Nchi yetu inaitwa Tanganyika

Ah ah unajua kuwa ata zanzibar ni muungano wa sehemu mbili?Zanzibar imeundwa na Unguja na Pemba then Tanzania=Tanganyika+Unguja+Pemba au inakuaje? 1964 Tanganyika +Zanzibar=Tanzania sasa nchi ya Tanzania bara ilitoka wapi?Then kama imeanza 1977 bado haijafikisha 50yrs na hapo muungano Tanganyika na Zanzibar basi ulivunjika 1977 then ukaanza wa Tanzania bara na Zanzibar then hiyo tz bara nani aliiunda na hiko wapi ana its government???
 
Tanganyika + Zanzibar = Tanzania govt + Zanzibar govt
Nahisi hesabu haziko sawa hapa! Tanganyika imepotelea wapi?
 
turudishe tananyika ye2 ili kuharakisha maendeleo ye2 kuliko kukaa na wa2 tusioaminiana,pia itatusaidia kufanya mabadiliko ya kisiasa si unaona CUF wanavyoturudisha nyuma na ndoa yao na ccm kule znz.Watanganyika na znz hakuna usawa na watanganyika ndio wanaoonewa sana jiulize nani anaepanga mambo ye2,mbona mambo ya znz yanapangwa kivyao nabunge lao alafu wanaingia bunge la muungano na kuamua ya kwe2 pia.Mbona hakuna mbara anaepewa madaraka znz,wakati wao wanatawala na kua mawaziri huku bara.Its time to stop this nonsense,turudishe tanganyika ye2
 
Bendera yako hii Tanganyika ilikuwa na uzuri wa pekee, lakini wewe ukauawa na yenyewe ikapotezwa, ikazaliwa Tanzania. Hilo kwangu si tatizo, lakini kinachonisikitisha na kuniliza sana ni ile siku ya uhuru wako inayoadhimishwa kila mwaka, na hasa mwaka huu unapotimiza miaka 50 kubatizwa jina jipya , eti ni Siku ya Uhuru wa Tanzania Bara...Wanaoimba wimbo huo wanajua fika kuwa wakati Mama yangu Tanganyika unapata uhuru Desemba 9, 1961 Tanzania ilikuwa haijazaliwa. Wanajua kuwa mwaka huu 2011 Tanzania (iwe bara au visiwani) haitakuwa imetimiza miaka 50.

Ninakulilia sana Mama yangu Tanganyika. Hata kama umekufa, ukazikwa, waliofanya hicho kitendo watambue basi kwamba ulikuwapo na ulikuwa mama yetu kweli.

 

Attachments

  • Tanganyika.jpg
    2.5 KB · Views: 30
sasa Mpwa si ndio miruko yenyewe hiyo jamani? usilie na mie utaniliza Mpwa tukose wa kumbembeleza mwenzie.....yana mwisho tumedhulumiwa haki yetu ya utambulisho kama watanganyika, naelewa sana maumivu yako ni kama yangu.
 
haha mnaona sasa munajikanyaga,sasa hivi media zinasema munasherekea uhuru wa tanzania bara,hahaha uhuru huo mumeupata wapi wa tanzania bara ? inamana nyie ni wabara. au watanganyika ?
 
Kifuu cha nazi wewe hahaha.

zanzibar haijaundwa na muungano wewe,unajua history ya zanzibar ? angalia ramani yake hapo katika picha yangu,ilivyo tawala kabla halijaundwa taifa la watanganika,wala south africa,wala zimbabwe,wala somali,wala kenya na nyengine,,,kifuu kasome history ndio uwongee
 
Mbona hizi sherehe za miaka 50 hawasemi "kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika?" Nadhani hapa hata wao wanashangaa. Kama tuliungana ya nini tena kila nchi inasherehekea kivyake? Hili kweli changa la macho!
 
Nchi yetu yaitwa Tanganyika. period! Uhuru wa Tanzania bara watausherehekea watanzania bara kama Dr. Bilal, Dr. Hussein Mwinyi, Shamsi Nahodha, Balozi Seif Idd, Maalim S. S. Hamad na wengine wenye kufaa katika kada hiyo.
 

Jamani mara nyingi tunapenda ku externalize our own faults!! msiwalaumu Wazanzibari kwani ni sisi wenyewe tumeiua Tanganyika! mie naona wenzetu wako safi bila unafiki ndio maana yule kiongozi wa maimam kule zaenji alichana ule waraka wa Katiba mbele ya Kombani na Sita na akatamka wazii leteni katiba ya Tanganyika kwanza ndio tuongelee muungano!!! Iko wapi tanganyika???? wacha watuite wabara kwa uzandiki na unafiki wetu
 


Wewe una akili kuliko Nyerere si hawa wapumbavu wengine wanaandika Nyerere kasema hivi Nyerere kasema vile Kwani Nyerere ni nani hata akawa hakosei kuweni na akili za karne mpya musiwe wapumbavu wa kuburuzwa tu
 

Aliuliza, "mmeshafanya ya Tanganyika?"
 
Katika kuelekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika ningefurahi kuona ile bendera yetu ya Tanganyika nayo walau ipepee ili kuweka kumbukumbu sawa
 
Hapana sisi sio watanganyika kwa kuwa Tanganyika ilikufa toka tarehe 26 aprili 64, hata kama wao ni waznz sisi ni watz tu, tuidumishe tz hata bila znz.

Nchi hii kuna watanganyika na wazanzibari. Kwa hili nadhani wazanzibari wametushinda uelewa kwa kiasi kikubwa. Ni dhana potofu kuamini kuwa Tanganyika imekufa na haipo tena kwani Tanzania ni muunganiko wa Tanganyika na Zanzibar. Bila Tanganyika Tanzania haipo kama ambavyo bila Zanzibar Tanzania haipo.
 
oooh my tanganyika Ilove you from the bottom of my heart, we want our tanganyika back, we need our flag with our Tanganyika national antherm, if zanzibar they have theirs what about us. IM NOT A TANZANIAN I AM A TANGANYIKAN.
 

sasa mbona zanzibar na wazanzibari wana haki ya kujiita hivyo ndani ya muungano wakati sisi Watanganyika hatuwezi? BIG B.S!!!!!
 
sasa mbona zanzibar na wazanzibari wana haki ya kujiita hivyo ndani ya muungano wakati sisi Watanganyika hatuwezi? BIG B.S!!!!!

wewe tu ndio huwezi kujiita hivyo lakini kwetu sisi nchi yetu inaitwa Tanganyika na sisi ni Watanganyika asilia...
 
Sasa wakati umekaria kupigwa changa la macho. watanganyika kuweni macho. Katiba ya jamuhuri ya Muungano isijadili mambo ya muungano?
 
Kuna kila dalili kuwa Tanganyika ipo mbioni yaja! ati kuna wazenji wamepeleka ajenda ya kujitenga UN. Kuna haja gani kwenda UN? Tukiitisha kura ya maoni upande wowote wa muungano uamuzi utakuwa kujitenga tu. Tanganyika oyeeee!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…