwenye mzunguko kuna watu tusingekuwa hata na chenga yake. [emoji1][emoji1][emoji1]

Pia kama dhahabu ingalikuwa kwenye mzunguko, thamani ya pesa duniani ingekuwa mojaa, je ushindani ungekuwa wapi? Taifa gani lingetawala taifa lingine?
 
Pamoja na kwamba Afrika ndiyo bara linaloongoza katika uzalishaji wa dhahabu lakini ndiyo nchi zenye reserve ndogo zaidi ya dhahabu, HOPELESS PEOPLE!!...
Sasa tutunze wakati hata kazi yake hatujui si bora tuuze tu tufanye mambo mengine[emoji3][emoji3].
 
Hivi, kazi ya dhahabu ni gani

IMG_7249.jpg
 
Dhahabu ina thamani ya kihistoria na imekuwa juu kwa sababu, kwa miaka mingi sana imetumika kama "store of value" na watu wamejaribu kuitengeneneza kwenye lab wakashindwa. Hivyo pure gold ina a measure of authenticity. You just can't fake it, as in create it in a lab.

Ukisoma historia ya Chemistry, enzi za Alchemy, watu walijaribu kila njia kutengeneza dhahabu wakashindwa.

Na hii inatokana nabsababu kubwa mbili. Kwanza, dhahabu hai react na vitu vingine. Pili, namna pekee ya kuitengeneza dhahabu ni kutumia nuclear reactions zenye nishati kubwa sana kiasi gharama za kuitengeneza hiyo dhahabu zitaizidi thamani ya dhahabu itakayotengenezwa. Hivyo hiyo itakuwa biashara kichaa. Dhahabu tuliyonayo ilitengenezwa katika nuclear reactions katika nyota mbalimbali ambazo ziliishia katika kupasuka kwenye supernovae.

Tabia hizi mbili za dhahabu za kuto react na vitu vingine (ukilinganisha na kitu kama chuma kinacho oxidize na kupata kutu), pamoja na kutoweza kutengenezeka kwenye lab, pamoja na thamani ya kihistoria kama "store of value" (kihistoria fedha zilihesabiwa kwa dhahabu na chumi nyingi za dunia zilitumia "the gold standard" mpaka karne iliyopita.

Kuna mengi mengine ambayo yanahusika, lakini kwa uchache kabisa hayo ni ya muhimu.
Safi sana
 
Asilimia kadhaa ya Dhahabu hiyo inatoka Afrika na hakuna nchi hata moja ya Afrika kwenye orodha
Wao wanatusaidia kupigania democracy na kutusambazia silaha ili tuasi nchi zetu (silaha zenyewe ni outdated technology) kisha sisi tunawaachia migodi wanachimba dhahabu ndio maana wanazo nyingi kuliko sisi mkuu.
 
Wao wanatusaidia kupigania democracy na kutusambazia silaha ili tuasi nchi zetu (silaha zenyewe ni outdated technology) kisha sisi tunawaachia migodi wanachimba dhahabu ndio maana wanazo nyingi kuliko sisi mkuu.
Shida kubwa ni sisi na si wao. Akili ndio zimetupungukia kwa hizi mali tungetakiwa kutawala dunia
 
Shida kubwa ni sisi na si wao. Akili ndio zimetupungukia kwa hizi mali tungetakiwa kutawala dunia
Mimi nasema shida ni wao sio sisi, kwasababu wao ndio chanzo Cha machafuko kwenye kila nchi yenye rasilimali wanayoitaka Africa pindi anapotokea kiongozi mzuri wa kuwapinga tu basi tegemea taifa hilo litaingia kwenye machafuko makubwa kisha mali zote kukombwa.

Mfano Mzuri ni hapo tu Congo walipoona Lumumba hadanganyiki haraka sana wakamuua Kisha kuweka puppet wao Mobutu na vikundi vya waasi kibao huku wao wanajizolea madini yote.
Yaani Africa akipatikana tu kiongozi mzuri wa kusimamia masilahi ya waafrica basi lazima tu atapata msuko suko mkubwa wa kutengenezwa kwa makusudi kabisa.
 
Back
Top Bottom